Kumbe Zanzibar ina Katiba yao, Msikilize Hussein Mwinyi

Kumbe Zanzibar ina Katiba yao, Msikilize Hussein Mwinyi

Kumbe ulikua hujui, zazibar sio mwenzio kabisa, taifa la watu 1.8m anatoka moja anakuja kuongoza taifa la watu 65m, lakini hamna wa kutoka kwenye taifa la 65m atawale taifa la 1.8m....huo ni udhalimu wa hali ya juu.
Bora hata buyu Lina mbegu ndani lakini siyo bichwa lako
 
Zanzibar ni nchi ilio ungana na Tanganyika ina kila sifa kama nchi kamili. Unatakiwa ushamgae kumbe Tanganyika haipo na katiba haina.
 
1762814607656.png
 
1. Ina katiba yake ila Tanganyika haina katiba tunatumia ya jamuhuri ambayo hailindi maslahi ya watanganyika.
2. Ina Bendera yake sisi ya Tanganyika tumeweka kabatini.
3. Rais na makamo wake, sisi hatuna raisi wala serikali ya tanganyika wala mawaziri wala wabunge.
4. Wana mamlaka zao kamili kama mamlaka ya mapato ZRA sisi tanganyika ukitoa TLS hakuna kitu tunamiliki.
5. Wanazo ofisi za BOT sisi tanganyika hatuna.
6. Wana vitambulisha vya taifa la zanzibar sisi tanganyika hatuna vitambulisho vya taifa letu.


ila wanataka kutumia mapato na rasilimali za tanganyika kwaajiri ya maendeleo yao binafsi katika kivuli cha jamuhuri ya muungano. Huu upuuzi tuukatae kuanzia sasa. Kama kusomesha wazanzibar kwa gharama za kodi za huku.

Kodi tunazolipa huku wakati wa kuingiza vitu kama magari na mizigo kule hawana hicho kitu, gharama zao kule ni nusu ya za huku. wewe una nunua IST milioni 17 nenda kaulize Zanzibar ni bei gani. Umeme kaulize ni kiasi ganiwanalipia? Kaulizie bundles za internet wanalipia kiasi gani kule?

Tudai tanganyika yetu, ipate katiba yake na bendera yake ipepee upya na tuanze na maisha yetu mapya bila CCM.


hii video ni dedication kwa watanganyika wenzangu wote. Simba kaamka anataka territory yake.
 
1. Ina katiba yake ila Tanganyika haina katiba tunatumia ya jamuhuri ambayo hailindi maslahi ya watanganyika.
2. Ina Bendera yake sisi ya Tanganyika tumeweka kabatini.
3. Rais na makamo wake, sisi hatuna raisi wala serikali ya tanganyika wala mawaziri wala wabunge.
4. Wana mamlaka zao kamili kama mamlaka ya mapato ZRA sisi tanganyika ukitoa TLS hakuna kitu tunamiliki.
5. Wanazo ofisi za BOT sisi tanganyika hatuna.
6. Wana vitambulisha vya taifa la zanzibar sisi tanganyika hatuna vitambulisho vya taifa letu.
Huu ni mtego.. nafikiria muundaji wa huu mtego alikua na akili iliyojificha ikafichwa ikafichika isionekane ila hajawahi kueleweka alikua anamaanisha nini na watanganyika hawajawahi kuambiwa nini haswa maana yake ndio maana wengi wamebakiwa na viulizo kwamba ....
 
Back
Top Bottom