Elections 2010 Kukatishwa Kwa Matangazo Jangwani: Tido Mhando Alonga

Ha ha ha ama kweli CHADEMA ni wageni wa siasa za CCM ,yaani matangazo yamekatwa kidogo mnapiga makelele ,sizani kama mtaiweza mizengwe na mikakati ya Chama Tawala ? Mambo ndio kwanza ata CCM awajafungulia majibwa yao !!:lol:
Sasa unachoshangilia nini? Hamuwezi kushinda bila kuwabana wenzenu?
 
Mara ya kwanza Johnson Mbwambo alimchambua udhaifu wake wa kumuuliza kikwete maswali ya kishkaji nikadhani ana,wonea, sasa nimeanza kuona udhaifu wake laivu. Ni matusi yapi aliyotamka marando? alichofanya marando ni kutukumbusha tu ambayo tunayafahamu.

Huyu bwana huwezi kuamini kama ni mtu ambaye amefanya kazi BBC alikuwa akijionea mwenyewe jinsi David Cameron na Godon brown walivyokuwa wakichambuana , hakuna anayemsifia mwingine eti "kampeni ya kistaarabu" Kusema ukweli ndo kutokuwa mstaarabu?
 
Najua CCM Wasingependa neno Ufisadi likitamkwa hasa na wapinzania...Nilisikia Marando akizungumzia EPA sijui aliongelea na nini kingine maana TBC walifanya kazi yao..au Meremeta, Richmond ....
 
Hata wakati Tido anaongea jana usiku, ukiangalia uso wake kwa makini unaona kabisa alikua anajisikia aibu kwa anayoyasema...hivi Tido,heshima yote uliyojijengea ukiwa TBC, ndo unaishusha kwa kasi hivi?? Unajua ni vijana wangapi umewa-inspire wawe watangazaji kutokana na influence yako ya zamani?? Unadhani hapo TBC utakaa milele?? Unanisikitisha sana siku hizi, ulivyotoka BBC kwa jinsi tulivyokuheshimu, mojawapo ya maoni ya wadau ilikua ni pamoja na kukupa udaktari wa heshima katika fani ya habari, lakini kwa haya yanayoendelea chini yako, sijui unawaandalia future ya aina gani Evans na ndugu zake hapo TBC,kumbuka miaka inaenda....

Tido Dunstan Mhando umjuaye wewe na mimi miaka ile kabla haja ondoka Tanzania kwenda Sauti ya Kenya Nairobi na hatimaye kujijengea jina kubwa kwenye anga za Kimataifa na kuwa mpaka Mkuu wa idhaa ya BBC siyo yeye yule wa leo. Tido Dunstan Mhando wa leo amelewa togwa la kifisisadi, kwani anazungumza kama wao na na anafanya kila kitu kama wao. Tido Dunstan Mhando wa leo amekubali kuwa kibaraka wa siasa kandamizi. Tido Dunstan Mhando wa leo ameamua kuisaliti taaluma. Sasa amekuwa kundi moja na mafisadi wengine waliokwisha jivunjia heshima za taaluma zao kama akina Salva Rweyemamu na wapuuzi wengine on the list.
 
Wana jamii kwani hamjui kuwa ni Jakaya Kikwete ndiye aliyempa kazi TIDO??? Jakaya amemsaidia TIDO kutoka kuishi ughaibuni UK, kwa hiyo ni lazima atii amri ya BOSS wake, tena siyo BOSS tu ni kuwa kamsaidia kampa kazi.
Naamini kuwa TIDO alipigiwa simu au aliamurishwaa na CCM azime TV haraka sanaaaaaaa, of course TIDO kama TIDO angetaka na angependa sana watanzania wajuwe jinsi CCM wanavyoibaaaaaa mahela yao, na mambo ya KISHENZI wanayofanya CCM, TIDO angetaka watanzania wafahamu, lakini hao majambazi wanaogopaa sana.
Watanzania wasikatishwe tamaa na ujinga na michezo ya kuigiza inayofanywa na CCM, iko siku kitaeleweka tuuu, kama siyo kwa KURA basi kwa BUNDUKI, maana CCM wameigeuza hii nchi ya kwao wanafanya wanachokitaka.
Mapambano yanaendelea mpaka kieleweke!!!
 
