Kumleta Mwekezaji wa Parachichi ni kufinya ajira

ibanezafrica

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,261
6,543
Jana kupitia habari saa mbili usiku Utv kuna mwekezaji toka arabuni ameletwa huko Njombe na tayari yupo mbioni kutaka kuwekeza katika zao la Parachichi akihitaji apatiwe maelfu ya hekari.

Imeelezwa Tanzania ni kama nchi ya tatu au nne katika nchi zinazotoa parachichi bora kabisa duniani.hii ina maana soko la uhakika lipo.

Nimejiuliza tumeshindwa kujiongeza sisi kama nchi kupitia wizara za fedha/kilimo/Sua kuwa organize vijana tuliojazana mitaani kwa kukosa ajira kukatiwa vipande vya mashamba either kwa vikundi au mtu mmoja mmoja kuwezeshwa vianzio na baadae kurejesha yaani kuwe na mpango maalum wa kuzungusha mitaji.

Hawa vijana wangezalisha parachichi kwa wingi serikali ikatafuta masoko duniani hapo serikali ingepata pesa za kigeni,vijana wengi tungeweza kujipatia ajira ya kudumu na kujikimu na maisha.

Zoezi hili lingefanyika sehemu tofauti nchini kwa mazao tofauti kutegemea na hali ya hewa sememu husika
Hilo pia lingefanyika kwenye mabonde makubwa,upande wa uvuvi maziwani humo,kwenye ranchi za taifa upande wa ufugaji,asali,upande wa uwindaji pia kilimo cha mboga na matunda,migodini nk

Nina imani seikali kupitia wizara zake wangezingatia hili tatizo kubwa la ajira na umasikini lingeenda kupungua pakubwa

Tujitaahidi kuilinda ardhi na mali asili zetu zilinufaishe taifa na Watanzania,bado ninaamini ile kauli ya baba wa taifa kwamba ili tuendelee tunahitaji Watu na Ardhi.

Rasilimali zetu tuzitumie sisi wenyewe kwanza kabla ya kuita wageni kwa mambo ambayo hata sisi tunaweza kufanya.
 
Wazo lako zuri ila nawaza, vijana hawajui kuhusu hiyo fursa?!
Ila tujitahidi kujielimisha na kuzikimbilia hizi fursa.
Serikali za kiafrika kuzisubiri zilete matokeo chanya ya kuinua vijana wake kwa vitendo si rahisi.
Shida ni uwezeshaji hasa mtaji. Nimezikimbilia hizi fursa ila Viongozi wengi sio waelewa, ni kama wana watu wao na jamaa zao. Wakiona hakuna masilahi yao katika mradi mnataka kuufanya wanawa ignore.....
 
Wazo lako zuri ila nawaza, vijana hawajui kuhusu hiyo fursa?!
Ila tujitahidi kujielimisha na kuzikimbilia hizi fursa.
Serikali za kiafrika kuzisubiri zilete matokeo chanya ya kuinua vijana wake kwa vitendo si rahisi.
Tena hizo mbegu ni za kuokota na kupanda, mashamba ni ya urithi , kwa nini wasipande na kuihudumia miparachichi wao wenyewe?
 
Tena hizo mbegu ni za kuokota na kupanda, mashamba ni ya urithi , kwa nini wasipande na kuihudumia miparachichi wao wenyewe?
Huku kwetu kuna uvumi kuwa kuna aina fulani za parachichi za kigeni hadhifai kuliwa na watoto wa kiume? Huko kwenu zimeshafika pia?
 
Naona unataka kutusambaratishia wapiga kura wetu, tumepata hasara kwa kuwaondoa wamachinga ambapo kura zimepungua kwani mijini ndiko ziliko kura nyingi, kama pesa za kigeni huwa tunasafiri kwenda kuomba misaada na kukopa hivyo hilo tumelipatia ufumbuzi.
 
Back
Top Bottom