Ramea
JF-Expert Member
- Mar 19, 2015
- 2,146
- 4,090
Katika kipindi hiki ambacho kuna vifo vingi, nime experience baadhi ya matukio ambayo huwa ni nadra kutokea ila huashiria jambo ambalo si la kheri
1. Kuna siku jirani yangu nilimkuta anamwaga takataka za vyombo vilivyovunjika nikamwuliza ilikuwaje vyombo vyote hivi vivunjike kwa wakati mmoja? Akajibu ni kabati limeanguka bila kusukumwa wala uwepo wa upepo likiwa lenyewe tu. Hata sisi tukio hili limetustaajabisha sana. Haikupita wiki yule jirani yangu alipata ajali ya kugongwa na gari akiwa anaendesha pikipiki akafariki papo hapo. R.I.P Mpambanaji.
2. Rafiki angu ambaye alikuwa mtaalam wa ultrasound hospitali x, wiki kadhaa kabla hajafariki alikuwa anazungumzia sana kifo. Yaani ukikaa naye Hadi anaudhi stori zake za kifo tena akijizungumzia yeye mwenyewe ataiachaje familia yake kana kwamba alikuwa anajua. Cha kushangaza alikuwa na afya njema tu nilishtuka napigiwa simu nikiwa safarini kuwa rafiki yangu amefariki alikimbizwa hosp usiku alikosa pumzi na hakuwahi kupatiwa matibabu. R.I.P Comrade.
3. Brother wangu wa tumbo moja, alikuja nyumbani kwangu ingawa huwa anakuja mara kwa mara, ila hii ya mwisho alikuwa wa tofauti kidogo. Aliomba achukue vitu vyake(huwa anaacha mabegi au mabox ) mara zote tunamletea begi au box analotaka akiwa sebuleni, lakini awamu hii aliingia mwenyewe chumbani, chumba ninachokitumia kama store. Kumbe ndo ilikuwa last visit. Ameondoka kwa changamoto ya upumuaji, kukohoa na kukosa hamu ya kula. R.I.P Brother

Msg zako za mwisho WhatsApp bado nazisoma kila muda. Naona kama bado upo nasi.
1. Kuna siku jirani yangu nilimkuta anamwaga takataka za vyombo vilivyovunjika nikamwuliza ilikuwaje vyombo vyote hivi vivunjike kwa wakati mmoja? Akajibu ni kabati limeanguka bila kusukumwa wala uwepo wa upepo likiwa lenyewe tu. Hata sisi tukio hili limetustaajabisha sana. Haikupita wiki yule jirani yangu alipata ajali ya kugongwa na gari akiwa anaendesha pikipiki akafariki papo hapo. R.I.P Mpambanaji.
2. Rafiki angu ambaye alikuwa mtaalam wa ultrasound hospitali x, wiki kadhaa kabla hajafariki alikuwa anazungumzia sana kifo. Yaani ukikaa naye Hadi anaudhi stori zake za kifo tena akijizungumzia yeye mwenyewe ataiachaje familia yake kana kwamba alikuwa anajua. Cha kushangaza alikuwa na afya njema tu nilishtuka napigiwa simu nikiwa safarini kuwa rafiki yangu amefariki alikimbizwa hosp usiku alikosa pumzi na hakuwahi kupatiwa matibabu. R.I.P Comrade.
3. Brother wangu wa tumbo moja, alikuja nyumbani kwangu ingawa huwa anakuja mara kwa mara, ila hii ya mwisho alikuwa wa tofauti kidogo. Aliomba achukue vitu vyake(huwa anaacha mabegi au mabox ) mara zote tunamletea begi au box analotaka akiwa sebuleni, lakini awamu hii aliingia mwenyewe chumbani, chumba ninachokitumia kama store. Kumbe ndo ilikuwa last visit. Ameondoka kwa changamoto ya upumuaji, kukohoa na kukosa hamu ya kula. R.I.P Brother


Msg zako za mwisho WhatsApp bado nazisoma kila muda. Naona kama bado upo nasi.

