Kuna ugomvi wa chini chini India dhidi ya Tanzania?

Kuna ugomvi wa chini chini India dhidi ya Tanzania?

Zitto

Former MP Kigoma Urban
Joined
Mar 2, 2007
Posts
1,562
Reaction score
10,890
Kuna nini Tanzania na India

Kwenye ziara tunayotembelea madiwani wetu wa ACT Wazalendo kuna jambo nimeliona linajitokeza mahala pengi kila ninapoongea na Wananchi. Jambo hilo ni kushuka kwa bei za mazao ambayo Wakulima walikuwa wanategemea soko la India. Mbaazi, Choroko, Dengu na giligilani ni baadhi ya mazao ambayo nimesikia malalamiko makubwa ya bei zake.

Jana nilipokuwa Sumbugu, Misungwi Wananchi walinieleza kuwa mwaka 2016 waliuza choroko kwa shilingi 300,000 kwa gunia Lakini bei hiyo ilishuka mpaka shilingi 150,000 na kwamba wanunuzi wamepungua mno. Vile vile Dengu imeshuka sana bei kutoka shilingi 7000 kwa kilo 4 hadi kufikia shilingi 2500.

Nilipokuwa Gehandu, Hanang nilielezwa kuwa bei ya giligilani imeshuka kutoka shilingi 150,000 kwa gunia mpaka shilingi 25,000 tu.

Chama chetu kilifanya utafiti wa zao la mbaazi kwa mikoa ya kusini mwaka Jana. Kadhia ya mbaazi tumeikuta pia Mkuranga, Morogoro na Mkoa wa Manyara. Bei imeshuka kutoka wastani wa shilingi 1500 kwa kilo mpaka shilingi 50 kwa kilo na maeneo mengine hakuna soko kabisa.

Swali
Mazao yote haya yaliuzwa India. Kwanini Bei zimeshuka na masoko kuanguka kabisa wakati mahitaji ya bidhaa hizi huko india yanakua mwaka hadi mwaka? Kuna nini kati ya Tanzania na India? Kuna nini Wakulima na Watanzania hawaelezwi?
 
Pia tungejaribu kuangalia kuanguka kwa mazao kama Nazi, kahawa na pamba enzi zile nini kilisababisha ndo iwe kama literature review zetu then sasa tutajua why now mazao haya. Unajua enzi zile sisi tulikua ndo wauzaji wakubwa wa bidhaa nlizotaja mpk zikapelekea baadhi ya nchi ikiwemo uarabuni kugombea kututawala lakini baada ya miaka kadhaa mbele zimekua sio kitu so yaezekana sababu iliyoiangusha bidhaa zile ndo the same zinayoitenda bidhaa hizi
 
Rais amelala usingizi wa nusu kaputi kuhusu shida halisi za watanzania, na akikurupuka kutoka usingizini basi ni kufukuza watendaji wake, kununua na kuwaangamiza wapinzani na mwisho kuvamia bandarini na kujidai kukamata cargo zilizoagizwa na taasisi za serikali.

Mawaziri nao wamekuwa kama kuku wa kienyeji, kutwa kuzurura ovyo na kudokoa dokoa (kutatua shida ndogo ndogo za mwananchi mmoja mmoja na hapo hapo kuwaadhibu watumishi wa umma) na mwisho wanawika kama kuku (Wanaropoka matamko yasiyokuwa na kichwa wala mkia ili kutafuta kick).

Serikali imepoteza mwelekeo.
Taifa limepoteza mwelekeo.
Nchi inazidi kuangamia kwa kasi.
 
Kwanza maajenti wakubwa wa makampuni ya India yanayonunua haya mazao ni hawa wafanyabiashara wetu hapa Bongo kama kina Manji, Mo and the likes. Kitendo cha kuwa destabilize wao, kunawafanya kutopromiti effectively hayo mazao India kwa wateja wao. Kumbuka Marketing in the competitive world is a continue issue. WAMESUSA.

Pili. Serikali kuingilia ingilia biashara na kufikiri kuongea na serikali ya India ndo kutafanya hao wafanyabiashara wanunue. NOPE!!! Mahusiano ni kati ya biashara na biashara. Serikali ya India haina kiwanda wala duka.

Sisi wa alizeti, hata mashudu hayaendi tena India.Halaf diplomasia inainua biashara sana. Tena kwa impact kubwa. Mkuu wa nchi anapotoka yeye mwenyewe kwenda kwa mkuu wa nchi nyingine kuyajenga inashawishi kiheshima zaidi kuliko kutuma tuma watu walio chini yake. JUST THINKING LOUD!!
 
Ingawa wahindi wanadharau lakini kwenye serikali hii Kuna mengine wanawafanyia kwa uonevu, mtu kapewa tenda ya kushona sare za jesho, unamwambia muhujumu uchumi, aliyekula pesa za escrow wanajulikana anakamatwa singa singa peke yake
 
serikali ikapiga marufuku kuuza mahindi wakati uwezo wa kuyanunua hawana Magufuli na genge lake wameleta siasa kwenye maisha ya mkulima tena wanajibu kwa viburi na dharau na kusema wanayojisikia leo hii umenitonesha kidonda basi tu.
 
Back
Top Bottom