Zero IQ
JF-Expert Member
- Dec 21, 2016
- 13,917
- 24,674
Kuna maswali mengi sana wanadamu tunajiuliza mengine yana majibu na mengine yanakosa majibu sana sana maswali yale ya kiimani zaidi.
KIFO _Kuna maandiko yanasema kila kilicho na Uhai basi siku zake za kuishi zinaesabika hapo haijarishi ni binadamu,Mmea au mnyama basi chochote chenye uhai ni lazima kife na hapo ndio tunapata neno kifo.
Kifo kililetwa na nani? Na kwa nini kuna kifo? na baada ya kifo kile kilichokufa kinaenda wapi? kuna siri gani kwenye kifo?
Hayo ni baadhi ya maswali ambayo ukiuliza baadhi ya wanazuoni kila mmoja atakupa jibu lake hii ina maana hakuna jibu la moja kwa moja kuhusu kifo,
Lakini leo tujadili Swali hili ,
Je Ukifa unaenda wapi?
Ukija kwenye imani za dini wanasema kinachokufa ni mwili lakini Roho inabaki hai na hiyo uchukuliwa mpaka mbinguni ambako kuna hukumu kama ulitenda mema basi Roho yako itaingia kwenye Raha ya milele ila kama ulitenda Dhambi Roho yako itatupwa Motoni.
Lakini pia ukija kwenye upande wa wale wasio na imani watakujibu kwamba kifo hakitenganishi Mwili na Roho bali ukifa Umekufa hakuna kingine kinachoendelea juu yako.
Kutokana na majibu hayo hapo juu hauwezi kujua yupi yuko sahihi kwa sababu hakuna ithibati iliyowahi kusibitisha kwamba kuna maisha mengine baada ya kifo.
Nami nisiwakatishe Tamaa au kuwaingiza uoga mioyoni mwenu ila Kifo hakina budi kuheshimiwa kwa sababu kila aliye na uhai ni lazima atakufa tu.
Ukitaka kujua ukifa unaenda wapi basi jaribu kufikiria kabla ya kuzaliwa kwako wewe ulikuwa wapi?
Na ndivyo hivyo Kifo kitakavyokuwa baada ya kifo Chako.
_Jf Mtawangu.
KIFO _Kuna maandiko yanasema kila kilicho na Uhai basi siku zake za kuishi zinaesabika hapo haijarishi ni binadamu,Mmea au mnyama basi chochote chenye uhai ni lazima kife na hapo ndio tunapata neno kifo.
Kifo kililetwa na nani? Na kwa nini kuna kifo? na baada ya kifo kile kilichokufa kinaenda wapi? kuna siri gani kwenye kifo?
Hayo ni baadhi ya maswali ambayo ukiuliza baadhi ya wanazuoni kila mmoja atakupa jibu lake hii ina maana hakuna jibu la moja kwa moja kuhusu kifo,
Lakini leo tujadili Swali hili ,
Je Ukifa unaenda wapi?
Ukija kwenye imani za dini wanasema kinachokufa ni mwili lakini Roho inabaki hai na hiyo uchukuliwa mpaka mbinguni ambako kuna hukumu kama ulitenda mema basi Roho yako itaingia kwenye Raha ya milele ila kama ulitenda Dhambi Roho yako itatupwa Motoni.
Lakini pia ukija kwenye upande wa wale wasio na imani watakujibu kwamba kifo hakitenganishi Mwili na Roho bali ukifa Umekufa hakuna kingine kinachoendelea juu yako.
Kutokana na majibu hayo hapo juu hauwezi kujua yupi yuko sahihi kwa sababu hakuna ithibati iliyowahi kusibitisha kwamba kuna maisha mengine baada ya kifo.
Nami nisiwakatishe Tamaa au kuwaingiza uoga mioyoni mwenu ila Kifo hakina budi kuheshimiwa kwa sababu kila aliye na uhai ni lazima atakufa tu.
Ukitaka kujua ukifa unaenda wapi basi jaribu kufikiria kabla ya kuzaliwa kwako wewe ulikuwa wapi?
Na ndivyo hivyo Kifo kitakavyokuwa baada ya kifo Chako.
_Jf Mtawangu.