Kumbe freemasons ni watu poa sana!

Kumbe freemasons ni watu poa sana!

Wenye namba za simu zifuatazo 0765552597 na 0693212509 waache kushawishi watu kujiunga freemasons
 
Ukweli ni kwamba freemason hawapingi Mtu kuwa wa dini yoyote na ndio maana moja wapo ya sharti lao kuwa member lazima uwe muumini wa hizi mainstreaming religion na hii ni kwa sababu wanataka watu wanaoamini kuhusu divine being (God or gods) maana kama huamini kuhusu divine being hata wao utawasumbua maana kuna Mambo ya kiibaada za kishetani itabidi itabidi ufanye so kama huamini kuhusu Superior being in spiritual realm hata shetani hutamwamini pia na kinachotakiwa hapo ni imani kwa hiyo huwezi kuendana nao na ndio maana freemason yoyote unayemjua lazima utakuta ni muumini mmoja wapo wa hizi mainstreaming religion kuanzia yule mkuu wao kwa Tz (maana anajulikana wala sio siri) mpaka member wengine wa kawaida, kiufupi ni watu wanaojua nini wanafanya na wameamua kumuabudu Lucifer kama Mungu wao kwa hiari with full understanding wa kile wanachokifanya.

Sasa kuna mtu anashangaa inawezekanaje kusali kanisani au msikitini na bado kuwa Freemason, mpendwa inabidi utambue kuna Dini na Imani, Dini ni mfumo waliojiwekea wanadamu katika kumtafuta Mungu, lakini kumbuka hakuna aliyewahi kumwona Mungu, na ndio maana mfumo wa dini moja ni tofauti na nyingine, maana yake ni nini sasa, maoni na mawazo ya waasisi wa dini zetu (sio imani) katika kumtafuta Mungu ingawa huenda ni kwa nia njema, yalitofautiana kulingana na kila mmoja alivyokuwa na idea yake kumhusu Mungu na namna gani ya kumuabudu kwa kumpendeza.

Lakini imani ina asili ya uungu, au naweza kusema ndio mpango halisi wa Mungu kumtaka mwanadamu amuabudu katika namna gani ambayo inampendeza, ndio maana mtu hata asipokuwa muumini wa hizi mainstreaming religion kuna kitu kingine atakuwa anakiabudu na kukiamini maana ibada na imani ni asili tuliyoumbiwa lakini Dini tumejitengenezea wenyewe (sijasema ni mbaya) kwa makusudi mbalimbali maana kila Dini (sio imani kumbuka) inategemea mwanzilishi wake alikuwa na mtizamo na makusudi gani kuianzisha.

Kwa hiyo inawezekana kabisa akawa muumini mzuri tu wa Dini fulani, na kwa sababu ya nature ya jamii tunazoishi (maana mtu akiwa anaenda kwenye nyumba za ibada hata kwenye jamii ni mtu anaechukuliwa amestaarabika na ana utu fulani), Lakini IMANI yake sasa imejengwa katika kitu kingine tofauti na huko unakomuona kila siku za ibada yupo. Maana freemason ni kama uchawi kwa mantiki ya kujificha (mazingara ombwe) na ndio maana zinaitwa secret societies zikiwemo Skull and bones society n.k). Why they do called secret societies? Kuna siri gani hapo ingawa hili ni somo refu lakini siku nikipata muda nitakueleza sio tu imani yao na siri pia zilizojificha kwao.

Na katika uchawi wenye nguvu kubwa ni wa hawa members ni wachawi wa high quality, hakuna tunguli,sijui kujipaka majivu, masizi, sijui kuruka ungo, wao utawakuta na suti yake safi huku anasukuma v8 yake, kinachowapa nguvu sana kuliko wachawi wengine ni ule mkataba walioingia katika kumtumikia moja kwa moja Lucifer kama Mungu wao huku wakielewa kile wanachokifanya, kwa hiyo hupokea nguvu yao moja kwa moja kwa Lucifer mwenyewe na mashetani wakuu maana tayari waliwahi kuwa waaumini katika Dini zao na walifundishwa habari za Mungu tofauti na Lucifer ila kwa hiari wakamchagua.

