Kukazia hukumu maana yake nini?

Focus120

JF-Expert Member
Nov 10, 2014
1,090
786
Hellow Learned brothers and sisters. Naomba mnifahamishe maana ya kukazia hukumu kisheria , nimekuwa nikilisikia hili neno Mara kwa mara lakini sijui maana yake.



Katika kesi za madai (tofautisha na kesi za jinai) mahakama huwasikiliza wadaawa (wenye kesi) na baada ya kuwasikiliza hutoa hukumu kulingana na ushaidi.

Aliyeshinda kesi hupata kitu kinaitwa DECREE. Kwa hiyo yeye nakuwa DECREE HOLDER, aliyeshindwa anakuwa JUDGMENT DEBTOR (utanishamehe sababu maneno haya siyafahamu katika lugha ya kiswahili. DECREE HOLDER ataluhusiwa kufungua shauli jingine la kukaza hukumu katika mahakama (Applicatin for Execution of Decree).

Kisheria hii hatua inatakiwa ifanyika mda wowote ule lakini usizidi miaka 12. Mahakama itamuita JUDGMENT DEBTOR ili ajieleze kwa nini amri za kwenye hukumu (ambazo zinakuwa zimeainishwa kwenye DECREE) zisitekelezwe.

Mahakama ikilizika kwamba hakuna Rufaa iliyokatwa kupinga hukumu basi mahakama itaamuru hukumu itekelezwe (kukaza hukumu). hapa sasa mdaiwa (JUDGEMENG DEBTOR) atazimishwa kulipa deni analodaiwa au kuondoka sehemu asiyotakiwa kuwepo.

Hapa sasa mahakama inaweza kuteua madalali au wafilisi ili kumlazimisha JUDGMENT DEBTOR atekeleze amri za mahakama. Hii ndio inaitwa kukaza hukumu.
 
ukipata kesi ya madai utajua tu. kwa kifupi ni kutekeleza amri za mahakama baada ya hukumu
 
Unaweza kuongeza nyama kwenye hii habari Mkuu?

Katika kesi za madai (tofautisha na kesi za jinai) mahakama huwasikiliza wadaawa (wenye kesi) na baada ya kuwasikiliza hutoa hukumu kulingana na ushaidi.

Aliyeshinda kesi hupata kitu kinaitwa DECREE. Kwa hiyo yeye nakuwa DECREE HOLDER, aliyeshindwa anakuwa JUDGMENT DEBTOR (utanishamehe sababu maneno haya siyafahamu katika lugha ya kiswahili. DECREE HOLDER ataluhusiwa kufungua shauli jingine la kukaza hukumu katika mahakama (Applicatin for Execution of Decree).

Kisheria hii hatua inatakiwa ifanyika mda wowote ule lakini usizidi miaka 12. Mahakama itamuita JUDGMENT DEBTOR ili ajieleze kwa nini amri za kwenye hukumu (ambazo zinakuwa zimeainishwa kwenye DECREE) zisitekelezwe.

Mahakama ikilizika kwamba hakuna Rufaa iliyokatwa kupinga hukumu basi mahakama itaamuru hukumu itekelezwe (kukaza hukumu). hapa sasa mdaiwa (JUDGEMENG DEBTOR) atazimishwa kulipa deni analodaiwa au kuondoka sehemu asiyotakiwa kuwepo.

Hapa sasa mahakama inaweza kuteua madalali au wafilisi ili kumlazimisha JUDGMENT DEBTOR atekeleze amri za mahakama. Hii ndio inaitwa kukaza hukumu.
 
mahakama inapo fika mwisho inapotoa hukumu hua inaeleza tu nani kashinda katika kesi ile na kama ameshinda ni haki zipi anastahili kuzipata kulinga na kesi husika, pia hutoa decree(amri), hii inaweza kumtaka aliyeshindwa kulipa chochote kwa mdai kulingana na madai. baada ya kusoma hukumu mdai atasubiri muda furani ili mdaiwa atekeleze maamuzi ya mahakama. asipo tekeleza ndipo huleta maombi ya kukaza hukumu( kutekeleza amri ya mahakama kama ilivyo semwa ktk hukumu) pia mdai anaweza kupendekeza jinsi madai yake yanavyo weza kulipwa.Hivyo kama hakuna sababu yoyote ya mdai kuto timiza amri ya mahakama, huamua kutumia uwezo waake kutimiza amri iliyotoa. hii ni pamoja na kupiga mnada na nyingine nyingi. hivyo kukaza hukumu ni kuiomba mahakama itumie nguvu yake kumfanya aliyeshindwa katika hukumu kutekeleza amri ya mahakama, baada ya yeye kushindwa kutimiza hilo.
 
