KUMEKUCHA: Vigezo kupata watendaji bomba la Uganda vyatajwa

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
2,012
5,571
Muhongo asema Sekta Binafsi "mguu sawa"

WAZIRI wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo ametaja vigezo vitakavyotumika kuwapata watendaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi ya Uganda.

Profesa Muhongo ameyasema hayo ikiwa ni siku moja tu baada ya kuwasili nchini akitokea Kampala, ambako alihudhuria kikao cha viongozi wa nchi wanachama wa jumuia ya Afrika Mashariki ambapo Rais Yoweri Museveni wa Uganda alitangaza uamuzi wa Serikali yake.

Rais Museveni aliitangaza njia ya Kabaale hadi Tanga nchini kuwa ndio sahihi kupitisha mafuta ghafi yake.

Baadhi ya vigezo vitavyotumika kuwapata Viongozi na Watendaji hao ni hizi kama vifuatavyo: Uadilifu, Uzalendo, Ubunifu na Utaalamu.

Aliendelea kusema kuwa vigezo vingine ni Uzoefu, Umakini, Ufanisi, Ushirikiano, Historia ya mafanikio kikazi na kasi ya utekelezaji wa majukumu yaliyotolewa.

"Tumedhamiria kupunguza muda (mid 2020) uliopangwa wa kukamilika kwa Bomba hili mapema zaidi," alisema Prof Muhongo.

Waziri alilakiwa kwa mbwembwe na bashasha na wananchi waliojitokeza katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.

Profesa Muhongo ameitaka SEKTA BINAFSI kujiandaa kwa kazi za aina mbalimbali zitakazotangazwa karibuni.

Katika mchakato huo, Tanzania ilipata upinzani mkali sana kutoka kwa Serikali ya Kenya, ambao walitaka bomba hilo lipitie katika bandari ya Lamu yenye miundombinu hafifu.

Mbali na miundombinu hafifu na hatari ya uwezekano wa hujuma kutoka kwa magaidi wa al-shabab, ingechukua muda mrefu zaidi hadi mwaka 2022 kumaliza ujenzi wa bomba hilo.

Habari kutoka chanzo cha habari cha kuaminika kimemtaja Mwanasiasa maarufu, Makongoro Nyerere kuhusika katika ushawishi wa mradi huu.
 
Wale waliokuwa wana njama za kumng'oa Prof Muhongo wanaaibika sasa
Moja kati ya sababu za umasiki wa Tanzania and hence Watanzania ni kuto ku deal na chanzo cha tatizo badala yake hua tuna dela na tatizo, mfano tatizo la malaria, kama tuki deal na mbu waenezao malaria then masuala ya kua na net za mbu yatakua hayana maana; hivi huoni mtu aliyejirekebisha hapo ni Muhongo na sio hao walikua wakitaka atoke? Muhongo alikua hana IMANI na wafanya biashara wa Tanzania (wawekezaji wa kizalendo) sasa hivi anatenda tofauti na IMANI yake ya zamani, kama ungekua una akili kichwani ungewapongeza walikua wanambishia profesa Muhongo kwakua yeye ndio kabadirika. Leo anawaambia wawekezaji wa Kitanzania kukaa mguu sawa, umeelewa?
 
Moja kati ya sababu za umasiki wa Tanzania and hence Watanzania ni kuto ku deal na chanzo cha tatizo badala yake hua tuna dela na tatizo, mfano tatizo la malaria, kama tuki deal na mbu waenezao malaria then masuala ya kua na net za mbu yatakua hayana maana; hivi huoni mtu aliyejirekebisha hapo ni Muhongo na sio hao walikua wakitaka atoke? Muhongo alikua hana IMANI na wafanya biashara wa Tanzania (wawekezaji wa kizalendo) sasa hivi anatenda tofauti na IMANI yake ya zamani, kama ungekua una akili kichwani ungewapongeza walikua wanambishia profesa Muhongo kwakua yeye ndio kabadirika. Leo anawaambia wawekezaji wa Kitanzania kukaa mguu sawa, umeelewa?
Unapoteza mda wako kuelekeza kopo
 