Nina mengi ya kusema kuhusu hivi vyama lakini kiukweli kuna ushetani mwingi unafanyika huku,sema watu hawafahamu wao ukiwaambia freemason picha inayokuja ni watu wenye pesa na mafanikio ya kidunia(sipingi kuwa hawana) lakini behind hizo pesa na hayo mafanikio hakuna anayejua nini kinaendelea na hawawezi kujua maana hata member wenyewe wanaviapo zaidi ya vitatu vya kutokutoa siri, ndio maana leo hata umkamate member mmoja umwambie tunakuua au useme kila kitu, nakuhakikishia atakakimbilia kitanzi kuliko kusema, ingawa naonaga humu JF kuna watu wanajaribu kuelezea lakini ukisoma vizuri utagundua, they know nothing kuhusu hawa monsters au wanagusa vitu vile vya juu juu tu ambavyo hata wao huruhusu watu wengine wavijue maana haviathiri maslahi yao, lakini ukipagusa penyewe nakuhakikishia uwe umejipanga vizuri maana hata wao wamejipanga kuilinda siri yao kwa gharama zote na hii niliwahi kusema na ninarudia tena kuwa uchawi una kawaida ya kukosa nguvu kwako unapofunua siri yake maana uchawi ni kujificha (mazingara ombwe) ukiufichua huwa unakawaida ya kupoteza uwezo wake kwa mhusika.

Lakini niwatahadharishe usije kuona mtu tajiri anatikisa jiji au nchi kabisa halafu ni member nyuma ya hizo mali kuna Nafsi nyingi sana,zisizo na hatia zimedhurumiwa uhai, maana watu wanafikiri freemason ni moja, ila ndani kuna vitengo mbalimbali kikiwemo cha machinjo na kusababisha ajali na magonjwa ili kupata damu maana ufalme wa giza umeimarishwa kwa kafara za damu za wanadamu, kuna illuminate ingawa wengine wanafikiri hiki nacho ni chama cha siri lakini sio kweli ila hiki ninaweza kusema ni kitengo cha intelligence na mastermind katika freemason huku ndio utakuta ma genius wanaopanga mikakati ya kidunia, dunia iendeje?, nini kifanyike? ili kipi kitokee na kwanini isiwe vile?, huwa mnasema JF the home of great thinker lakini hamjui msemalo (utani tu [emoji16]) ila maana yangu ni kuwa kule ndio kuna watu ni wanadamu kama wewe ila mpaka leo hata mimi huwa najiuliza hivi ni wanadamu 100% au kuna namna.
Msione sijui matukio ya kigaidi sijui waasi wa wapi sijui pandemic gani ya kiulimwengu ndugu yangu havitokei by nature, kuna watu kabisa wanaopanga nani apigane na nani ili iwe hivi, nani amuue nani ili kitu fulani kitokee, ingawa kuna vingine vinaonekana vimekaa kiimani zaidi (mf.ugaidi) , lakini hiyo ni danganya toto behind the scene kuna mastermind na ma great thinker wameplan ili kije kitokee kitu fulani kwa lengo fulani ili kutimiza matakwa yao ya kuutawala ulimwengu.

Sasa mwingine atajiuliza kama wanauwezo wa kufanya hayo yote wanashindwaje kuutawala ulimwengu, labda hufahamu hiki kitu nikujuze, kiukweli ulimwengu uliumbwa na Mungu pamoja na vitu vyake akiwemo mwanadamu, kwa hiyo ulitengenezwa katika namna ya ku favour utawala wa kiMungu au mamlaka za nuruni ndio maana watu kwenda ibadani kusali akiwa na Bible yake sio shida, kufanya mikutano ya hadhara ya injili nijambo lakawaida ila je uliwahi ona wachawi au freemason wanafanya ibada zao au mambo yao hadharani, hata tu elimu ya giza haipatikani kirahisi kama unavyoweza enda Sunday school ukafundishwa habari za Mungu, hii ni kwa sababu nature ya ulimwengu tuliopo haijaweza kubeba ushetani wa kutosha ili igeuke iwe ya giza ili wao waitawale wanavyotaka maana wao ndio wenye mamlaka ya gizani ndio maana kuna mambo yao kutoka sheol mengine hupingwa na wanakuwa hawana uwezo wa kuforce(mf,ushoga),

Ila mkakati upo wa kuitawala na mpaka saa hizi unatekelezwa ila kuna watu wanazuia kwa namna fulani (ingawa sipo kidini) maana siko hapa kutetea dini yoyote au imani fulani ila naelezea ninachokijua

Kuna watu wa imani fulani huwa wanaomba sana [emoji2960] na kufunga tena wakati mwingine kwa kukemea na kuvunja kabisa kwa jina fulani. Hawa ndio kikwazo kikubwa kwa sababu katika kunena kwao kuna mipango mingi huwa inaharibiwa na hata kama imeanza kutekelezwa huwa inafell na ndio sababu wakaundiwa kitengo maalum katika freemason (sitakitaja kwa jina kwa sababu fulani) ambacho hu deal na watu wa imani hii na katika nyumba zao za ibada kuwaharibu na kuzisambaratisha ili wasielewane na ile nguvu ya maombi yao ipotee ili watimize mambo yao ,usione leo pastor kazini na muumini wake ukafikiri ni tamaa tu ya kawaida ya kibinadamu au anatoa mpaka rushwa ili awe askofu au ana wake wawili, ndugu mambo hayatokei hivi hivi, hapo mtu kaishatumiwa swaibu zinaa [emoji16] mapema sana linamuendesha tu, usione kwaya zinavunjika kwa sababu ya zinaa (something is working behind physical reality).