ililkuwa kama zile sinema za akina rambo na waigizaji wengine,tbc kwa kile cha kulinda maslahi ya wakubwa wakaamua kukatiisha kurusha matangazo kwa sababu mabere marando alikuwa akifichua ufisadi wa kikwete,watu walishindwa kuzuia hasira zao na kuanza hata kmtupia makopo ya maji mtangazaji na kada wa chama marini hassan marini ambaye aliokolewa na vyombo vya usalama,
tbc eleweni kuwa watanzania si mabwege tena

Nasikitika sikuwepo make ninge samasoti nikamramba teke, make kodi yangu ndo inaendesha TBC, iweje iwe ya watu fulani?
 
Kama mambo yenyewe ndo haya basi haina hata maana ya kwenda kupiga kura kwa sababu zitaibiwa tu na ntakuwa nimepoteza kura yangu.Vyombo vyote na tume zinaonekana zipo upande wa CCM.
 
Hebu ngoja niweke hivi; uhuru wa maoni ni pamoja na uhuru wa maoni ya kijinga. Uhuru wa maoni si lazima yawe maoni tunayoyataka sisi au tunayojisikia ni ya kutufurahisha. Uhuru wa maoni haupo ati kwa sababu lugha ni ya kistaarabu kwa hiyo ikitumika lugha isiyo ya kistaarabu basi kuna polisi (Tido) na wenzake ambao wanaamua kusema "hatutatiki kukusikiliza". Endapo mtu anasema kitu ambacho kinavuka uhuru huo yule anayesemwa anatakiwa kwenda mahakamani. TBC siyo msimamizi wa maoni hayo.

Lakini jingine ni kuwa madongo yaliyorushwa na JK na wenzake Jangwani dhidi ya wapinzani yalikuwa ni ya kistaarabu? Au ni ustaaarabu kuelekea CCM na siyo kwingine?

Lakini kubwa zaidi ni kuwa Watanznaia ni watu wazima na wana uwezo wa kusikiliza, kuamua na kukataa hoja za kijinga au kipuuzi. Hawahitaji serikali ikae kama nanny kuamua kusema "hili watanzania hawastahili kulisikia". Hakuna chochote ambacho kimetamkwa jangwani ambacho hakijawahi kluandikwa au kuzungumzwa na vyombo vya habari.

Jamani, kama demokrasia imewashinda wajaribu udikteta!

Mkuu sana MMMJ,
JK aliwaita wapinzani kuwa ni FOTOKOPI na CCM ndio ORIJINO....Hili sio tusi?....na Mungu akamlaani kwa kutukana huku kafunga....Pwa akaanguka.....AISEE
 
Kwa akili na tafsiri ya TIDO na TBC1 mtu mstarabu ni yule anayeisifia CCM pamoja wa JK na kuwaponda wengine
 
Kilicho muharibia Tido Muhando ni kutumiliwa na CCM. Na unapotumiliwa mara zote huwa huna mwisho mwema. Ni kheri angebakia kule kule BBC ambako alikuwa tayari amesha jijengea. Alianza na kuziba harakati za CUF na 2005 na alidiriki hata kumuondosha Ally Saleh kutooka Zanzibr na kumleta Dar, kituu ambacho ni kinyume nyume kabisa. Ally Saleh amekuwa na BBC kwa muda mrefu na mtu ambaye anaeleweka zaidi Zanzibar na ni muandhishi pekee ambaye hana woga katika kazi yake. Sasa kumuondosha kwa siku za uchaguzi hapo kunatia mashaka!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom