Kumbe UKAWA walikuwa Wanatupotosha?

Kumbe UKAWA walikuwa Wanatupotosha?

Watapotoshaje wakati hiyo rasimu ilikuwa inapatikana bure kwenye mitandao, labda wewe ndo wamekupotosha.

Nasikitika wanaopenda kuambiwa na si kujisomea wao wenyewe kama wewe ni wengi kweli.

Ngoja wakale tena mabilion mengine wengine tuendelee kulia tu.
 
Ni kweli Bunge Hutunga SHERIA na ni kweli Bunge Maalumu la Katiba linatakiwa kutunga Katiba (lakini iliyopendekezwa!).Uhalisia katika mabunge yote mawili ni kuwepo kwa draft/rasimu. Kwa Bunge la kawaida, serikali kupitia wizara ya sheria huandaa Bill ambayo hupelekwa bungeni kwa kujadiliwa, kama bunge litakubaliana nayo huwa ni sheria, ikifanyiwa maboresho mengi basi hurudishwa kwa serikali na ikingangania bunge huvunjwa. Kwa tafsiri hii rasmi ni jambo la kawaida tu kama bill yeyote kwa bunge (tofauti ni kwa kuwa hii ni sheria mama, uandaaji wa bill/rasimu ushirikishe wananchi kupitia kazi ya tume. Haiwezekani kamwe BMK likafanya marekebisho makubwa au kuibadili halafu zoezi likaendelea, itabidi irejeshwe kwa Tume! Tafsiri anayotoa mleta hoja hapa na zile za CCM inadhamiria kubadili rasimu kuwa kitu kingine nje ya maoni ya awali ya wananchi.

Kinachotegemewa na WATU WA AINA YA CCM ni kuburuza ipatikane Katiba na kwenye kura za maoni kazi kubwa iwe ni uchakachuaji. Kinachoogopwa ni kuwa na katiba isiyokidhi mahitaji ya CCM

Mkuu,
Acha ndoto za Tume ambayo haipo tena kisheria, Rasimu haitarudi kamwe kwenye Tume "hewa!"
Marekebisho "makubwa" au "madogo" yatafanywa na Bunge na si vinginevyo!
 
Watapotoshaje wakati hiyo rasimu ilikuwa inapatikana bure kwenye mitandao, labda wewe ndo wamekupotosha.

Nasikitika wanaopenda kuambiwa na si kujisomea wao wenyewe kama wewe ni wengi kweli.

Ngoja wakale tena mabilion mengine wengine tuendelee kulia tu.
Sijajua uhusiano kati ya upatikanaji na upotoshwaji wa Rasimu ni upi!
 
Credibility yake huyu DHAIFU ni SIFURI, kwa watu wasiojitambua kama wewe ndio wanaweza kumuamini, lakini kwa wale ambao wanajitambua kama SAS hawaoni aibu kumkosoa hadharani kama chanzo cha kuharibu mjadala wa kupatikana katiba mpya.

JK kafafanua hili la kupewa taarifa ya kila kilichokuwa kinaendelea, halina mashiko tena!
Tafuteni singo nyingine!
 
Credibility yake huyu DHAIFU ni SIFURI, kwa watu wasiojitambua kama wewe ndio wanaweza kumuamini, lakini kwa wale ambao wanajitambua kama SAS hawaoni aibu kumkosoa hadharani kama chanzo cha kuharibu mjadala wa kupatikana katiba mpya.
Kosa la JK liko wapi hasa ukizingatia Hotuba murua ya jana?
 
Hivi hii ID ilikuwa moderator???!!
Sikuchukii lakini kwa uandishi wako kama ulikuwa mod basi hukutakiwa kuwa!!!! Au umebadilika baada ya kumaliza???!!!

Kwa nini usiandike in a neutral manner wasomaji ndio waseme kama wanapotoshwa au laa???!!!

Mkuu umenena, huenda jamaa alikuwa m-ban cd. kisa anauzoefu wa kuchezea mouse ndo akapewa kazi.
 
Ungekuwa unajitambua ungeelewa kosa la DHAIFU pamoja na hotuba ya jana. Hata kabla ya hotuba ya jana hukuwahi hata siku moja kupinga MACCM wenzio kuhusiana na mjadala wa katiba.

Kosa la JK liko wapi hasa ukizingatia Hotuba murua ya jana?
 
Weye ndo unayetaka kuupotosha uma kuwa UKAWA ni wopotoshaji. Tamka wazi kuwa maccm ndo wanapotosha uma. Wamepata wapi rasimu hiyo wanayoitetea ya serekali 2?? Au wanafuata tu maneno ya m/kiti wao kuwa 3 zitaleta vita?? Maneno ya kukaririshwa jamani hayana mashiko.
Waacheni wajadili serekali zao 2 lakini kuna siku, watalipa hizi kodi wanazo jilambisha bila matokea. Warudi njia kuu, mchepuko siyo dili. Waache kudharau mawazo mama ya wananchi. Mengineyo yoote ni mchepuko tu. Kama wanataka kupinga rasimu ile ya Warioba, waipinge yoote, wamrudishie Warioba akakusanye upya si wao kutoa za mifukoni na kuwasilisha BMK.
 
Jk ana taaluma gani kweli?

Eti walidai kuwa Rasimu ilitakiwa "iboreshwe" tu na sio kubadili chochote!
JK amewapatia akina Tundu Lissu na wenzake vifungu kimoja baada ya kingine! Kinachowapa shida sasa hivi UKAWA ni namna ya kufuta uongo wao!
Hongera JK, umekuwa smart sana kuhusu Katiba Mpya so far!
 
Jk elimu ya sheria hajui kabsa.Muulize uchumi nao ali-sap mpaka paper la mwisho
 
Warudi tu waache kutupotezea muda tunahitaji katiba mpya that all
 
Weka hapa CV ya JK, Nchemba, Wasira, Nape and Jr Makamba, na zile za Judge Warioba na wajumbe wote wa tume pamoja na za viongozi wa UKAWA, tuone ni nani ana sifa na utaalamu wa katika masuala ya katiba!. Acheni kuzungumza kama wote mmesoma elimu ya madrasa kiasi kwamba hamtambui hata maana na umuhimu wa elimu na taaluma za watu.

Kwanza JK ana taaluma gani? Uraisi wenyewe wa magumashi. Nani asiyejua kwamba uchaguzi wa 2010 alitupwa mbali sana akachakachua? Anadhani alivyochakachua kwenye uraisi wake na katiba atachakachua? Wananchi wa Tanzania wamesema sasa basi!l Na asijidanganye.



JK amewapatia sana UKAWA!
 
Ungekuwa unajitambua ungeelewa kosa la DHAIFU pamoja na hotuba ya jana. Hata kabla ya hotuba ya jana hukuwahi hata siku moja kupinga MACCM wenzio kuhusiana na mjadala wa katiba.

Kosa liko wapi mkuu, acha danadana za ki-UKAWA!
 
Eti walidai kuwa Rasimu ilitakiwa "iboreshwe" tu na sio kubadili chochote!
JK amewapatia akina Tundu Lissu na wenzake vifungu kimoja baada ya kingine! Kinachowapa shida sasa hivi UKAWA ni namna ya kufuta uongo wao!
Hongera JK, umekuwa smart sana kuhusu Katiba Mpya so far!

Hivi Katiba mpya inaandikwa na Watawala au inaandikwa na wananchi?

Kama ni Katiba ya wananchi na ni mawazo ya wananchi, kwa nini watawala wanataka kuweka vitu ambavyo wananchi hawakivisema?

Fikiri mara mbili mbili.
 
Back
Top Bottom