Haioneshi uchawi uko wapi? hiyo ni moja ya "complications" za uja uzito. Kambana mtoto tumboni na nguo za harusi ili kitumbo kisitokeze na hayo ndio matokeo yake.
Hakuna chochote kinachoonyesha kwamba uchawi upo hapo.
Inawezekana dada alikuwa na matatizo yake na saikolojia ya "matrimony anxiety" ika triger matatizo ya kiafya.
Nitakupa mfano.
Mie kila siku nasema humu kwamba siamini any supernatural power, siamini mungu, shetani. malaika au uchawi.
Akaja dada mmoja akasema atanipiga "al-badiri", kiutani.
Nikaenda kulala. Nikalala na headphones kubwa, nasikiliza "BBC World Service", katika utamu wa dreamworld kusikiliza BBC nikajikunja vibaya, nikaulalia mkono. Kuamka asubuhi, nimeulalia mkono, mkono unaniuma kichizi, yaani I am talking about agony.
Sasa hapa kama mie mtu wa kuamini uchawi, mungu na al-badiri, ni rahisi sana kuona mie kuumwa mkono ni al-badiri imenipata na inaanza kuni badili polepole.
Bahati nzuri siamini mambo hayo.
Nimejitahidi kusoma post vizuri nijue labda kuna habari mpya za kunionyesha uchawi upo, nikakuta watu wanaogopa vivuli na wanaweza kuabudu coincidence kama uchawi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.