Nakushukuru mkuu inaonkena hii ni fani yako mtu akitaka huduma yako unapatikanaje?
 
mahakama inapo fika mwisho inapotoa hukumu hua inaeleza tu nani kashinda katika kesi ile na kama ameshinda ni haki zipi anastahili kuzipata kulinga na kesi husika, pia hutoa decree(amri), hii inaweza kumtaka aliyeshindwa kulipa chochote kwa mdai kulingana na madai. baada ya kusoma hukumu mdai atasubiri muda furani ili mdaiwa atekeleze maamuzi ya mahakama. asipo tekeleza ndipo huleta maombi ya kukaza hukumu( kutekeleza amri ya mahakama kama ilivyo semwa ktk hukumu) pia mdai anaweza kupendekeza jinsi madai yake yanavyo weza kulipwa.Hivyo kama hakuna sababu yoyote ya mdai kuto timiza amri ya mahakama, huamua kutumia uwezo waake kutimiza amri iliyotoa. hii ni pamoja na kupiga mnada na nyingine nyingi. hivyo kukaza hukumu ni kuiomba mahakama itumie nguvu yake kumfanya aliyeshindwa katika hukumu kutekeleza amri ya mahakama, baada ya yeye kushindwa kutimiza hilo.

mkuu nakutafuta nimekutumia na PM.
 
safi, kwa kuongeza ni kwamba si kazi ya mahakama kuandaa decree bali ni yule aliyeshinda kesi ndy anayeandaa na kupeleka kwa hakimu au judge kwa ajili ya kusaini na kugonga mhuri. Ieleweke kuwa watu wamekuwa wakishinda kesi halafu wananyamaza kimya wakingojea mahakama itekeleze hukumu, hiyo si sawa. Tatu, maombi ya kukazia hukumu yaweza kuombwa ktk mahakama yoyote yenye mamlaka kulingana na hukumu hiyo na sababu kubwa ni kwamba wakati mwingine shauri laweza kuwa lilikuwa linahusu mali isiyohamishika kama vile nyumba, shamba nk. sheria inataka mahakama itakayokuwa na mmlaka ya kutekeleza hukumu ni ile ambayo mali hiyo ipo. mfano. mshitakiwa anaishi dar lakini shitaka lake linahusu nyumba iliyoko mbeya na kwakuwa sheria inata mtu ashitakiwe anakoishi au ambako mali ipo, ikitokea mlalamikaji ameamua kumshitaki mshitakiwa katika mahama ya dar anakoishi mshtakiwa basi mahakama itakayo toa amri ya kutekeleza hukumu ni ile ya mbeya lakini kama ingekuwa si shitaka linalohusu mali yakutohamishika basi mahakama ya dar ingeweza kutekeleza hukumu hiyo. IKIWA KUNA SWALI LINAHUSU SHERIA NIULIZE NITAKUWA TAYARI KUJIBU KAMA LIPO NDANI YA UWEZO NALO
 
Cha kuongezea ni kwamba, lazima ieleweke hapo kuwa kuna maombi mawili yanayotolewa ili kufanikisha kukaza huku. Ombi lakwanza ni LA kukamata Mali zinazokamatika kisheria, Mali zikikamatwa mdaiwa anaweza kuamua kulipa deni ili Mali zake ziachwe, km mda Fulani hope 15 days zikipita, mdai ana nafas nyingine ya kuomba Mali iliyokamatwa iuzwe, nayo pia Ina mda wake namatangazo yatatolewa, baada ya hapo amri yakuuza itatekelezwa.
Thnx
 
safi, kwa kuongeza ni kwamba si kazi ya mahakama kuandaa decree bali ni yule aliyeshinda kesi ndy anayeandaa na kupeleka kwa hakimu au judge kwa ajili ya kusaini na kugonga mhuri. Ieleweke kuwa watu wamekuwa wakishinda kesi halafu wananyamaza kimya wakingojea mahakama itekeleze hukumu, hiyo si sawa. Tatu, maombi ya kukazia hukumu yaweza kuombwa ktk mahakama yoyote yenye mamlaka kulingana na hukumu hiyo na sababu kubwa ni kwamba wakati mwingine shauri laweza kuwa lilikuwa linahusu mali isiyohamishika kama vile nyumba, shamba nk. sheria inataka mahakama itakayokuwa na mmlaka ya kutekeleza hukumu ni ile ambayo mali hiyo ipo. mfano. mshitakiwa anaishi dar lakini shitaka lake linahusu nyumba iliyoko mbeya na kwakuwa sheria inata mtu ashitakiwe anakoishi au ambako mali ipo, ikitokea mlalamikaji ameamua kumshitaki mshitakiwa katika mahama ya dar anakoishi mshtakiwa basi mahakama itakayo toa amri ya kutekeleza hukumu ni ile ya mbeya lakini kama ingekuwa si shitaka linalohusu mali yakutohamishika basi mahakama ya dar ingeweza kutekeleza hukumu hiyo. IKIWA KUNA SWALI LINAHUSU SHERIA NIULIZE NITAKUWA TAYARI KUJIBU KAMA LIPO NDANI YA UWEZO NALO
Kama mtu alikuwa na kesi ya jinai akahukumiwa kifungo cha nje na kutakiwa kulipa, kuna haja kwa mlalamikaji kuandika barua ya kuomba kukazia hukumu kwa ajili ya utendaji zaidi? Au kukazia hukumu inahusika kwenye civil case pekee? msaada tafadhari. na kama kukazia hukumu haihusiki kwenye kesi za jinai ni kipi kifanyike kama mshitakiwa kamaliza muda wa kifungo na hajalipa?
 
