Kumekucha: Maji kutoka Ziwa Victoria mpaka Dodoma

I am Groot

JF-Expert Member
Jul 20, 2018
3,727
10,023
Katibu Mkuu Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo amesema Wizara hiyo inatarajia kufanya utafiti mkubwa na usanifu wa mradi mkubwa wa maji wa kuchukua maji kutoka Ziwa Victoria kupeleka Mkoani Dodoma kwa kupitia Mkoani Singida katika mwaka wa fedha wa 2020/2021>>”hii itaondoa kabisa shida ya maji Dodoma na Singida”

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Prof.Kitila Mkumbo alitoa kauli hiyo kwenye hafla ya kupokea mabomba ya maji ambayo ni sehemu ya Programu kubwa inayotekelezwa kwa nchi nzima katika mikoa 17, Singida ikiwa ni moja ya Mikoa hiyo.

Mkumbo amesema fedha za mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kupeleka Dodoma kupitia Singida tayari zimetengwa katika bajeti ya mwaka huu wa fedha, hivyo anaamini kipindi cha miaka 5 ijayo Singida na Dodoma wanaweza kupata maji kutoka Ziwa Victoria.

Source; millard ayo
 
Ndio yale yale ya maji kutoka arumeru mashariki na kupelekwa monduli wakati raia huko arumeru mashariki hawajui maji ya bomba yakoje.
Hayo maji ni ya Arumaru Magharibi mkuu ya Lowassa hadi leo wananchi wa maeneo hayo ya arumeru wanasikia tu pump zikinguruma kupeleka maji wameachiwa vumbi
 
Endapo Jambo Hili Litafanikiwa Hakika Ndugu Zangu Dodoma
Kutumia Maji Ya Visima Toka Mzakwe Itabaki Story
Huu Mradi Ulikuwa Unasemwa Zamani Sana


Dodoma Pia Tutachimba Mtaro Wa Maji Bahari Toka Dar es salaam Yaende Dodoma
 
Juzi kwenye taarifa ya habari nimeona wananchi wa mara wanalalamika hawana maji wakati wapo karibu na ziwa inakuwaje maji yanapelekwa mbali wakati waliozungukwa na maji wanalalamika
Tatizo matumizi ya ya hayo maji. Egypt wanatumia maji ya mto Nile ambao chanzo chake ni ziwa Victoria na wao chanzo hicho ni zaidi ya 90% ya maji wanayotumia. Sasa unashangaa Mara?
 
Mnataka kutumia loophole ya mtifuano uliopo kati ya Misri na Ethiopia, au mnafikiri hao jamaa wamelala....hizi ahadi huwa zinatoka sana kuelekea uchaguzi, lakini mara nyingi hazina uhalisia..

Misri hawawezi kutifuana na sisi,, kwa mradi tuliowapa wa Bwawa la Umeme lazima watakaa kimya. Ila pia ni ujinga eti upo na chakula unakilinda then unakufa njaa wakati jirani yako anakuja anakula na kushiba hicho hicho unacholinda.

Mikataba mingine ni wehu mtupu!!
 
Ushauri kwa wizara.

Wangefuata utaratibu kama wa REA ili baada ya hayo mabomba makubwa kutandazwa na hao wachina na wahindi hizo mamlaka za maji za miji husika zikikabidhiwa miradi zitafute wakandarasi wa kusambaza nyumba kwa nyumba kwa maana wao wanaelemewa kutokana na maombi kuwa mengi matokeo yake inachukua muda mrefu mno watu kuunganishiwa.

Hizo mamlaka zina uhaba wa resources ikiwemo wafanyakazi wa kuendana na mradi mkubwa kama huu nimeona pale Isaka wako slow mno.
 
Mnataka kutumia loophole ya mtifuano uliopo kati ya Misri na Ethiopia, au mnafikiri hao jamaa wamelala....hizi ahadi huwa zinatoka sana kuelekea uchaguzi, lakini mara nyingi hazina uhalisia..
Wakumbushe tu kuwa wenzetu husimamia mikataba pale Mwanza kuna wamsiri kabisa na ofisi zao kwa ajili ya kutoa ripoti kwa serikali yao kile kinachoendelea pale ziwa Nyanza
 
Back
Top Bottom