Kumbe ITV ni hata Mwanza?

Kumbe ITV ni hata Mwanza?

Imegeuka kuwa TV ya taifa. Nilikuwa mwanza kwa siku 10, nilikuwa nahama hotel na bar kila siku, kila ikifika saa 2 usiku wateja wote wanaomba wawekewe taarifa ya habari ya ITV sio tv nyingine yoyote ile.


Ilifanya kazi kubwa sana mwaka 1999 wakati wa kifo cha Baba wa Taifa,
 
Kuna kitu kinaitwa ITV Syndrome kwa watanzania Karibu wote kwasababu TV ziliporuhusiwa kumilikiwa na watu binafsi ITV ni miongoni ya TV za mwanzo kabisa.

Hata huo mlio au melody ya taarifa ya habari haijawahi kubadilishwa toka wameanza na wamekuwa na habari nyingi nzuri toka mwanzo wakazoa watazamaji wengi dar na mikoani.

Na ilichukua watangazaji na waandishi wengi toka Redio Tanzania ya Serikali.
 
Hiyo me mwenyewe nimeiona maeneo yote niliyopita Kanda ya ziwani kila saa mbili ni automatically wanatune Itv habari na muandishi ambae walikua wanampenda sana ni Sam Mahela na walikua wanashangilia kabisa hasa zile swagga zake za uhitimishaji maeneo ya kahawa.
 
Kwa sasa Azam two wanaongoza hawabagui taarifa zao nimeona itv wameiga ile style ya azam ya kusoma habari na kuweka matangazo katikat hawana tena habari za kitaifa sijui mataifa ni mchanganyiko like azam,.
 
Wachache sana wanaongalia taarifa ya habari now, habari zote unakuwa umeshazipata hapa hapa JF.
 
Kuna kitu kinaitwa ITV Syndrome kwa watanzania Karibu wote kwasababu TV ziliporuhusiwa kumilikiwa na watu binafsi ITV ni miongoni ya TV za mwanzo kabisa.

Hata huo mlio au melody ya taarifa ya habari haijawahi kubadilishwa toka wameanza na wamekuwa na habari nyingi nzuri toka mwanzo wakazoa watazamaji wengi dar na mikoani.

Na ilichukua watangazaji na waandishi wengi toka Redio Tanzania ya Serikali.
Ukitaka biashara yako idorore iwekee ushabiki wa vyama vya siasa
 
Hawana uwezo wa kuifikia TBC kwenye habari na weledi..
 
ITV inapendwa sana!
Nimewahi kuishi Mwanza hilo nalijua vyema kabisa ilinifanya niwajue watangazaji wake wengi sana akiwemo Rehema Mwakangale(R.I.P), Fatma Almasi Nyangasa, Albert Nitwa, Mzee fulani wa kipindi cha kipima joto(nimemsahau jina) na wengineo.........
 
Back
Top Bottom