Kuna tofauti kubwa kati ya Masaki niliyoishi mimi na Masaki ya leo

THE BOILER ROOM

JF-Expert Member
Sep 17, 2018
1,054
3,210
Kwanza kabisa naomba mnisamehe kama Uzi wangu unaofanania na kudhihaki ila hii si shabaha yangu!Shabaha yangu kubwa ni kutoa taswira ya namna mabadiliko ya matumizi ya ardhi ya maeneo husika yalivyotofautiana sana na mpango wa awali wa matumizi ya ardhi ya maeneo hayo kabla;

Enzi hizo wakati naishi mimi:
Masaki ilikuwa ni Residential Area pekee huwezi kuta ofisi yoyote iwe ya serikali au taasisi binafsi ikifanya shughuli zake maeneo hayo.

Miaka hiyo Masaki huwezi kuta jengo lenye urefu wa ghorofa zaidi ya ghorofa tatu kwa uchache na upekee wake utakutana na mazingira ya namna hiyo kwny maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya flats yakiwemo maeneo kama ya TIB,THB na kule Harbors.

Masaki ya wakati huo wahudumu walikuwa hawarudi makwao zaidi ya kuishi kwenye nyumba za servants zilizokuwa nyuma ya nyumba kubwa za maboss wao

Wakati huo Masaki huwezi kuta watu wakiwa wamezagaa zagaa hovyo asilimia kubwa kwenye mtaa husika watu tulikuwa tukifahamiana kwa sura hata kama tulikuwa hatusalimiani.

Kwa kifupi mimi nimeishi na kukua kwenye mtaa wa Haile Selassie.
 
Tanzania Urban Planning ni changamoto Kubwa sana. Mfano states kuna hood ni dry town alcohol hairusiwi kuuzwa na ofisi hazitakiwi ila Tanzania mtu anajisikia sehemu yeyote kufungua bar au guest katikati ya makazi ya watu, mara kuna kanisa la walokole kila ijumaa wanakesha ni makelele mtindo mmoja, mara utakuta shule ya nursery, ni kama tunaishi porin ambapo hakuna utaratibu yaan ni vuruguvurugu.
 
Masak naona imeanza kuwa uswazi, na mdogo mdogo inaanza kuwa ya kawaida saana, yani saana...

Bar na restaurants nyingi, na security ya premier residential inaondoka kwa kuwa na maghorofa yenye watu wengi sana, lakini zaid nyumba za ghorofa kumi kuendelea zinaongezeka sana.. soon itaanza fanana na Kariakoo.

Security kwa premier residential services ni priority... sasa hapa bungalow hapa ghorofa lenye apartments 40.

Hapo sijazungumzia frame na viduka uchwara.... hadi mama ntilie
 
Enzi hizo masaki ikiitwa, kichangachui ilikuwa ukitaka kufanya shopping kuanzia oysterbay kule ubalozi wa marekani hadi kichangachui ( masaki) unaenda Morogoro store unapata mahitaji yako yote hapo plus huduma za posta.

Petrol station ( sheli) ikiwa kando yake, yatch club ikiwa pale msasani peninsular na Oysterbay hotel kule coco beach kwa ajili ya starehe Mitaa yote ilikuwa tulivu kabisa nyumba zimetengana kwa michongoma tu Enzi hizo mbawala wakikamatwa kichangachui.

Kweli enzi hazirudi
 
Yalibadilikaje Mkuu Unaweza kutoa Maelezo Tuelewe,Miaka Hiyo hatukuwepo Wengine au tulikuwa wadogo sana
Mfano, Kuanzia pale Mfugale kwenda ubungo maziwa mitaa iliyopo Hostel mpaka kambi ya jeshi kuja Kibangu mpaka Kisukulu watu walikuwa wachache na wanafahamiana, mitaa ilikuwa misafi kiasi fulani na nyumba zilikuwa mbalimbali. Ubungo haikuwa uswahilini.
 
Tanzania miji na mitaa mingi inachakaa badala ya kupendeza kuendana na ukisasa. Kwa wale tulioishi Ubungo miaka ya 90 wanaelewa hili, maaisha yalianza kubadilika baada ya kuja kwa Mabibo Hostel.
Mabibo hostel ilianza1998 kama sikosei,Ila ujue ubungo mi kubwa Sana,kibangu,maziwa,kibo,msewe,shekilango NHC,urafiki,mabibo hostel imeafect sehemu ndogo ya ubungo
 
Iko hivi miji inatanuka masaki ya zamani au sinza ya zamani au kinondoni ya zamani sio ya sasa hiviipo hivi watu wanahamia na watu wanaondoka kwaiyo miaka 20 ijayo masaki itakuwa ya kawaida kama sinza ya zamani kwaiyo mji mwingine utaibuka kuwa wakishua maana siku hizi wengi wanaamia kigamboni uko kuna mijengo ya maana au bagamoyo siku hizi mjini kuna makelele sana
 
Tanzania hatuna mipango Miji sikuhizi hamna tofauti ya makazi ya watu,soko, makazi ya watu yamezungukwa na bar na Kila mtu kwenye nyumba yake anajenga fremu tu.

In short sikuhizi makazi mazuri ya watu hamna, na hata aliyeanzisha wazo la fremu na wote kuiga sijui nani Yani fremu nyingi kuliko wateja
 
Masaki ya leo sio ile tulivu ya kishua tena, limebaki jina tu.

Kuna ushamba katikati umetokea ata upanga wakati sisi tunakuwa yalikuwa maeneo ya wafanyakazi wa serikali wenye kipato cha kawaida hasa walimu. Eti siku hizi prime areas.

Yaani watu badala ya kutanua jiji wamevunja na kujenga maeneo hayo hayo machache na kuharibu mandhari ya maeneo; masaki kuna maeneo nilipita nikawa najiuliza hivi ndio hapa kweli ata kilima nyege sikukitambua niliposhuka kwa kushangaa.
 
Trend ya miji ya Kibongo ni kwamba pesa ikifumuka watu wanaanzisha ka-mji ka kishua wanafunga kuta na mageti makali. Watoto wanalelewa kishua kila kitu kipo.

Wazazi Wakizeeka na kuaga dunia watoto wanaishi kwenye majumba mazuri lakini ukute hawana kipato.

Mwisho wa siku wanauza majumba au wanaishi humo wakiendesha biashara haramu nao wanaaga dunia nyumba zinakaliwa na wajomba na mashamgazi ndo hao mnaowaona Masaki.
 
Back
Top Bottom