Mi mtazamo wangu ni kwamba vijana hawa hawajaandaliwa mazingira ya ustaarabu kwa hiyo hawawezi kuwa wastaarabu kamwe. Mojawapo ya huduma za jamii ambazo serikali yetu imezipuuzia ni pamoja na maliwato, ambayo mi nilipokuwa naanza kupata akili miaka ya 80 mwanzoni kulikuwa na vyoo vya serikali karibia kila mahali ambavyo watu walivitumia bila malipo na vilikuwa na huduma zote za msingi km maji na sabuni. Leo hii, vile vyoo vyote vya serikali vimebinafsishwa, na wawekezaji hao wameachiwa uhuru wa kutoza kiwango cha pesa watakazo, cjawahi kusikia EWURA wakidhibiti bei ya kujisaidia kwny maliwato ya umma! Tutafakari! :A S thumbs_down: