Kuna mtu anataka kunitapeli naomba msaada

Pole sana kaka.
 
Pole sana kijana...Fanya ukatoe taarifaa polisi haraka inavyowezekana..
Polisi ipi? Madalali wanakuambia mdaiwa hafungwi aje na nauli ya kurudia akiona anazungushwa atafute Uongozi wa soko awaeleze akiona hakuna msaada arudi akaanze moja Ila visimchanganye sana yeye si wa kwanza kutapeliwa, na akifanikiwa ashukuru Mungu.
 
Kuna kitu mnakoseaga, biashara be front it was too early for u to trust someone hizo siku 3 ungetafuta lodge ya bei rahisi ukapembejea hela yako! Uaminifu hakuna sikuhizi trade with caution!
 
safi sana ila pole, nadhani sasa umejifunza, next time hutapigwa kijinga ivyo
mjinga wakati wa kwenda, kurudi unakua mjanja, vuta soksi juu, pambana
 
faida ya 250 iyo ni biashara kichaa fanya utafute biashara nyengine
 
Du... pole mkuu
Umesha kutana na kambale la utapeli.
Biashara ni mkono kwa mkono.
 
Kwanza biashara za kuuza jumla sokoni kama unaumwa BP, usifanye kabisa!!! Unaambiwa binafsi nililipwa pesa yangu baada ya mlemavu dalali kumpora magongo yake aliyokuwa anatumia kutembelea, sasa ikawa hawezi kwenda popote!!

Nilifanya huo uhuni baada ya kunipiga kalenda kwa siku kama 3, na alipoona nimemkalia kooni, jamaa akapotea sokoni, nami kwa kujua atakuwa anakuja kuchungulia kama nipo au hapana, nikawa najibana mahali namlia timing!

Ambacho hakujua ni kwamba chige mwenyewe ni mtoto wa Uswahilini, vurugu zote kafanya kabla hajagusa 20!!!
 
Faida ni shilingi za kitanzania 250 au nimesoma vibaya!?

Wewe ni msomi kweli!?
 
umesema anataka kukutapepli mbona kwa uzoefu inaonekana kashakutapeli.
 
"Put all eggs in one bucket and watch it closely"
 
Acha hizo, mali kauli na tapeli?
 
Biashara gani ya kukopesha halafu unapata faida ya 250/=
Chifu,

Siku ukifanya biashara ya perishable goods ndipo utafahamu sio tu unaweza kukopesha na kupata faida ya Sh. 250 bali pia unaweza kukopesha kwa makubaliano ya kulipwa NUSU tu ya gharama zote ulizotumia!!

Na usisahau, amesema ni biashara ya samaki, tena wa kubanika kwa moto! And out of 2000 fishes, zaidi ya samaki 600 walikuwa wamevunjika!!!!

Sasa jiulize hata wewe mwenyewe: Je, ukienda sokoni kununua samaki wa mboga unaweza kununua samaki waliokatika?!

Ninachojaribu kusema kwa hilo swali hapo ni kwamba, samaki waliokatika wanauzwa kwa bei ya hasara kwa sababu, pamoja na kukatika, wengine miongoni mwao wanakuwa wamevurugika!!!

It's all about packaging and transportation problems!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…