Kumuoa binti msomi

zagarinojo

JF-Expert Member
Jul 26, 2020
2,622
2,838
Mara nyingi katika masuala yanayowapa wakati mgumu vijana katika kuchagua wenza wao. Ni pamoja na suala la kiwango cha elimu walichonayo.

Wasichana wengine huwakataa wavulana kwa kigezo cha elimu waliyonayo? Je mnahisi elimu inaweza kuwa kikwazo cha mahusiano baina ya watu wawili lakini kabla lazima tutambue akili siyo elimu na elimu siyo akili

Mleta mada ni mvulana
 
Elimu haiwezi kuwa kikwazo kwa mwanaume anayejielewa
Yeah naelewa lakini dada hawa wasomi hupenda wavulana wasomi pia....ni ngumu kupata msichana aliye na elimu yake kaolewa na jamaa wa maskani asiye na elimu
 
Nyie wasomi mkuje mumjibu mtoa mada.
Umenisaidia kaka wasichana wanashindwa kuelewa akili siyo elimu wapo wengi ambao wana akili na wako kitaa
Mara ngapi tumeshudia watu waliokwenda veta wanashindwa kuendesha magari na wale waliojifunza mtaani ni madereva mahiri
 
Yeah naelewa lakini dada hawa wasomi hupenda wavulana wasomi pia....ni ngumu kupata msichana aliye na elimu yake kaolewa na jamaa wa maskani asiye na elimu
mwanamke msomi humpenda mwanaume sio mvulana.hebu rekebisha kidogo mwandiko wako
 
Mkuu mvulana hata iweje lazima akataliwe tu hakuna namna.siku akiwa mwanaume atarudiwa na mwanamke msomi
Lakini baadae mambo kumbe yanabadilika mvulana yuleyule atakapo pambana na kupata mali na fedha za kujikimu wasichana hukubali wenyewe
 
Back
Top Bottom