Wale waliokuwa wana njama za kumng'oa Prof Muhongo wanaaibika sasa
Baadhi ya vigezo vitavyotumika kuwapata Viongozi na Watendaji hao ni hizi kama vifuatavyo: Uadilifu, Uzalendo, Ubunifu na Utaalamu.
Sasa wewe Lizaboni, huoni kwamba Muhongo amebadilika? Zamani hakuwa kabisa anazungumza lugha ya wazalendo, yeye aliamini wawekezaji wa nje ndio wachapa kazi. Leo hii anaalika Watanzania wenye uzalendo. Kwa ufupi, wale mliokuwa mnamshabikia Muhongo enzi zile ndio mnaoaibika
 
Sasa wewe Lizaboni, huoni kwamba Muhongo amebadilika? Zamani hakuwa kabisa anazungumza lugha ya wazalendo, yeye aliamini wawekezaji wa nje ndio wachapa kazi. Leo hii anaalika Watanzania wenye uzalendo. Kwa ufupi, wale mliokuwa mnamshabikia Muhongo enzi zile ndio mnaoaibika
Muhongo amechange for the better na hivyo ndivyo tunategemea viongozi wetu wawe.
 
Muhongo amechange for the better na hivyo ndivyo tunategemea viongozi wetu wawe.
Sawa, sasa wale waliokuwa wakishabikia yale aliyoyafanya zamani, wanaaibika maana wanashindwa kuamua na wenyewe wabadilike au wasibadilike! Mfano ni huyu Lizaboni
 
Tuache porojo porojo hazitatusaidia ,hii ni fursa imeibuka tuichangamkie wenzetu wanakimbia sie bado tunatembea ,tuache mambo yasiyofaa tujikite kwenye mambo ya msingi kwa manufaa ya taifa.
 
Tuache porojo porojo hazitatusaidia ,hii ni fursa imeibuka tuichangamkie wenzetu wanakimbia sie bado tunatembea ,tuache mambo yasiyofaa tujikite kwenye mambo ya msingi kwa manufaa ya taifa.
Tena vigezo viko simple na vinaeleweka...lakini wengine tumeona tu issue ya Makongoro
 
Sawa, sasa wale waliokuwa wakishabikia yale aliyoyafanya zamani, wanaaibika maana wanashindwa kuamua na wenyewe wabadilike au wasibadilike! Mfano ni huyu Lizaboni
Kiukweli tangu awali hakuna mahali Prof. Muhongo alisema au alimaanisha kuwa hawapendi wawekezaji wazawa, bali baadhi ya watu walidhamiria kupotosha kauli zake, aidha kwa kutokuelewa au kwa makusudi. Kwa mfano, kama Tanzania ndio ingekuwa inajenga bomba hili wangependa Prof. Muhongo aseme tenda ya kazi hii ni kwa wazawa tu hata kama hawana uwezo wa kuifikia kampuni ya TOTAL.
 
Kiukweli tangu awali hakuna mahali Prof. Muhongo alisema au alimaanisha kuwa hawapendi wawekezaji wazawa, bali baadhi ya watu walidhamiria kupotosha kauli zake, aidha kwa kutokuelewa au kwa makusudi. Kwa mfano, kama Tanzania ndio ingekuwa inajenga bomba hili wangependa Prof. Muhongo aseme tenda ya kazi hii ni kwa wazawa tu hata kama hawana uwezo wa kuifikia kampuni ya TOTAL.
It was loud and clear, "Wazawa uwezo wao huko kwenye kuwekeza kwenye viwanda vya juisi".

Lakini kauli zake za karibuni zimekuwa za kurithisha.
 
Back
Top Bottom