@ Njilemera: Ninashukuru kwa jinsi ulivyojaribu kulinganisha wajibu wa BJMT na BMK katika kutunga sheria. Aidha pia nimefurahi umeweka wazi kwamba kuna tofauti kati ya sheria za kawaida zinazotungwa na BJMT na katiba.
NInapo tofautiana na wewe (na wengine wanao unga mkono UKAWA) ni kwenye swala la uzito wa rasimu iliyopendekezwa!
Ni mtizamo wangu kuwa kwenye sura na vifungu vya muundo wa Muungano, Rasimu HAIKUWAKILISHA MAONI YA WANANCHI WALIO WENGI!
Kwenye eneo hilo Rasimu imewakilisha TAFSIRI ya Warioba na wenzake kuhusu maoni ya wananchi- Tafsiri ambayo haiungwi mkono na kanuni yoyote ya kitakwimu (Yes… Ninajua hizo kanuni na nimezifundisha katika ngazi ya chuo kikuu – kama unataka kujua!)
Kwa mujibu wa takwimu; takwimu za tume ya Warioba zinaonyesha kwamba ni asilimia 8.36 tu ya waliotoa maoni ndio walio gusia na kusema wanataka s3… alichojaribu ni ku "Draw inference" kutoka kwa hawa waliosema wanataka s3… si sahihi inapokuja kwenye Population nzima!
Swala la "Ni nini hasa maoni ya wananchi walio wengi" ndilo linalogomba!
UKAWA wanadai 8% ya wote waliotoa maoni NDIO maoni ya wananchi walio wengi! – inaleta shida kuelewa!
Ukweli ni kwamba kwa wananchi walo wengi; LA MUHIMU kuliko chochote kingine ni 1. Huduma bora za Jamii, na 2. Uongozi Bora (in that order!) UKAWA kwa kutumia kanuni rahisi sana ya "the Loud minority" wanataka tukubaliane nao kwamba "Muundo wa Muungano" is everything! Wanadharau kabisa ukweli kwamba la Muhimu kuliko yote ni "UONGOZI BORA" (utakaopelekea siasa safi na mikakati yenye ufanisi) Bila Uongozi bora hata uwe na s10… bado maisha ya mwananchi wa kawaida yataendelea kuwa mabaya!
Wanaounga mkono UKAWA wameshupalia kwamba wanaozuia uwepo wa katiba ni CCM… sidhani Hivyo!
Aidha kuna tatizo katika kudhani kwamba KILA anayepinga UKAWA ni CCM – hilo ni dhahiri ingawa wengi wanaendelea kulitangaza Hivyo!
Tatizo hapa sio wanapinga uhalali na msimamo wa UKAWA… tatizo ni UKAWA!
Kwa UKAWA kushinikiza kwamba hawarudi BMK hadi wanachotaka wao Kiwe – ni kujaribu kuteka nyara uhuru wa kujadili hiyo rasimu.
Kwa waTz wenye mawazo kama yangu, NILITEGEMEA sana mijadala ndani ya BMK inisaidie kuelewa umuhimu, ulazima na uhalali wa s3… UKAWA wananinyima haki hiyo kwa ku LAZIMISHA BMK liwe rubber stamp ya rasimu (ambayo kwa mawazo yangu imekaa kushoto kwenye swala la Muundo wa Muungano). Kama mTz SITAKI BMK liwe rubber stamp! UKAWA warudi bungeni; Toeni hoja zenu! Wasikilizeni na kuwapinga wanaopinga msimao wenu KWA HOJA!
Aidha
Bila kuwa kisheria zaidi, Uwepo wa UKAWA hauna uhalali wowote kwa mantiki ya faida kwa wananchi wa kawaida.
Kwa baadhi yetu, Wanachofanya UKAWA ni USALITI mkubwa kwa wananchi tuliowatuma kutuwakilisha! – (MB wangu amesimama na UKAWA)
Ukweli ni kwamba; wanachofanya UKAWA ni kutelekeza wajibu wao kama viongozi wetu! Kwa wao kukataa kurudi bungeni, wanatunyima uwakilishi kwenye BMK! – Binafsi hili SILIPENDI KABISA! Kiongozi wa watu ANALAZIMIKA kuwa tayari kufanya majadiliano! Nina ogopa sana "kiongozi" asiyetaka kujadiliana… Laiti Mhe. MB wangu angeliona hili!
BMK linaendeshwa WAZI!- na KILA mwananchi ana uwezo wakuona kinachoendelea! UKAWA wasidhani wananchi hawana akili! UKAWA warudi bungeni… Kama kuna kufanyiwa ambavyo sivyo…– si wananchi wanaona? Kuna kura ya maoni, na mwakani (2015) ni uchaguzi mkuu! WaTz sio mbumbumbu kama mnavyodai! Wana uwezo wa kuamua! Heshimuni japo hilo… Ndio demokrasia!
Wengi wa waliobaki UKAWA (Idadi yao imepungua kutoka walivyokuwa mwanzo), ni wabunge wa kuchaguliwa! Sijui ni nani "strategist" (mpanga mkakati) wa upande wa wasio UKAWA. Ila ningekuwa mimi, msimamo wa UKAWA ni mtaji tosha!