Kulipa kisasi kumenifikisha hapa

Kulipa kisasi kumenifikisha hapa

lailaty88

New Member
Joined
Jun 10, 2015
Posts
2
Reaction score
2
Habari wapendwa,

Poleni na majukumu ya maisha. Wandugu nisiwachoshe mwenzenu kuna mkasa umenipata yaani nashindwa kufanya maamuzi.

Stori inaanza hivi, mimi niliolewa na nikajaaliwa kupata watoto watatu wawili ni twins, mume wangu ni mkristo mimi muislamu.

Sasa wakati mume wangu ananioa nimemkuta na mtoto alizaa na mdada flani hivi muigizaji wa Bongo Movie.

Huyo dada hakumuoa alizaa nae tu wakaachana na mtoto huyo nimemlea mimi mpaka sasa yupo darasa la2.

Mwaka juzi nilipata mkasa mzito sintosahau, nilipakaziwa kitu ambacho sijafanya ikawa ndo sababu na nikaachika kwa talaka kabisa.

Ni kwamba kuna mtu inasemekana alipiga simu kwa wakwe zangu na kujitambulisha kwamba yeye ni rafiki yangu na tupo kwa mganga kwa lengo la kumroga mume wangu nimuue ili nirithi mali zake.

Muda wote huo me skujua kwanini mama mkwe ananichukia ghafla wakati mwanzo alinipenda kama amenizaa.

Mwisho wa siku nikapewa talaka nikarudi kwetu nikiwa na mimba ya mtoto mwingine, nimehangaika peke yangu mpaka nimejifungua.

Nikarudi chuo nimemaliza chuo mume wangu amenifuata kuniomba msamaha turudiane tulee watoto wetu.

Kibinadamu nikamsamehe lakini Mungu hamfichi mnafiki siku ikafika nikagundua aliefanya huo mchezo ni yule mwanamke aliezaa nae lengo lake arudi yeye.

Lakini kisicho riziki hakiliki pamoja na kufanya hayo bado mume wangu hakumrudia.

Akapata bwana mwingne ni askari akazaa nae mtoto mmoja, huyo bwana aliona picha yangu Instagram akanitafuta,yeye hakujua na hajui kama namjua.

So amekua mpenzi wangu kwa muda kidogo, mimi nilikua nafanya kwa kumkomoa yule mwanamke alieniharibia kwangu.

Sasa jamaa huyu ndo amenogewa anataka ndoa nampa tarehe tu kila siku yani nimedata tu hapa.

Nampenda sana na ananipenda hivi keshokutwa anataka kunipeleka kwao Usukumani kunitambulisha.

Mume wangu wa kwanza huyo ni mkristo, huyu ni mkristo but yupo tayari kubadili dini hata leo.

Nampenda ni mstaarabu, muwazi, mkweli, ana huruma, anajua mapenzi tofauti na wa mwanzo.

Sasa nawaza je, akija kujua kama mimi nilikua nalipiza kisasi atanichukuliaje?

Atanipenda? Haya nitamuachaje yule niliezaa nae watoto watatu wakati ameshaomb radhi?

Ushauri please
 
Duuuuh... Hii kali .. Polee sana mkuu,, hebu wasubiri wengine wanakujaaa...
 
Mmmh!!!!!!!! visasi hadi umegewa safi sana, ila jua kama huna mapenzi nae tegemea kujuta baadae.

Raha ya mapenzi ucje jiuliza ilikuwaje nikawa na huyu.

Sema na moyo wako ndio utakupa mwongozo, maana kama uliishaishi na mtu unajua machungu na raha za ndoa ivo jiongoze wewe mwenyewe.
 
Mmmh!!!!!!!! visasi hadi umegewa safi sana, ila jua kama huna mapenzi nae tegemea kujuta baadae.

Raha ya mapenzi ucje jiuliza ilikuwaje nikawa na huyu.

Sema na moyo wako ndio utakupa mwongozo, maana kama uliishaishi na mtu unajua machungu na raha za ndoa ivo jiongoze wewe mwenyewe.

Yeah umenena mkuu.... Afuate moyo wake...
 
Mwanamke wa visasi namuogopa sana anaweza kukuwekea sumu kwenye chakula akakuulia mbali

Unaonekana ni mkatili sana pamoja na mme wako kukuomba samahani bado unaenda kujitongozesha kwa bwana wa adui yako. Kwa jinsi ilivyo ulidhamilia kutenda ujinga huu eti alikuona insta acha hiyo tabia ya visasi.
 
Kuna vitu vingine ni ngumu kuvitolea ushauri!
 
Unalipiza kisasi kwa kutembea na mume wa mtu? huoni kuwa unajiongezea matatzo, siku zote visasi ni vibaya sana kwani wewe mwenye kulipiza unajiweka kwenye shida na matatizo.

Jifunze kusamehe dada.
 
Jibu unalo mwenyew, maana hamna mtu hp anaeona moyo wako..
 
Visasi sio vizuri tulia na mmeo mlee watoto wenu acha kuwatangisha watoto maisha ni kuvumilia shida na raha ndio binadam tumeumbwa hivyo,anza kukata mawasiliano na huyo jamaa mwisho utamwacha kabisa na mwombe sana mola wako maisha hubadilika hujui leo wala kesho itakuwaje?
 
Pole sana mkuu, ila kumbuka visasi huwa analipa mwenyezi mungu.....mrudie mume wako achana na huyo mchepuko.
 
una pepo la kisasi Umalaya....kapime VVU alafu utuletee mrejesho ndio tuendelee kukushauri....
 
Niccolò Machiavelli said some like, if an injury is to be caused to a man, it must be so severe that revenge need not be feared. In this case una baba wa watoto wako na ex wake, wote umewashadhuru, and chances are..wakigundua watataka kulipa kisasi na wao. Tayari una watoto watatu na aliyekuwa mumeo, na ulishamsamehe, kwanini msiendelee mlipoishia kama familia?

Besides, the fact uko hapa kuomba ushauri na unasita kuingia kwenye hiyo ndoa na bwana askari ni sababu tosha usiingie.
 
visasi sio vizuri tulia na mmeo mlee watoto wenu acha kuwatangisha watoto maisha ni kuvumilia shida na raha ndio binadam tumeumbwa hivyo,anza kukata mawasiliano na huyo jamaa mwisho utamwacha kabisa na mwombe sana mola wako maisha hubadilika hujui leo wala kesho itakuwaje?
mkuu kula like5 kwanza........huu ndio ushauri mzuri.
 
"Wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu
ya Mungu; maana imeandikwa, kisasi ni juu yangu
Mimi, Mimi nitalipa, anena Bwana" (Warumi 12:19)

Umeona mungu hawezi kukusaidia umeamua uchukue madaraka mkononi
 
Back
Top Bottom