Elections 2010 Kuna aliyeamini?

Hapo kwenye bold ni kweli kabisa. Ukisubiri maish aboa yakukute kitandani wakati umelala basi utasubiri sana.Serikali yeyote hata bila Kikwete kuahidi maisha bora inachofanya ni kuweka mazingira wezeshaji ( sijui kana ni kiswahili sanifu kwa enabling environment) ili mtu anaye jibidiisha aweze kufanikiwa. Cha kujiuliza ni kuwa je Kikwete aliweka mazingira wezeshaji kipindi chake tofauti na vipindi livilivyopita?

Huwezi kuendelea kama mazingira yanayokuzunguka hayakuwezeshi kujiendeleza. Huwezi kujiendeleza kama u mgonjwa na hupati dawa, huwezi kujiendeleza kama hupati elimu nzuri, hata kama una akili vipi. Mazingira mazuri ya kujiendeleza lazima yawepo, na hilo ni jukumu la serikali iliyopewa dhamana na wananchi. Hebu tujiulize, kazi ya serikali ni nini?
 
Hivi mwaka 2005 Kikwete alipoahidi maisha bora kwa kila Mtanzania, kati yetu humu kuna aliyemwamini kweli au niko peke yangu tu ambaye sikuamini hayo?
Nilidanganyika ndugu yangu. Ama kwa hakika sintorudia kosa tena. Nawaomba radhi watanzania kwa kumpa kura mtu huyu aliyetufikisha hapa kwenye dimbwi la maisha holela kwa kila mtanzania
 
Maisha bora unaletewa nyumbani kwako, au ni baada ya mtu binafsi kujishughilisha?

Kinachotakiwa ni kwa watanzania wote kwa ujumla kuamka na kutafuta hayo maisha bora. Haiingii akilini kusubiri maisha bora kwenye kibanda chako kama hutaki uwe na maisha bora!

Mkuu,

Tatizo hapa sio kusubiria maisha nyumbani, tatizo ni kwamba serikali inachukua mali za wananchi (wao wanaita kodi) ili ilete maendeleo kwa njia ya shule, barabara, maji, afya, nk. Maendeleo yanayotegemewa ni hayo. Je Kikwete ametekeleza hayo?
 
maisha bora kwa mtanzania yanawezekana ikiwa watanzania tutajituma, sote tunajua watanzania niwavivu tunataka kila kitu tuletewe wengine waliamini maisha bora maana yake kutakuwa na sehemu za kwenda kula bure, watapewa nyumba walale bure na mengineo

ila ktk kipindi hiki tumeona elimu ikiimarishwa na fursa za kusoma elimu ya juu iko kwa kila mtanzania ataejituma kufanya maisha yake yawe bora.

miundo mbinu imeimarishwa ili wakulima na wafanya biashara wahangaike kuitumia ili waboreshe vipato vyao

serikali imesisitiza na kufanya marekebisho mengi kwenye masuala ya fedha ili wananchi wenye kutaka maisha bora wakopesheke na kufanya biashara kuinua vipato vyao.

hata sheria nyingi zimepitiwa na kufanyiwa marekebisho kumuwezesha mtanzania kujitafutia maslahi kama sheria ya madini, ardhi, uwekezaji na mengineo

kikwete amejitahidi la kweli tusemeni

hata vyama vya siasa vimewezeshwa na ndio maana baada ya kutumia fursa walizonazo wanatukana


fadhila ya punda mateke
 
Maisha bora unajiwekea mwenyewe, Chama/serikali vipo kukuwezesha kufikia hayo maisha. Binafsi niliamini hivyo na nina uhakika wale waliotaka maisha bora wameyapata.

Hii ni kejeli na dharau kwa maelfu ya Watanzania wema waliopoteza maisha/wanaohangaika kwa ajili ya uongozi mbovu wa Kikwete na wana mtandao wezi. Mungu atakulaani wewe unayetoa kejeli hizi!!!!
 
Mwenye akili hawezi kuamini hata kidogo mwenyewe nilikuwa mshabiki mkubwa sana wa awamu ya nne lkn baada ya kuahidiwa maisha bora kwa kila mtu nakakata shauri,

maisha bora yapi? kilimo kwanza kwa power tila mmeona wapi? au pesa ya epa kupelekwa kwenye mbolea, productivity imeongezeka kwa kiasi gani? mbolea imebaki au imeisha msimu ulee? priority ni zipi mazao ya chakula au miti ya mbao, ni uvuvi, au urinaji wa asali ukishajiuliza haya na mengine mengi utaona ni uzushi mtupu
 
Maisha bora unaletewa nyumbani kwako, au ni baada ya mtu binafsi kujishughilisha?

