DOKEZO Kuna kodi mpya ya majengo Mwanza

DOKEZO Kuna kodi mpya ya majengo Mwanza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Kavimbe jr

Member
Joined
May 9, 2023
Posts
63
Reaction score
94
Miaka 7 iliyopita nilinunua kiwanja cha SQm 400 hivi maeneo ya Sahwa.
Kutokana na uwezo wangu mdogo tukashauriana na wife tujenge nyumba ndogo kwanza ya vyumba viwili na sebule baadaye tukitulia ndio tujenge nyumba ya nafasi.

Kweli nilifanikiwa kujenga nyumba ndogo na nikaunga umeme pia na maji.
Kodi ya majengo ilikuwa tayari imo katika mfumo wa umeme. Kama kawaida ninalipa kodi kupitia manunuzi ya umeme.
Baada ya miaka nikafanikiwa kujenga nyumba kubwa ya familia iliyoshikana na ile nyumba ndogo.

Sasa nikawa napokea meseji za TAMISEMI zenye control namba kunitaka nilipie kodi ya jengo.. nikawa ninashangaa kwa sababu tayari ninalipa katika umeme.

Siku hiyo nitakutumiwa control namba na mtendaji kata kunitaka nilipie jengo langu. Nikampigia na kumwambia mimi ninalipa kodi ya jengo kupitia umeme. Mtendaji akanijibu hapo kwako una nyumba mbili unayolipia ni moja katika umeme na moja nyengine haina mita ya umeme, kwa hiyo unatakiwa kulipia kupitia control namba.

Kwa kweli sikumuelewa.. nikamwambia mimi mwenyewe ninajua nina nyumba moja siwezi kujitapa nina nyumba mbili hapa.

Akaniambia wao wanahesabu majengo, kama katika kiwanja chako kuna majengo manne basi ni nyumba nne hizo na unatakiwa zote uzilipie kodi ingawa zipo katika kiwanja kimoja.
 
Elfu ngapi mkuu changia serikali tulivu ya Mama tuzidi kuwajengea mijengo viongozi wetu, au hujayaona matunda ya kodi zako kwenye hekalu la Marehemu Ndugai?.
 
Elfu ngapi mkuu changia serikali tulivu ya Mama tuzidi kuwajengea mijengo viongozi wetu, au hujayaona matunda ya kodi zako kwenye hekalu la Marehemu Ndugai?.
Ili wazidi kujenga mahekalu yao
 
Hamiashia hiyo mita ya luku kwenye nyumba kubwa halafu hiyo nyumba ya kuanzia ndogo fugia kuku au weka kama stoo uone kama watakuletea hizo mbanga
 
Back
Top Bottom