Kuna nini katikati ya mbuga ya Serengeti?

Kuna nini katikati ya mbuga ya Serengeti?

jerryempire

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
5,830
Reaction score
10,089
Mambo vipi wadau,

Niende moja kwa moja kwenye swali ambalo huwa najiuliza sana lakini mpaka sasa sijapata majibu ya kueleweka au ya moja kwa moja.

Huenda kuna maeneo mengi sana duniani ambayo mpaka leo ambayo hayaruhusiwi kabisa kuingia ama kuyasogelea duniani unayoyajua kama area 51 nk.

Je unafahamu kuwa kuna eneo ndani ya Tanzania katika hifadhi ya taifa ya serengeti ambayo hakuna mtu yoyote anayeruhusiwa kuingia ama kusogelea?

Ni takribani mwezi toka nitembelee mbuga hiyo kwa mara ya kwanza katika maisha yangu (baada ya rafiki zangu kutoka Norway kutaka niwapeleke)

Nilijitahidi sana kutaka kujua kuhusu eneo hilo lakini nilichoambulia ni kufikishwa kwenye fensi ya kwanza tu ya eneo husika ambayo ni restricted kusogea zaidi ya hapo na hakuna kiunzi kimoja.

Kwenye kutafiti kwa ma guider wengi nao walikuwa watupu kila unae muuliza anakupa story tofauti je kuna ambae anajua katikati ya hifadhi ya taifa ya serengeti kuna nini atujulishe huenda humu ikawa rahisi sababu hatujuani?

Maana ni eneo ambalo hata kwenye google map limefutwa na kuna ulinzi mkali mno

Reason ya kuuliza na kutaka kujua ni kupenda kujifunza mambo mampya na si vinginevyo
 
Kuna tende zimefichwa humo
Umerusha jiwe kwenye mzinga wa nyuki. Wakija wahusika hapatakalika hapa.
20250515_074959.jpg
 
Kuna uzi ulishawahi kuletwa humu kuhusiana na eneo hilo, kwa mujibu wa mleta mada alisema eneo hilo kuna hazina kubwa sana ya madini imegunduliwa (dhahabu au almasi) sikumbuki vizuri. Yanasafirishwa kwenda nje ya nchi. Tanzania hatuna chetu hapo pashauzwa kitambo sana.

Hiyo ni kwamujibu wa mleta mada
 
Back
Top Bottom