Sasa unachoshangilia nini? Hamuwezi kushinda bila kuwabana wenzenu?Ha ha ha ama kweli CHADEMA ni wageni wa siasa za CCM ,yaani matangazo yamekatwa kidogo mnapiga makelele ,sizani kama mtaiweza mizengwe na mikakati ya Chama Tawala ? Mambo ndio kwanza ata CCM awajafungulia majibwa yao !!:lol:
Mpambalyoto kuna uwezekano wa kuondoa hilo panga kwenye Avatar yako? linaogopesha kukujibu si unajuwa sisi ni watu wa amani TZ.
Hata wakati Tido anaongea jana usiku, ukiangalia uso wake kwa makini unaona kabisa alikua anajisikia aibu kwa anayoyasema...hivi Tido,heshima yote uliyojijengea ukiwa TBC, ndo unaishusha kwa kasi hivi?? Unajua ni vijana wangapi umewa-inspire wawe watangazaji kutokana na influence yako ya zamani?? Unadhani hapo TBC utakaa milele?? Unanisikitisha sana siku hizi, ulivyotoka BBC kwa jinsi tulivyokuheshimu, mojawapo ya maoni ya wadau ilikua ni pamoja na kukupa udaktari wa heshima katika fani ya habari, lakini kwa haya yanayoendelea chini yako, sijui unawaandalia future ya aina gani Evans na ndugu zake hapo TBC,kumbuka miaka inaenda....
ililkuwa kama zile sinema za akina rambo na waigizaji wengine,tbc kwa kile cha kulinda maslahi ya wakubwa wakaamua kukatiisha kurusha matangazo kwa sababu mabere marando alikuwa akifichua ufisadi wa kikwete,watu walishindwa kuzuia hasira zao na kuanza hata kmtupia makopo ya maji mtangazaji na kada wa chama marini hassan marini ambaye aliokolewa na vyombo vya usalama,
tbc eleweni kuwa watanzania si mabwege tena
Hebu ngoja niweke hivi; uhuru wa maoni ni pamoja na uhuru wa maoni ya kijinga. Uhuru wa maoni si lazima yawe maoni tunayoyataka sisi au tunayojisikia ni ya kutufurahisha. Uhuru wa maoni haupo ati kwa sababu lugha ni ya kistaarabu kwa hiyo ikitumika lugha isiyo ya kistaarabu basi kuna polisi (Tido) na wenzake ambao wanaamua kusema "hatutatiki kukusikiliza". Endapo mtu anasema kitu ambacho kinavuka uhuru huo yule anayesemwa anatakiwa kwenda mahakamani. TBC siyo msimamizi wa maoni hayo.
Lakini jingine ni kuwa madongo yaliyorushwa na JK na wenzake Jangwani dhidi ya wapinzani yalikuwa ni ya kistaarabu? Au ni ustaaarabu kuelekea CCM na siyo kwingine?
Lakini kubwa zaidi ni kuwa Watanznaia ni watu wazima na wana uwezo wa kusikiliza, kuamua na kukataa hoja za kijinga au kipuuzi. Hawahitaji serikali ikae kama nanny kuamua kusema "hili watanzania hawastahili kulisikia". Hakuna chochote ambacho kimetamkwa jangwani ambacho hakijawahi kluandikwa au kuzungumzwa na vyombo vya habari.
Jamani, kama demokrasia imewashinda wajaribu udikteta!
Nimesikiliza mkuu
Na hapa ndipo anadhihirisha kuwa na akili sawa na ya kuku.Kwa akili na tafsiri ya TIDO na TBC1 mtu mstarabu ni yule anayeisifia CCM pamoja wa JK na kuwaponda wengine