safi, kwa kuongeza ni kwamba si kazi ya mahakama kuandaa decree bali ni yule aliyeshinda kesi ndy anayeandaa na kupeleka kwa hakimu au judge kwa ajili ya kusaini na kugonga mhuri. Ieleweke kuwa watu wamekuwa wakishinda kesi halafu wananyamaza kimya wakingojea mahakama itekeleze hukumu, hiyo si sawa. Tatu, maombi ya kukazia hukumu yaweza kuombwa ktk mahakama yoyote yenye mamlaka kulingana na hukumu hiyo na sababu kubwa ni kwamba wakati mwingine shauri laweza kuwa lilikuwa linahusu mali isiyohamishika kama vile nyumba, shamba nk. sheria inataka mahakama itakayokuwa na mmlaka ya kutekeleza hukumu ni ile ambayo mali hiyo ipo. mfano. mshitakiwa anaishi dar lakini shitaka lake linahusu nyumba iliyoko mbeya na kwakuwa sheria inata mtu ashitakiwe anakoishi au ambako mali ipo, ikitokea mlalamikaji ameamua kumshitaki mshitakiwa katika mahama ya dar anakoishi mshtakiwa basi mahakama itakayo toa amri ya kutekeleza hukumu ni ile ya mbeya lakini kama ingekuwa si shitaka linalohusu mali yakutohamishika basi mahakama ya dar ingeweza kutekeleza hukumu hiyo. IKIWA KUNA SWALI LINAHUSU SHERIA NIULIZE NITAKUWA TAYARI KUJIBU KAMA LIPO NDANI YA UWEZO NALO
Hapana hapana mkuu, badala ya kuongeza UMEPOTOSHA watu bora ungelike basi.

Hata mfano wako co vivid (km mali isiyohamishika ipo mbeya kisheria kesi itasikilizwa huko mbeya na sio Dar). Km bado upo chuo PROCEDURAL LAW ni changamoto subiri uje uraiani komaa tu na SUBSTATIVE LAW!.
 
Cha kuongezea ni kwamba, lazima ieleweke hapo kuwa kuna maombi mawili yanayotolewa ili kufanikisha kukaza huku. Ombi lakwanza ni LA kukamata Mali zinazokamatika kisheria, Mali zikikamatwa mdaiwa anaweza kuamua kulipa deni ili Mali zake ziachwe, km mda Fulani hope 15 days zikipita, mdai ana nafas nyingine ya kuomba Mali iliyokamatwa iuzwe, nayo pia Ina mda wake namatangazo yatatolewa, baada ya hapo amri yakuuza itatekelezwa.
Thnx
Umepotosha badala ya kuongezea!.
 
Je, kama kesi ni ya jinai mtu akahukumiwa kifungo cha nje na kulipa, mlalamikaji anatakiwa kukazia hukumu ili kulipwa endapo mlalamikiwa hajalipa ndani ya muda aliopewa na mahakama? Msaada tafadhari.
 
Je, kama kesi ni ya jinai mtu akahukumiwa kifungo cha nje na kulipa, mlalamikaji anatakiwa kukazia hukumu ili kulipwa endapo mlalamikiwa hajalipa ndani ya muda aliopewa na mahakama? Msaada tafadhari.
Jieleze vizuri upate msaada Mkuu.

Maelezo yako hayako wazi.
 
Mwishoni mwa mwaka jana kuna mtu tulikuwa tumesainiana mkataba ambapo nilimkabidhi pikipiki ili awe anarejesha kiwango fulani cha hela kila wiki. Baada ya wiki zisizozidi tano huyo jamaa akasitisha marejesho na hakunipa taarifa yoyote, kila nilipokuwa napiga simu yake ya kiganjani muda mwingi alikuwa hapokei na muda mwingine hapatikani.
Nilihamua kumfuata nyumbani kwake cha kusikitisha nilimkuta amelala bila jeraha lolote mwilini lakini akaniambia kuwa amepata ajali na pikipiki iko kwa fundi, nilipomuomba anipeleke niione pikipiki hiyo alikoiweka kwa fundi alijitahidi kunikwepa. Sikuwa tayari kuendelea kuumiza kichwa changu nikaamua kumpeleka mahakamani kwa kesi ya jinai ya kujipatia mali kwa njia za udanganyifu. Mahakama ilimtia hatiani akahukumiwa kifungo cha nje miezi sita na kulipa shilingi milioni mbili (gharama ya pikipiki) mara tu baada ya miezi mitatu ya awali katika kifungo hicho. Sasa huu ni mwezi wa tano jamaa hajaleta hela yoyote. Ndo hapa nauliza kesi hii ya jinai natakiwa kuandika barua ya kukazia hukumu pia?
 
Back
Top Bottom