Sasa utajiuliza mtu wa Mungu inawezekanaje akatumiwa jini likampata, kuna siri kubwa sana hapa unakuta mpaka kufikia kumshinda hivyo wamemuwinda karibu miaka 3 mpaka 5 maana sio kazi rahisi kama unavyofikiri na jini kwa mfano wa zinaa anayetumwa kwa mtumishi fulani wa Mungu aliyesimama ni tofauti na yule anayetumwa kwa kabinti fulani hapo mtaani kwenu maana ingawa kazi ni moja lakini yanatofautiana sana kwa nguvu na uwezo wa kiutendaji(somo lingine), na kibaya anayewindwa hajui kama anawindwa, kwa hiyo kupitia mistake zake ndogo ndogo akiteleza tu wanaye[emoji17], na hakuna kitu kigumu kama kushindana na adui usiemwona na hujui kama akuwinda ndio maana tunatakiwa kuomba toba kila wakati ili Mungu asiondoe ulinzi wake kwa sababu ya dhambi zetu, maana laiti ungeona watumishi wa Mungu waaminifu wanavyowindwa nakuhakikishia usingetamani hata kuifanya hiyo kazi maana wewe ndio unakuwa main target yao, Ndugu usikimbilie kuanza huduma au kanisa kabla hujapokea nguvu ya kutosha labda kama unawafanyia wao (wanangu wa keki ya upako mikono juu[emoji16]), ila Mungu ni mwaminifu anawatetea sana na ndio maana hata katika harakati za kumuangusha au kumuua lazima mnakuwa makini maana kufa ni kugusa Maana Mungu hana utani kwa watu wake potential, Maana kitendo hata cha kumtaja tu jina kilingeni (madhabahu ya kichawi) mnaweza kufa kama mende kwa huo moto utakaowalipukia kwa hiyo ni vita hasa na ni hatari pia kwa upande wa muwindaji.

Na ndio maana saa hizi wanamkakati mpya unaitwa mpango mpya wa Dunia New world order huu ni mkakati wa kuipanga Dunia upya tofauti ilivyopangwa na aliyeiumba ili iweze kubeba ushetani wa kutosha, kuwezesha itawalike na hawa monsters ila shida ndio hao wanenaji ni waharibifu sana [emoji16] wa hizi mambo halafu wao hawajui kama wanaharibu na ndio maana wanawachukia sana kule [emoji23], yaani akisema nasambaratisha, kama yupo muhusika humu nafikiri atakuwa shahidi mzuri wa nini ambacho kinaendelea behind the scene ni kusaambaa haswa hakibaki kitu, maneno ya kinywa ni silaha hatari sana yakitumika kwa maarifa na imani kamilifu sema wengi wao hawajui na ni kwa sababu hawaoni kinachoendelea ule upande mwingine.

Inshort freemason ni pana na wengi wanaojaribu kuilezea wanajua vichache sana kuhusu hawa Monsters, lakini kwa jinsi ninavyowaelewa huwezi toa siri yao hata moja kama navyoona nyuzi za humu JF wakuache uendelee kula ugali[emoji16] hata kama una Mungu lazima watakusumbua mpaka ujute sema ambacho hawataweza ni kukuterminate kwa sababu ya nguvu inayokulinda, tofauti na hapo wewe ni supu yao ya asubuhi.

Lakini utashangaa kuna mtu eti anatoa uzi wa siri za freemason humu na anaandika muendelezo wa uzi wake kabisa, mi huwa nasoma nacheka tu maana hakuna siri yoyote wanatoa zaidi ya porojo nyingi, maana navyowajua wale wadau unatoa siri yao hujajipanga wanakupoteza.

Source: Elimu changa [emoji3]

#Zakuambiwachanganyanazako

Hahaha so wewe umejipanga mkuu?
 
Mungu ni upendo, na upendo ni kuwatendea kwa haki hao unaowapenda. Upendo ni matendo. Will ya Mungu ni sisi tupendane

Simple.
Kama matendo yako ni kujifaidisha mwenyewe kwa kuwatia maumivu/hasara wenzio basi huo ndio ushetani. Huhitaji kusaini mkataba wala nn. Mfano mwanasiasa mwizi na mjasiriamali anayepima ki feki na wiziwizi. Umekiuka will ya Mungu

Na ikiwa matendo yako ni kunufaika na kunufaisha wapendwa basi wewe ni wa Mungu machoni pa Mungu na wanadamu. Hauhitaji kusaini wala. Haya mambo ni ya kiroho. Mfano mwanasiasa mzalendo na mjasiriamali anayepima kihalali na orijino. Umeendana na will ya Mungu.
 
