Kuna urafiki mkubwa Kati ya pesa na matatizo

Kuna urafiki mkubwa Kati ya pesa na matatizo

sepema

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2019
Posts
603
Reaction score
1,011
Heshima kwenu wakuu...

Napata shida Sana kwenye kuelewa hili Jambo.Binafsi nafanya shughuli ambazo malipo yake ni ya mwisho wa mwez.

Napanga bajeti zangu vizuri kuwa nikipokea pesa nitafanya jambo flani Ila Cha ajabu kila ikifika karibu na huo mshahara lazima litokee jambo au tukio linalohitaji nusu au zaidi ya nusu yakipato changu. Baada ya mshahara (ukiisha),hakuna tatizo lolote linalojitokeza linalohitaji pesa.

Hili swala nikwangu tu ama matatizo yakigundua unavipesa nayo yanaibuka kutoka huko yalipokua?
 
Heshima kwenu wakuu...

Napata shida Sana kwenye kuelewa hili Jambo.Binafsi nafanya shughuli ambazo malipo yake ni ya mwisho wa mwezi...
Hela ya mshahara ni kwa ajili ya chakula, kulipa kodi na usafiri tu, ukitaka kufanya maendeleo hakikisha unakuwa na vyanzo vingine vya kukuingizia pesa kama biashara

NB: Pia kuna kanuni inasema matumizi hijitahidi kujiinua ili yakutane na kipato chako, ndio maana unaweza kusema kama mshahara utaongezeka au kama nitapata mshahara kiasi fulani sehemu nyingine mambo yatakuwa safi lakini,utaona bado hautoshi
 
Nina waza kwa namna tofauti kidogo.

Huenda katika harakati zako uliwahi kujipatia riziki kwa njia isiyostahili na kusababisha masononeko kwa mtu mwingine. Ni aidha upatane naye kama unamjua au ufanye ibada ya toba(kwa imani yako). Ikibidi toa sadaka ili maombi yako yaweze kupokelewa.

Upande mwingine ni kwamba inawezekana una moyo wenye huruma kiasi cha kuchukulia kila tatizo la watu walio karibu nawe kama yako.

Unapata amani kwa kujitolea kwakk, lakini unabaki na maumivu .

Kumbuka, matatizo hayaishi kwa jamii kwani kila mtu na msalaba wake, pia kuna watu wazuri sana wa kufanyia hesabu ya pesa za wenzao. Hivyo kila ukikaribia mwisho wa mwezi utatungiwa matatizo kiasi kwamba miezi ambayo hujapata majanga hayo itakuwa ya kufukia mashimo uliyobaki nayo miezi iliyotangulia.
 
Matatizo gani yanayikukuta wakati salary ikikaribia isijekuwa ni kuzidisha kiwango cha bia ukaandikiwa deni
 
Heshima kwenu wakuu...

Napata shida Sana kwenye kuelewa hili Jambo.Binafsi nafanya shughuli ambazo malipo yake ni ya mwisho wa mwez.

Napanga bajeti zangu vizuri kuwa nikipokea pesa nitafanya jambo flani Ila Cha ajabu kila ikifika karibu na huo mshahara lazima litokee jambo au tukio linalohitaji nusu au zaidi ya nusu yakipato changu. Baada ya mshahara (ukiisha),hakuna tatizo lolote linalojitokeza linalohitaji pesa.

Hili swala nikwangu tu ama matatizo yakigundua unavipesa nayo yanaibuka kutoka huko yalipokua?
Fanya kitu,
 
Hela ya mshahara ni kwa ajili ya chakula, kulipa kodi na usafiri tu, ukitaka kufanya maendeleo hakikisha unakuwa na vyanzo vingine vya kukuingizia pesa kama biashara
Hii ni hata kwa mtu anaechukua mshahara wa mil 15 kwa mwezi au
 
Back
Top Bottom