JOKA55
Senior Member
- Nov 1, 2014
- 110
- 74
Heshima kwenu wanajamvi
Napenda kuleta kwenu hii hoja tusaidiane kuelimishana,
Nimesoma na jamaa mmoja kwa sasa ni Padre wa Shirika fulani ndani ya Kanisa Katoliki, huyu bwana kipindi tuko shule hakua mwanadini sana wala hata katika siasa hakuwa mpenzi sana yeye alikua mtu mkimya ila akiamua alikua na vichekesho sana.
Baada ya kumaliza form 6 kila mtu alishangaa kusikia eti jamaa huyu kaenda kusomea upadre, miaka mingi ilipita na jamaa huyu alienda kusoma nchi mbalimbali kwani hilo shirika alilojiunga linafanya kazi karibu dunia nzima. Miaka kama 7 iliyopita huyu jamaa alimaliza masomo yake na kupadrishwa, kama kawaida baadhi ya wanadarasa wake tulikuwepo siku ya upadrisho wake kushuhudi na kushangaa jinsi huyu bwana alivyoamua na kusimamia maamuzi yake ya kuwa mtumishi wa Mungu.
Sasa kitu kinachonishangaza kwa sasa Padre huyu ni mpenzi wa siasa sana na wakati mwingine anafahamu matukio serikalini kana kwamba naye ni mfanyakazi wa serikali. Kwa mfano safari nyingi za viogozi wa serikali anazifahamu kabla na ukifuatilia utakuta ni kweli. Safari za raisi zote anazo kabla hata hazijafika, siri nyingi za serkali anazo, mfano ishu ya Kagame kusarender anaijua vizuri sana. Jinsi Mama Banda alivyokuja kushtuka kuwa ramani zote na mahali silaha za nchi yake zilipo hata zile alizozania ni siri Watz wanazo, kwamba kumbe hata baadhi ya madreva wa malori kwenda nchi za jirani ni watu wa usalama
Biography za viongozi wa serikali ndo basi tena, karibia viogozi wote wa serikali anafahamu makabila yao, sehemu walikosoma, marafiki zao, wengine hata aina ya vinywaji wanavyopendelea. Hapa nilipo ni jiji na vikao vingi vya kiserikali huyu bwana anaitwa, ana safari nyingi na viongozi wa serikali, na baadhi ya mashirika ya kimataifa.
Upande wa kanisani nako ni kati ya Mapadre wanaoaminika ndani ya hilo shirika, na anafanya kazi kama Paroko msaidizi na watu wanampenda sana. Kwa vile ni rafiki yangu wa tangia enzi, tunashirikishana mengi ila nimemuuliza hahusiano yake na serikali na hajawahi kuniambia chochote zaidi ya kucheka.
Pia huku kanisani anawahamu vizuri viongozi wa kanisa hasa maaskofu, walikosoma, wale wanaopenda hela, wanaotumia vibaya mali za majimbo yao, wanaoliwa kwa kucheza bahati na sibu huko ulaya kwa tamaa za hela.
Wanaopenda wanawake, wenye roho nzuri, wenye ukabila, wenye ukanda.
Pia anawafahamu maaskofu walioko kwa ajili ya kanisa na walioko kwa ajili ya masliahi yao na makabila yao.
Swali langu kwenu ni hili, kuna muunganiko gani? Je huyu jamaa anatumiwa na serikali kutoa siri za kanisa au anatumiwa na kanisa kutoa siri za serikali?
Karibuni
Napenda kuleta kwenu hii hoja tusaidiane kuelimishana,
Nimesoma na jamaa mmoja kwa sasa ni Padre wa Shirika fulani ndani ya Kanisa Katoliki, huyu bwana kipindi tuko shule hakua mwanadini sana wala hata katika siasa hakuwa mpenzi sana yeye alikua mtu mkimya ila akiamua alikua na vichekesho sana.
Baada ya kumaliza form 6 kila mtu alishangaa kusikia eti jamaa huyu kaenda kusomea upadre, miaka mingi ilipita na jamaa huyu alienda kusoma nchi mbalimbali kwani hilo shirika alilojiunga linafanya kazi karibu dunia nzima. Miaka kama 7 iliyopita huyu jamaa alimaliza masomo yake na kupadrishwa, kama kawaida baadhi ya wanadarasa wake tulikuwepo siku ya upadrisho wake kushuhudi na kushangaa jinsi huyu bwana alivyoamua na kusimamia maamuzi yake ya kuwa mtumishi wa Mungu.
Sasa kitu kinachonishangaza kwa sasa Padre huyu ni mpenzi wa siasa sana na wakati mwingine anafahamu matukio serikalini kana kwamba naye ni mfanyakazi wa serikali. Kwa mfano safari nyingi za viogozi wa serikali anazifahamu kabla na ukifuatilia utakuta ni kweli. Safari za raisi zote anazo kabla hata hazijafika, siri nyingi za serkali anazo, mfano ishu ya Kagame kusarender anaijua vizuri sana. Jinsi Mama Banda alivyokuja kushtuka kuwa ramani zote na mahali silaha za nchi yake zilipo hata zile alizozania ni siri Watz wanazo, kwamba kumbe hata baadhi ya madreva wa malori kwenda nchi za jirani ni watu wa usalama
Biography za viongozi wa serikali ndo basi tena, karibia viogozi wote wa serikali anafahamu makabila yao, sehemu walikosoma, marafiki zao, wengine hata aina ya vinywaji wanavyopendelea. Hapa nilipo ni jiji na vikao vingi vya kiserikali huyu bwana anaitwa, ana safari nyingi na viongozi wa serikali, na baadhi ya mashirika ya kimataifa.
Upande wa kanisani nako ni kati ya Mapadre wanaoaminika ndani ya hilo shirika, na anafanya kazi kama Paroko msaidizi na watu wanampenda sana. Kwa vile ni rafiki yangu wa tangia enzi, tunashirikishana mengi ila nimemuuliza hahusiano yake na serikali na hajawahi kuniambia chochote zaidi ya kucheka.
Pia huku kanisani anawahamu vizuri viongozi wa kanisa hasa maaskofu, walikosoma, wale wanaopenda hela, wanaotumia vibaya mali za majimbo yao, wanaoliwa kwa kucheza bahati na sibu huko ulaya kwa tamaa za hela.
Wanaopenda wanawake, wenye roho nzuri, wenye ukabila, wenye ukanda.
Pia anawafahamu maaskofu walioko kwa ajili ya kanisa na walioko kwa ajili ya masliahi yao na makabila yao.
Swali langu kwenu ni hili, kuna muunganiko gani? Je huyu jamaa anatumiwa na serikali kutoa siri za kanisa au anatumiwa na kanisa kutoa siri za serikali?
Karibuni