Mimi nakaribia kuwashindwa hawa jamaa...manake siwaelewi.Baada ya kusikia matangazo yao matamu kwenye Power Breakfast nikapata mzuka wa kuwekeza kwao ...na nikajua wapo serious lakini tangu last week mpaka leo bado natafuta kuonana nao imekuwa ngumu.Pale wanaposema ofisi yao ipo opposite na Mlimani City nimeshakwenda mara mbili sijapaona jamaa nikimpigia simu simwelewi anachoongea mara yuko Arusha mara sijui Kinyerezi...namuuliza kama hapa ni ofisini niruhusu niingie nipate maelekezo ,yeye anasema secretary hawezi toa maelezo ya kutosha mpaka yeye awepo,....nafikiri hii kampuni yuko mtu mmoja tu ambaye yeye ni mkurugenzi, meneja,mtaalam ,mhasibu nk...halafu nilitegemea kwamba sababu mimi nimeonyesha nia ya kuwa mteja wao angehangaika kunitafuta lakini wapi...mpaka nimtafute tena na tena.....naombeni mtu anayewajua kama wapo kweli au ndiyo walewale anipe mwongozo....manake kwa style hii ni pasua kichwa kweli kweli