Wenye namba za simu zifuatazo 0765552597 na 0693212509 waache kushawishi watu kujiunga freemasons
Mh hawa ni wale matapeli, kama wako siriazi me nataka kujiunga huko, mnicheki inbox [emoji400] iko free
I wanna join the team
 
Mungu ni upendo, na upendo ni kuwatendea kwa haki hao unaowapenda. Upendo ni matendo. Will ya Mungu ni sisi tupendane

Simple.
Kama matendo yako ni kujifaidisha mwenyewe kwa kuwatia maumivu/hasara wenzio basi huo ndio ushetani. Huhitaji kusaini mkataba wala nn. Mfano mwanasiasa mwizi na mjasiriamali anayepima ki feki na wiziwizi. Umekiuka will ya Mungu

Na ikiwa matendo yako ni kunufaika na kunufaisha wapendwa basi wewe ni wa Mungu machoni pa Mungu na wanadamu. Hauhitaji kusaini wala. Haya mambo ni ya kiroho. Mfano mwanasiasa mzalendo na mjasiriamali anayepima kihalali na orijino. Umeendana na will ya Mungu.
Kwakweli tutawatambua kwa matendo yao
 
Hakuna kitu kinaitwa Freemasons na wala hawatoi mtakuja kupigwa za uso,, hizi ni propaganda kama zingine
 
Miaka ya mwanzo wakati ukristo unaanza kulikuwa na vuguvugu la wayahudi na wakristo. Watu hawa walikuwa wakipinga kuwa kwenye dini zozote. Waliamini mtu anaweza kumuabudu Mungu bila kuwa kwenye dini. Watu hawa walianzia huko Alexandria Misri.

Baada ya dola ya Roma kuanguka, kanisa Katoliki likashika hatamu. Liliua sana watu waliolipinga, likaanzisha vita nyingi na kuhodhi elimu yote. Jambo hili likafanya watu wa vuguvugu hilo la freemason wafanye mambo yao kwa siri. Walipinga kanisa kuhodhi elimu na mambo mengine. Miaka ya 1700 vuguvugu hili likakua sana. Mbali na kupinga kanisa kuhodhi mambo, pia lilianza kupinga na tawala za kifalme. Hotspot ya vuguvugu hizi zilikuwa Ufaransa. Wakitaka ufalme ukome na hata wakitaka dini hizi rasmi zikome(Hasa baada ya kuona jinsi dini rasmi zilivyotenda uovu, kusababisha vita, na kumrudisha nyuma mwanadamu). Hao ndiyo walichochea na mapinduzi ya Ufaransa. Walikuwa wakihubiri Undugu, usawa na uhuru(Liberty). Freemason hawa wa Ufaransa ndiyo waliwapa Marekani zawadi ya mnara wa Libery. Ambao upo New York leo.

Napoleon Bonaparte na freemasons wenzake wengi wa Ufaransa, walifunga safari hadi Alexandria Misri mwishoni mwa miaka ya 1700. Huko lengo ni kujifunza maarifa ya Misri na sehemu ambako Freemasonry ilianza. Huko ndiko alama yao ya pyramid ilitoka.

So freemasons ni watu walioona uovu wa dini na kuukataa. Wanaamini katika uhuru, undugu na usawa. Ni watu poa sana.

Statue of liberty ni zawadi ambao freemason wa Ufaransa waliwapa wale wa US, kusherekea miaka 100 ya uhuru. Chini ni maneno waliyoandika.

View attachment 2236835

View attachment 2236849
Mauaji yote ya kikatili ndani ya kanisa yanaratibiwa na illuminat.

Kuna vyama maalum kama Jesuit ndani ya kanisa wanahusika na kuratibu matukio ya kutisha dhidi ya binadamu

Ushoga ni moja ya agenda ya siri ya hawa watu ikiwa katika mpango mahsusi wa new world order unaoungwa mkono na mamlaka ya kipapa.

Papa aliyejiuzulu na hivi karibuni kufariki,alipinga mpango huo wakati akitakiwa kuu endorse. Aliamua kujiuzulu ili kujivua uhusika katika kutekeleza ushetani wa hawa illuminat.

Hata hivyo kwa kizazi hiki chenye tamaa ya pesa free mason ni kama malaika wa mafanikio kwao

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom