Kuna Halmashauri inauza viwanja mpaka kufikia, shilingi 8000 kwa square meter moja kama ilivyo sasa kwa Manispaa ya Dodoma?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Tangu Dodoma itangazwe kuwa jiji, bei za viwanja katika manispaa hii zimekuwa juu mno kiasi cha mita moja ya mraba kufikia kuuzwa kwa bei ya shilingi 8000 kwa maeneo ya Michese na hata Nzuguni bei inatarajiwa kuwa ni hiyo.

Bei zingine kwa mita moja ya mraba ni kati ya shilingi 5000/= mpaka kufikia shilingi 7500/= kutegemeana na location na aina ya matumizi ya kiwanja ambapo viwanja vya makazi na biashara ndio bei yake huwa ipo juu zaidi kulinganisha na vya makazi tu ila vyote viko katika hiyo range.

Maeneo haya mengi ni mapori kwa maana hata miundombinu kama maji na umema bado ila bei ndio hizo.

Sasa najiuliza,katika nchi hii,kuna Halmashauri yoyote imewahi kuuza viwanja ambavyo ni mapori na vilivyo mbali na katikati ya mji kwa bei za aina hii huku wakitoa muda wa kulipa wa ndani ya miezi mitatu?

Hivi hata Manispaa za Dar-es-Salaama,na wao leo hii wanaweza kuuza viwanja kwa bei hizo?

Tunawashukuru kitu kimoja kwamba ukilipia kiasi fulani au ukionyesha unajitahidi kulipa,basi wanaweza kukuvumilia na kukuongeza muda ingawa kulipia huku bado hakukupi guarantee

Hata hivyo,bei hizi na muda huo ni realistic kwa watanzania wengi?

Na kingine ni Manispaa hii kuuza viwanja kupitia ramani (mtu unachagua kiwanja kwenye ramani tu) bila kwenda sight na ili ukaone kiwanja husika ulichochagua, ni mpaka uwe umekamilisha malipo.

Waziri Lukuvi tunaomba utazame jambo hili hasa huu muda wanaoutoa kwani ni mfupi mno na unawafanya watu wengine hata kusita kununua kwa hofu ya kunyang'anywa muda uliopangwa kulipia ukiishi bia ya kukamilisha malipo.

Mipango na mikakati ya kuendeleza mji huu ni mizuri kwa mfano ujenzi wa hili jengo lnaloonekana katika picha hapo chini litakolejengwa katika Mji wa Serikali maeneo ya Mtumba, ila hizi bei za viwanja pamoja na muda mnaoutoa, kwakweli haviendani kabisa na maisha ya watanzania walio wengi.

1567109517091.png
 
Na si ajabu serikali ya awamu ya 6.. Ikarudi Dar Es Salaam... Hapo dodoma yabaki magofu tu
Kwakuwa kila Raisi akija anakuja na yake,hili unaloliseme linasemwa na wengi tu hivyo hatutoshangaa likitokea.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kwa kuwa ni ghali sana ulipaji unazidi mwezi mmoja. Waliruhusu kununua kwa kupitia mkopo wa benki au direct kutoka kwenye any source of allowances unazopata kila mwezi. Nadhani kila sehemu wana taratibu zao za deadline, lakini mara zote bei za viwanja zinaweza kutofautiana kulingana na fidia iliyolipwa kwa wakazi wa awali, potentials za eneo, utengenezaji wa miundo mbinu kama kuchonga barabara, kuweka umeme na maji n.k. Hizo costs automatic zitaleta bei tofauti za viwanja kati ya sehemu A na B.

Mbeya vijijini mkabala na uwanja wa Ndege wa Songwe, walikuwa wanauza 11,500/= Kwa square metre moja
 
Dogo unashinda unapiga porojo Jf halafu unabana pua 8000@Sqm ni ghali!

Halmashauri za miji kama Kahama zinauza kwa mpaka 10,000@Sqm!

Kule Kisesa wilaya ya Magu ni zaidi hata ya hiyo.
 
Dogo unashinda unapiga porojo Jf halafu unabana pua 8000@Sqm ni ghali!

Halmashauri za miji kama Kahama zinauza kwa mpaka 10,000@Sqm!

Kule Kisesa wilaya ya Magu ni zaidi hata ya hiyo.
Acha porojo unapesa hizo za rushwa na michongo ya kipuuzi unajiona una pesa?? hapa tunaangalia maslah ya wengi sio ya mtu mmoa mmoja mwenye pesa za kulipwa kuuwa wengine na kutesa.

Unamjua salary slip wewe??

Au unakuwa na roho.mbaya kama ya Maiba kusema Erick Kabendera analipwa na mabeneru kisa tu anamilik Mansion nzuri sana kule Mbweni??

Salary slip ukimjua utajiona wewe fala.
 
Acha porojo unapesa hizo za rushwa na michongo ya kipuuzi unajiona una pesa?? hapa tunaangalia maslah ya wengi sio ya mtu mmoa mmoja mwenye pesa za kulipwa kuuwa wengine na kutesa.

Unamjua salary slip wewe??

Au unakuwa na roho.mbaya kama ya Maiba kusema Erick Kabendera analipwa na mabeneru kisa tu anamilik Mansion nzuri sana kule Mbweni??

Salary slip ukimjua utajiona wewe fala.
Huyo jamaa anaongozwa na chuki binafsi na hana hoja za msingi.
 
Hata hivyo,bei hizi na muda huo ni realistic kwa watanzania wengi?
Katika tovuti ya wizara ya ardhi,kuna bei elekezi kwa mita za mraba kwa kila eneo nchi nzima.halmashauri wamefuata bei elekezi
Ardhi inapangiwa bei kutokana factors nyiingi,usiangalie uporini,huko ni mji mkuu,kuna uwanja mkubwa wa mpira unajengwa,na Sgr inafika hapo,baada ya miaka miwili utajuta kwa nini hukununua
 
We endelea kulalamika tu....mi nimeshakamata plot yangu Nala..pamoja na kwamba kuna mawe kama mlima lkn kitaeleweka tu..Dom baada ya miaka 5 itakuwa sio kabsa.
 
Back
Top Bottom