Kuna haja ya kuangalia mavazi ya mtu kwenye usaili wa kazi?

DINHO

JF-Expert Member
Dec 12, 2016
886
1,750
Kwenye kutafuta ajira kuna mambo mengi sana. Wasakatonge tunahangaika huku na huko kutafuta mrija wa Asali, iwe nje ya nchi au ndani ya nchi, iwe serikali au taasisi binafsi.

Sasa basi nikiwa mmoja wa wasakatonge nilibahatika kuomba hizi kazi za TRA, na mara baada ya kuomba nikafanikiwa kupata Group moja la tulioomba kazi.

Kupitia hili group bhana, juzi usiku nikaona mjadala umeanza, mmoja wa wanagroup alitoa angalizo kuwa iwapo wasailiwa watafanana kwa marks basi kuna kigezo cha mavazi kinatumika katika kuwaondoa au kuwapata best candidate.

Kwamba watu wavaze official, kwenye usaili inakuwa rahisi kupata kazi, na mjadala ukawa mkubwa sana.

Tiliozoea kufanya saili mbalimbali hasa za serikali tukakubaliana yes mavazi ni muhimu sana, na yanachangia kwa asilimia kubwa kwenye kuchaguliwa kupata kazi.

Hapa sasa akatokea member mmoja akasema kigezo cha Mavazi hakitumiki kwenye kuchagua best candidate kwa maana Mavazi ni kipimo cha utajiri wa mtu au familia. Hivyo kigezo cha Mavazi hakiwezi kuwa sifa moja wapo ya mtu kuajiriwa na kwamba mtu anaajiriwa kwa uwezo wake kichwani.

Na ikiwa umepata ajira basi taasisi husika ndio itakuwa kanuni na taratibu za mavazi ya taasisi hiyo kama mwajiriwa.

Akaenda mbali zaidi akasema kama mavazi yanaamua nani aajiriwe kwanini wasiweke sare maalumu za usaili ili watu wote waende wakiwa sawa kimavazi?

Nilitamani kuona ule mjadala unaendelea nipate kuona namna gani sisi vijana tunaweza kuchambua mambo kisomi na kwa kuzingatia Dunia inavyoenda. Bahati mbaya leo asubuhi nimeingia nimeona group sasa wenye uwezo wa kutuma kitu ni Admins tu.

Binafsi nimeona saili nyingi ma HR wakiangalia mavazi, na wengi wamekosa kazi kupitia uvaaji.

Je, wadau tujadili hapa, mavazi yana uhusiano na upatikanaji wa kazi? Na je unakubaliana na hoja ya jamaa kuwa mavazi hayapaswi kuwa kigezo cha mtu kuajiriwa bali weledi na uwezo wake wa kujua mambo?
 
Je wadau tujadili hapa, mavazi yana uhusiano na upatikanaji wa kazi? Na je unakubaliana na hoja ya jamaa kuwa mavazi hayapaswi kuwa kigezo cha mtu kuajiriwa bali weledi na uwezo wake wa kujua mambo?
Mwonekano wa mtu sio kigezo cha kupata kazi, ila ni kigezo cha kuaminika (kinatharia) kuwa unafaa. Smartness muhimu sana kwenye kila ofisi. Zingatia mabano.
 
Namuunga mkono jamaa hapo, usaili haupaswi kuweka kigezo cha mavazi. Na sio kwamba tukisema kigezo cha mavazi basi mtu avae bukta hapa, hapo naelewa mantiki yake ni kwamba hata ukivaa jeans basi ufanye usaili na upimwe kwa uelewa wako. Na inajulikana wazi kuwa huwezi kwenda kwenye usaili na nguo ya kulalia wa chupi tupu wala bukta.
 
Kwenye oral interview kuna max zinatolewa nje na maswali, hapa sikuzote hamuwezi kufanana lazima mtofautiane
1. Confidence
2. Smartness
Ndomana kwenye oral unasisitizwa sana uwe na confidence pamoja na kupendeza.
Sasa hapo kwenye Smartness huoni kwamba kuna watu utawanyima haki? Wale waliotoka maisha magumu mara nyingi hawawezi kuwa smart kama wa mjini. Hapo utakuwa umetenda haki?
 
Ndo naingia kwenye interview. Dua zenu wakuu 😁😁😁

Screenshot_20230627_131043_Chrome.jpg
 
Sasa hapo kwenye Smartness huoni kwamba kuna watu utawanyima haki? Wale waliotoka maisha magumu mara nyingi hawawezi kuwa smart kama wa mjini. Hapo utakuwa umetenda haki?

Mkuu smartness hawaangalii umevaa nini cha muhimu uwe umejipangilia vizuri, kwa govt they know ila kwa Private hzo huruma hawana kabisa. Hivi kweli hata kama maisha magumu utakosa suruali, shati, tai na kiatu kwa ajili ya interview??
 
Hebu siku moja vaa hivi halafu uingie kwenye interview na ukajibu maswali yote kwa usahihi wa asilimia 100 halafu uone kitatokea nini.

View attachment 2670296
Hoja yako ni dhaifu, inajulikana wazi huwezi kwenda hata sokoni umevaa chupi tupu. Ila umevaa jeans au track suit nk. unaweza kwenda na mambo yakawa fresh. Hapa umewaza tofauti na ungekaa kwa kutulia ungemuelewa mleta mada.
 
Mkuu smartness hawaangalii umevaa nini cha muhimu uwe umejipangilia vizuri, kwa govt they know ila kwa Private hzo huruma hawana kabisa. Hivi kweli hata kama maisha magumu utakosa suruali, shati, tai na kiatu kwa ajili ya interview??
Kwa maelezo ya jamaa alidai kuna kundi kubwa la watu hawana hizo nguo, na hata kuazima nguo na unaazima wale unaofanana nao miili na nk.

Hivyo lazima tutambue kuwa kuna watu wanatoka mazingira ambayo kununua nguo zikakaa kwenye begi kusubiri usaili ni anasa, hivyo wao huwa na nguo ambazo itaweza kuvaliwa na kudumu katika mazingira yote.
 
Kuna fani ambazo ukisoma, kazi ndio zinakuwa zinakutafuta wewe; na kuna fani zingine wewe ndio unakuwa unatafuta kazi.

Kwa hiyo, hizi fani ambazo wewe ndio unatakiwa utafute kazi inabidi uongeze 'point' kwenye mavazi; ila kwa hizi fani ambazo kazi ndio zinakuwa zinawatafuta, mavazi huwa hayana 'point' yoyote.​
 
Kuna fani ambazo ukisoma, kazi ndio zinakuwa zinakutafuta wewe; na kuna fani zingine wewe ndio unakuwa unatafuta kazi.

Kwa hiyo, hizi fani ambazo wewe ndio unatakiwa utafute kazi inabidi uongeze 'point' kwenye mavazi; ila kwa hizi fani ambazo kazi ndio zinakuwa zinawatafuta, mavazi huwa hayana 'point' yoyote.​
Kwanini tunaamini mavazi ni kipimo cha umahiri?
 
Hoja yako ni dhaifu, inajulikana wazi huwezi kwenda hata sokoni umevaa chupi tupu. Ila umevaa jeans au track suit nk. unaweza kwenda na mambo yakawa fresh. Hapa umewaza tofauti na ungekaa kwa kutulia ungemuelewa mleta mada.
Sikuwa siriazi mkuu....

Usinichukulie siriazi kihivyo.....

Nijuavyo mimi watahiniwa wakilingana mwajiri anaweza kutumia kigezo cho chote anachokitaka ili kumsaidia katika maamuzi yake. Na ni haki yake. Hili la mavazi kidogo ni extreme maana halihusiani na competence ya mtu japo linaweza kutoa picha mtahiniwa ni mtu wa aina gani.

Kwenye interview za wenzetu huko siku hizi wana maswali ya ziada ambayo hayahusiani na kazi unayoomba. Wanataka tu kupima uwezo wako wa kufikiri. Mf. Mshikaji mmoja aliwahi kuulizwa eti kama angechaguliwa aende one way trip to Mars angekubali au angekataa; na kwa nini? Au unaweza kuulizwa maoni yako juu ya vita vya Urusi na Ukraine....na hii inawapa picha ya jumla kuhusu uwezo wako wa kujenga hoja, kufikiri na mengineyo na hii inaweza kukupa edge kama ikitokea mmelingana....

Huku kwetu nadhani ni vimemo au bias tu pia vinaweza kumaliza kazi!
 
Kwa maelezo ya jamaa alidai kuna kundi kubwa la watu hawana hizo nguo, na hata kuazima nguo na unaazima wale unaofanana nao miili na nk. Hivyo lazima tutambue kuwa kuna watu wanatoka mazingira ambayo kununua nguo zikakaa kwenye begi kusubiri usaili ni anasa, hivyo wao huwa na nguo ambazo itaweza kuvaliwa na kudumu katika mazingira yote.

Mkuu mtu aliyemaliza chuo kweli inawezekana akaose shati, surual na kiatu kwaajili ya interview??. Oral zote nilizofanikiwa kwenda watu wanapendeza sana, honestly.
 
Kwenye kutafuta ajira kuna mambo mengi sana. Wasakatonge tunahangaika huku na huko kutafuta mrija wa Asali, iwe nje ya nchi au ndani ya nchi, iwe serikali au taasisi binafsi...
Mafazi yanatakiwa yaangaliwe lakini si kuwa nani kavaa za ghali kuliko mwenzie. Issue ni kuvaa Smart na Nadhifu. Smart namaanisha proper dressed mfano umeenda kwenye interview but umevaa track suit hata kaa itakua nadhifu lkn sio proper kwa muktadha kama huo
 
Sikuwa siriazi mkuu....

Usinichukulie siriazi kihivyo.....

Nijuavyo mimi watahiniwa wakilingana mwajiri anaweza kutumia kigezo cho chote anachokitaka ili kumsaidia katika maamuzi yake. Na ni haki yake. Hili la mavazi kidogo ni extreme maana halihusiani na competence ya mtu japo linaweza kutoa picha mtahiniwa ni mtu wa aina gani...
Hii nimeipenda sana, na ningetamani hapa kwetu wangetumia hii mbinu kuliko kuangalia mavazi. Big up kwa mchango huu muhimu sana.
 
Mkuu mtu aliyemaliza chuo kweli inawezekana akaose shati, surual na kiatu kwaajili ya interview??. Oral zote nilizofanikiwa kwenda watu wanapendeza sana, honestly.
Mtu aliyemaliza chuo mwaka 2010 huko bado atakuwa na hizo nguo? Na yuko kijijini mpanda huko?
 
Mafazi yanatakiwa yaangaliwe lakini si kuwa nani kavaa za ghali kuliko mwenzie. Issue ni kuvaa Smart na Nadhifu. Smart namaanisha proper dressed mfano umeenda kwenye interview but umevaa track suit hata kaa itakua nadhifu lkn sio proper kwa muktadha kama huo
Hoja hapa mavazi yanaakisi ubora wa msailiwa? Sababu za msingi za kuangalia mavazi ni nini? Kwann wasitumie maswali ya general katika kupima uelewa?
 
Kuna fani ambazo ukisoma, kazi ndio zinakuwa zinakutafuta wewe; na kuna fani zingine wewe ndio unakuwa unatafuta kazi.

Kwa hiyo, hizi fani ambazo wewe ndio unatakiwa utafute kazi inabidi uongeze 'point' kwenye mavazi; ila kwa hizi fani ambazo kazi ndio zinakuwa zinawatafuta, mavazi huwa hayana 'point' yoyote.​
Mh kwa sasa ni ngumu labda kwa hapo way back ndio baadhi ya fani unatafutwa mf engineers, Some Technicians, Designers nk but kwa sasa watu wamekuwa wengi ni gombania kombe
 
Hoja hapa mavazi yanaakisi ubora wa msailiwa? Sababu za msingi za kuangalia mavazi ni nini? Kwann wasitumie maswali ya general katika kupima uelewa?
Mkuu unataka kusema we huelewi kuna watu wanavaa hadi vipedo na vimini-skeit kanisani? Jiulize why?

Halafu pia take into consideration kwamba kwa fani kama walimu mtu inatakiwa aingie darasani afundishe watoto wamuelewe unadhani kwa mavazi hapo juu watoto watakuwa na concentration?
 
Back
Top Bottom