SWALI 1: Kodi nitakayotakiwa kulipa kama nimetumia DHL au njia nyingine tofauti na posta ni asilimia ngapi?
Kodi hukokotolewa kutokana na Declared item value/ Assesses value
- Declared value - Hii hutoka kwa muuzaji wa bidhaa, huonyesha kiasi ulichonunulia
- Assessed Value - Hii hutokana na Maafisa wa ushuru wa forodha baada ya kukagua mzigo.
(a) Iwapo atakubaliana na declared value, basi assessed value itakuwa ni hiyo hiyo ambayo iko kwenye invoice ilikuja na mzigo, KODI itakokotolewa kutegemea hiyo declared value
(b) Iwapo afisa ushuru wa forodha atakataa declared value, basi KODI itakokotolewa kutokana na thamani ya mzigo AUNAVYO YEYE, Assessed Value, hutumika hili neno "
UPLIFT" - Yaani mfano declared value kwenye invoice ni dola 100, na wewe umelipia dola 100; Wakifanya uplift utaambiwa thamani ya mzigo wako, assesses valu, mfano ni dola 300 - Hivyo ukokotozi wa KODI utatokana na assessed value, Japokuwa wewe ulilipia dola 100 kwa bidhaa yako.
Hiki kipengele B ndicho huwaliza wengi.
MALIPO UTAKAYOLIPA (TOTAL TAXES)
- IMP - Import Duty ( 25% ya
A )
- EX - Excise Duty ( _% )
- RDL - Railway Development levy ( 1.5% ya
A )
- CPF - Customs processing fee ( 0.6% ya
A )
- VAT - Value Added Tax ( 18% ya
C)
EX, RDL na CPF - huwa ni kiasi kidogo fedha shida iko kwenye IMP & VAT
IMPORT DUTY Vs VAT
Mfano
A = Bei ya kitu pamoja na ghalama ya kusafirishia.
A X
25%= B ( kiasi utakachotozwa kama IMP )
A + B + (EX + CPF + RDL) =
C (itatafutwa asilimia 18 yake)
C X
18% = G ( Ni kiasi cha VAT utakachotozwa )
TUANGALIE MFANO_1 WA BIDHAA NILIYONUNUA KWA DOLA 20 (SAWA NA TSH 43,819.60 KWA RATE YA 1USD=2,190.92TSH kwa Tarehe 05.03.2016)
Jinsi walivyo kokotoa KODI.
MFANO_2 THAMANI YA BIDHAA KWA TSH NI 255,135.00
NB: Ukiangalia vyema picha ya kwanza ina EX (Excise Duty), ila ya pili Haina. Hivyo kodi kwa sasa hutegemea IMP + RDL + CPF + VAT
SWALI 2. Je kodi hii nalipia bandarini au pale nitakapopata mzigo wangu?
- Malipo yote hufanyika kabla ya kupewa mzigo.
- Kama
kiasi cha kodi ni kidogo utalipa kupitia agents anayekuletea mzigo ofisini kwako au nyumbani - Hii hasa ni kwa DHL
- Kama malipo ya KODI ni kiasi kikubwa utapewa utaratibu wa malipo.
- Kuna njia zaidi ya moja ya kufanya malipo, waweza tumia menu ya MPESA, Maxmalipo, au Bank utapewa maelekezo na wahusika.
SWALI 3. Nasikia hawa jamaa wa posta
ni wezi sana wa mizigo kuna ukweli wowote hapo?maana naona wewe Kindle paperwhite yako uliipata salama.
- Mizigo yangu yote iliyokuja kwa njia ya Post ilifika salama. Sijawahi kupoteza mzigo.
- Hilo swala la wizi watu husema, ila kwa mimi haijwahi kunitokea
-
Kindle paperwhite yako uliipata salama? Ndio ilikuwa salama.
Nashukuru kwa maelezo yako mkuu, nina maswali matatu ya mwisho
1. Kodi nitakayotakiwa kulipa kama nimetumia DHL au njia nyingine tofauti na posta ni asilimia ngapi?
2. Je kodi hii nalipia bandarini au pale nitakapopata mzigo wangu?
3. Nasikia hawa jamaa wa posta ni wezi sana wa mizigo kuna ukweli wowote hapo?maana naona wewe Kindle paperwhite yako uliipata salama.