Kinachotakiwa ni kwa watanzania wote kwa ujumla kuamka na kutafuta hayo maisha bora. Haiingii akilini kusubiri maisha bora kwenye kibanda chako kama hutaki uwe na maisha bora!

Wakati mnaahidi hamkusema kama wananchi watajiletea wenyewe. Kuna nani huyo asiyeataka maisha bora? Nani amekwamba unapata maisha bora kwa kuyataka tu?
 
Wakuu Kibunango na Mtu wa Pwani,

Hakuna ambaye anataka maendeleo yaje yenyewe, kuna watu huko vijijini wanavuja jasho la damu na mwisho wa siku hakuna wanachopata. Mfano, juzi JK kapita Sumbawanga na Mby akaahidi kwamba ataongeza fedha za SGR ili kununua mahindi. Hakuna wanunuzi wa mahindi na serikali imepiga marufuku kuuza mahindi nje ya Tanzania, sasa niambie hapo mkulima afanye nini?

Nenda Lindi, wakulima wa Korosho wamevuna korosho zao, wakienda kuuza wanapewa stakabadhi kwamba malipo baadaye. Malipo yake hapo ni mbinde.

Kahawa ukiuza kwa wanunuzi kutoka Uganda unapewa bei nzuri, lakini ukiuza kwa vyama vya ushirika vya KNCU na KDCU, bei yake utalia. Sasa hao wakulima waende kuuza wapi na kuuza kwa waganda mnasema ni walanguzi.

Unasema hosp ni za Dar, umeishafika kwenye zahati za vijijini ambako hata wauguzi hakuna ila kuna wakunga wa jadi tu. Kuna shule zina mwalimu mmoja, hao watoto watasomaje?

Barabara za vijijini hazipitiki mwaka mzima, kila mwaka mnakuja na habari ya kutengeneza barabara ambazo zinahitaji ukarabati tu, feeder roads za vijijini hakuna anayeziangalia, matokeo yake wakulima wanabebeshwa gharama za kusafirisha mazao, pembejeo na mahitaji yao. Mwisho wa siku pembejeo bei juu, mazao bei chini, na bei ya mahitaji ni juu, cost of living inapanda mara 3 zaidi kuliko yule aliye mjini.

Kwa hiyo msiwatukane wananchi wa vijijini ati ni wavivu, wanajitahidi sana but juhudi zao za kujikamua zinakwazwa na matatizo ya barabara, masoko, na huduma duni za jamii.
 
Maisha bora unajiwekea mwenyewe, Chama/serikali vipo kukuwezesha kufikia hayo maisha. Binafsi niliamini hivyo na nina uhakika wale waliotaka maisha bora wameyapata.

Sasa kama maisha bora unajiwekea mwenyewe kwanini mliifanya kauli hiyo kuwa motto wenu 2005?That's like saying kula au kulala inawezekana kwa mwanadamu.No need to tell anybody about that kwa vile kila mtu anajua.

And of course,maisha bora yamewezekana kwa mafisadi including wamiliki wa Kagoda.
 
Maisha bora unaletewa nyumbani kwako, au ni baada ya mtu binafsi kujishughilisha?

Kinachotakiwa ni kwa watanzania wote kwa ujumla kuamka na kutafuta hayo maisha bora. Haiingii akilini kusubiri maisha bora kwenye kibanda chako kama hutaki uwe na maisha bora!

elimu duni.jpg

Hawa wameshaamka na wanatafuta maisha bora.Je, wanaweza kufanikiwa kupata maisha bora kwenye mazingira duni kama haya?
 
Hapo kwenye bold ni kweli kabisa. Ukisubiri maish aboa yakukute kitandani wakati umelala basi utasubiri sana.Serikali yeyote hata bila Kikwete kuahidi maisha bora inachofanya ni kuweka mazingira wezeshaji ( sijui kana ni kiswahili sanifu kwa enabling environment) ili mtu anaye jibidiisha aweze kufanikiwa. Cha kujiuliza ni kuwa je Kikwete aliweka mazingira wezeshaji kipindi chake tofauti na vipindi livilivyopita?
'A frog at the bottom of the well thinks the sun light is as big as the top of it' sasa watu watajua vipi what opportunities are available to them , hiwapo hawajui what opportunity looks like.

True JK kafungua milango fulani so far hila inawafurahisha a few Tanzanians and a little of Smattas walioelewa kitendawili chenyewe kibaya zaidi wanatutukana humu humu ndani ya forum for our ignorance and poor educational standards.
 
Back
Top Bottom