Je, watu waachwe waishi watakavyo?

Je, watu waachwe waishi watakavyo?

Kazanazo

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2023
Posts
7,129
Reaction score
11,372
Kumekuwepo na mmomonyoko mkubwa wa maadili katika jamii zetu miaka hii ya 2000s, japo huko nyuma pia mmomonyoko huu ulikuwepo lakini sio kwa kiwango cha sasa kutokana na kukuwa kwa teknolojia na utandawazi, kila kitu siku hizi hadharani, kamera imekuja kufichua yaliyokuwa yanafichwa na kufanyika kwa siri, sasa hivi hakuna miiko tena mambo ya sirini yanafanywa hadharani bila makatazo yoyote iwe kwa mkubwa au mdogo kila mtu na uhuru wa kujiamulia mambo

Wakati tunakua ukiachilia mbali mila na desturi za makabila mbalimbali, Dini zilitumika katika kukanya na kuwaweka watu katika maadili yaani matendo yaliyo mazuri machoni kwa watu kwa kutumia sheria za kidini ambazo ziliwafanya watu kuwa na hofu na kuogopa kuyaendea au kufanya matendo ambayo hayapendezi machoni kwa watu kama vile wizi, umalaya, ushoga, uvaaji, lugha nk. Dini zilikuwa ndio mbadala wa mila na desturi baada ya kuonekana kupungua kwa ushawishi wa mila za kabila mbalimbali kutokana na kuchanganyika kwa makabila mbalimbali hasa baada ya uhuru

Watu waliishi kistaarabu na kimaadili, mambo ya sirini yalifanyika kwa kificho na ikibainika fulani anafanya kitendo kichafu au kisichopendeza aliadhibiwa kwa kufuata sheria za dini kama muongozo, jamii ilinyooka kiasi kwa kujawa na woga na hofu pia ya adhabu zilizo ahidiwa katika vitabu vya dini

Siku hizi taasisi ya dini nayo inaanza kuishiwa nguvu kwani watu waliowengi hawaamini mambo za Mungu na uumbaji, hii imechangiwa sana na kukua kwa teknolojia na utandawazi, watu hawaamini tena adhabu zilizoahidiwa kwenye vitabu vya dini wala hawawezi kuadhibiana au kukanyana kwa sheria zilizoandikwa kwenye vitabu vya dini kwakuwa hawaviamini

Sheria zinayoaminika kwa sasa ni sheria za ki nchi kwakuwa zinasimamiwa na serikali yenye zana bora kama jeshi, mahakama na magereza hivyo hofu na woga wote ni kwaserikali. Sasa serikali ni watu na wengi wanaongoza kwenye mihimili ya kusimamia mambo ya nchi wengi wao ni either hawana maadili au mfumo unaowaweka hauna au hauzingatii maadili yaani matendo mema yanayopendeza machoni kwa watu

Sheria zinazotungwa na watu wa aina hii zinazingatia maslahi ya kiuchumi zaidi huku mambo mengine ya kimaadili yakiachwa na hata kama yakiwemo kwenye hizo sheria hayafuatiliwi wala kutolewa adhabu pale yanapotendwa. Watu wameachwa waishi watakavyo kwani sheria haiwabani tena kama ilivyokuwa sheria za dini pia kuna mianya mingi yakutokea endapo mmoja akikamatwa au kuhukumiwa ikiwemo rushwa

Swali langu kwa wanajamii, je watu waachwe waishi kama wanyama mwituni? Au nini kifanyike

Karibu katika mjadala
 
Jamii haijawahi kustarabika katika historia ya dunia hii.

Hata hao uliosema sijui dini, hao wenyewe ndio wabaya namba moja , mfano kuna dini moja ilikuja kwa staili ya kuua, kubaka na utumwa na hadi leo waumini wake ndio wanaongoza kulawiti watoto, kuoa watotoo wadogo na kufanya ugaidi na unyama.
 
Maadili muhimu ni kutowatendea wengine mambo mabaya na kutii Sheria za nchi yako husika

Ila the rest waache watu waishi wanavyota don't stress for the things ambazo ni nje ya uwezo wako.

You can't control people , let people live their life . Mind ur own business
 
Kila mtu afate ya kwake nakupunguza shobo kwenye maisha ya watu. Kiufupi usimpangie mtu namna ya kuishi. Japo sheria zipo na ni msumeno.
 
Watu wakiachwa waishi watakavyo watakuwa ni wanyama zaidi ya wanyama, afadhali wanyama wana code zao za kuishi. Ushetani utakuwa mwingi sana kuacha watu waishi watakavyo bila kutungiwa sheria
 
Jamii haijawahi kustarabika katika historia ya dunia hii.

Hata hao uliosema sijui dini, hao wenyewe ndio wabaya namba moja , mfano kuna dini moja ilikuja kwa staili ya kuua, kubaka na utumwa na hadi leo waumini wake ndio wanaongoza kulawiti watoto, kuoa watotoo wadogo na kufanya ugaidi na unyama.
China ukila rushwa wanakunyonga kama moja ya kudumisha maadili ya nchi

Anyways, nini kifanyike tuachwe tuishi tutakavyo? Unahisi hatutafika huko kwenye kuuana pia
 
Maadili muhimu ni kutowatendea wengine mambo mabaya na kutii Sheria za nchi yako husika

Ila the rest waache watu waishi wanavyota don't stress for the things ambazo ni nje ya uwezo wako.

You can't control people , let people live their life . Mind ur own business
Sheria za nchi zina mianya mingi ya kutokea hadi sasa sheria zetu hazina impact yoyote katika kuondoa mmomonyoko wa maadili nini kifanyike
 
Kila mtu afate ya kwake nakupunguza shobo kwenye maisha ya watu. Kiufupi usimpangie mtu namna ya kuishi. Japo sheria zipo na ni msumeno.
Hata kuua, kulawiti na kuiba?

Kila mtu akiachwa afanye anachotaka dunia itakuwa sehemu salama ya kuishi?
 
Watu wakiachwa waishi watakavyo watakuwa ni wanyama zaidi ya wanyama, afadhali wanyama wana code zao za kuishi. Ushetani utakuwa mwingi sana kuacha watu waishi watakavyo bila kutungiwa sheria
Sahihi kabisa, je ni sheria gani ifuatwe ili kuwaweka watu katika mstari wa maadili? Za nchi ni kama zimepwaya
 
Kuachwa waishi watakavyo ni ngumu maana kila sehemu ina sheria zake ishu kwenye kuzifata hizo sheria ndio hapo kunapo tokea mmong'onyoko wa maadi as long as kila familia ibebe jukumu la kulinda maadali yake binafsi
 
Back
Top Bottom