Kuna mzimu gani CCM?

mzimu wenyewe unaitwa "Njaa"

Chadema wana viroja sana
 
HIV kizazi Cha huyu mchawi forozo ganze kipo wapi hebu wajuzi wa Mambo tuchambulieni huyu kiumbe maana ndio alioshikilia dumba ya ccm inatakiwa kizazi Cha Sasa kinachotegemewa kuleta mabadiliko watambue kwa kina juu ya Mambo haya
 
Ikulu ni taasisi hivyo ukiingia pale unafuata unavyowekewa mezani bila hivyo .......
R.i.p magu
 
mataifa yote duniani hufanyiwa matambiko bt hakuna ujinga kama unaofanywa na ccm, mzimu unaowasumbua ccm ni ulafi wa madaraka na ubinafsi.
Hapa nakubali.We check kwa mfano ualimu ndio utoa viongozi wa juu wengi kila awamu lakini wakishapata tu nafasi ni ngumu Sana kuwakumbuka walimu wenzao.
 
Juzi walikua wanashangilia JPM kuondoka leo wanasema heri JPM

Sijui wako serious wapi hawa watu
Hakuna wanasiasa waongo, wenye uchu wa pesa na wanafiki kama hawa wa chadema. Wanachama wao wanawapambania wao, huku wao wanapambania matumbo yao. Just imagine..

 
Umeongea mambo magumu
 
Kuna jambo nyeti na zito sana huwa halisemwi, kuna mtu amezungumzia deep state ambayo nayo sio hii tunayoifikiria... Jambo hili ni zito sana, JK alijaribu kutaka kulivagaa kilichotaka kumkuta ikabidi awe mpole aende mdogo mdogo amalize nngwe yake.....yupo mtu humu anajaribu sana kulizungumzia sana lakini tunamdharau na kumuona taahira...kujinasua kwenye hiyo minyororo ni kazi ngumu sana maana tayari makosa yalianzia awamu ya kwanza...

TANZANIA ni moja na wote ni watanzania na siku tukiuweka utanzania mbele na kuanza kufanya mambo na kupendana kama watanzania kutoka tanzania bila kuangalia factors nyingine tunaweza kujinasua japo vita yake itakuwa ngumu....macho yakawaida hayaoni mambo mengi sana
 
Mara tu bunge LA katiba lilipopiga kura kuamua kupinga kura za siri mapendekezo ya kanuni,nikajua kwamba mchakato umeingiliwa na hofu kwamba mapendekezo yatapita kwa manufaa ya wanaotaka serkali tatu na tume huru ya uchaguzi.Umhimu was kura za siri ni kumshirikisha Mungu kupitia consciousness ya mtu binafsi pasipokuingiliwa.Mi naamini katiba mpya na bora itakuwa na manufaa kwa watu wote na vyama vyote
 
Kajima pia kakwama unazani mchezo!? Ukishakuwa ndani ya kibuyu utaonaje nje sasa
 
Mzimu wa CCM kizazi hiki cha dot com kizazi laini hakiwezi kuondoa huo mzimu.

Labda mbeleni huko ila kwa nyinyi wa sasa mmelegea sana.
Hebu tujulishe kidogo kwanini ukishaondoka kwenye mfumo wa ccm unakufa?
 
CCM ndio tatizo la Tanzania.
 
Hiyo ndio maana ya mfumo, ni mkubwa kuliko mtu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…