Kukaa na mashemeji

Kukaa na mashemeji

Mbege

Member
Joined
Oct 27, 2013
Posts
61
Reaction score
32
Wana JF, ushauri unahitajika. Nimeoa kwa muda wa miaka 7 sasa mke wangu ni kutoka kanda ya ziwa, kwamuda wote huo sikuwahi kukaa na ndugu wa mke wangu hata mmoja zaidi ya mimi kuwatembelea wao kuko kwao na kurudi. Hivi karibuni amekuja mdogo wa mke wangu mwanaume yeye hajaoa na hana kazi.

Ni muda wa miezi mitatu sasa yuko kwangu na nilitegemea kuja kwake ni kwa muda tu kusalimia na kuondoka. Hivi sasa nimekuwa nikikwazika sana hasa baada ya kuzoea hapa nyumbani kwangu, kwanza nirudipo nyumbani namkuta yuko jikoni na dada yake wanapiga stori muda wote hata siku nikiwa sijaenda kwenye misele kutwa ni yeye na dada yake tu.

Pili mke wangu amekuwa akifanya mambo mengi naye bila kunishirikisha kabisa mfano, amemtafutia kibarua mahali bila mimi kujua, na shemeji mwenyewe hayawahi kuniambia, tatu anaweza akaondoka kwenda kwa jamaa zake wengine wa kutoka kwao waliopo mji ninaoishi na kulala huko bila hata ya kuniaga mimi ni dada yake tu. Nne amekuwa akitoa amri hata kwa watoto wangu na dada wa kazi kwa kuwakoromea.

Mke wangu kwa sasa hana mda na mimi kabisa ni yeye na mdogo wake tu, hata chakula anaweza akapewa yeye kabla hata ya watoto na hata mimi pia. Jamani hiii imekaaje, au ni mimi mwenye tatizo? Ninampango wa kumwambia huyu shemeji aende zake alikotoka.

Semeni waungwana
 
Ongea na mkeo. Baba wa nyumba kulalamika sio vizuri. Ni kumkosea Mungu aliyekufanya kichwa.
Nilishaongea nae mara kibao ila nikizungumzia swala hili la nduguye huanza kulia na kununa ndio mana nawashirikisha weeeeee
 
Ongea na mkeo. Baba wa nyumba kulalamika sio vizuri. Ni kumkosea Mungu aliyekufanya kichwa.

Naunga mkono 100% hoja hii,hili ni jambo dogo sana pia halihitaji hata ushauri wa jf.

Unaonekana wazi ni mkongwe kwenye ndoa sasa ni vzr ukakaa na Mkeo mkaongea na mambo yakawa kama zamani vile.
 
Kuishi ma ndugu kazi sana mtafutie kazi mji mwingine aondoke hapo au kama dada yake hataki basi waache wote wakajitegemee
 
Yaani ww ..

1. Hukustagili kuoa ,.inaonyesha hukuwa tayari kuoa ,umekutupuka .

2. Mwanaume kamili tena anayesema ana mkr na watoto ,maswala ya kifamilia kama Baba wa nyumba ilikupasa kuyamaliza mwnyewe,hususani swala dogo kama hilo . Ww ndio kichwa .

3. Kuomba ushauri wa kifamilia kwenye Mitandao ya kijamii ni kuiabisha Familia yako ,zaidi ni huyo unayemuita mkeo. Kama swala lilikua kubwa na una uhakika ulifuata taratibu zote za ndoa basi kilichokupasa ni kuchukua hatua za kunuonana na mshauri wako wa ndoa ,na sio kuja kuanika mambo ya familia yako huku .

4. Hujui wajibu wako kwenye ndoa mpaka sasa ,mke kakukalia kooni.

5. Na mwisho ,acha kuiaibisha familia ,zaidi mkeo.
 
Kuna makabila mgeni kukaa miezi 6 ni jambo la kawaida. Mtafutie shuhuli ya kufanya akikataa nawe uvae uso wa kazi. Epuka watu jamii ya mbu. Piga baygon.
 
Ongea nae, halafu punguza wivu mkuu. Mimi mwenyewe nampenda mdogo wangu wa mwisho kupita maelezo, yani ts like namuonea huruma hajafaidi mapenzi ya baba, Mzee amefariki amemuacha mdogo sana, so najitahidi kuziba hilo pengo. Kila mtu anajua kuwa dogo anachukua nafasi ya kwanza moyoni mwangu, hata mchumba wangu anajua hilo. He comes first in everything I do.
So ongea na mke wako ili ujue whats going on in her mind, mdadisi historia yao, makuzi yao n.k.
 
Nilishaongea nae mara kibao ila nikizungumzia swala hili la nduguye huanza kulia na kununa ndio mana nawashirikisha weeeeee

Huyo huenda ana yake ya ziada sasa analia bila nae kusema yale unayomuuliza ikiwa ni sawa ama laa !
Sasa hapo kuna ulazima uongee nae kwa maana ya kumtishia kumwitia watu wazima myazungumze tena.

Anachotakiwa mkeo ni kuonyesha kubadilika mara tu baada ya kuongea hata kama alilia.
 
kwanza huyo shemeji yako uliwahi kutambuliswha hapo awali?i mean unamjua kama shemeji yako tokea siku nyingi au ameibukia from nowhere?maanek isije ikawa ni mume mweznio maanake huo ukarbi sasa hapana ni too much,
 
kwanza huyo shemeji yako uliwahi kutambuliswha hapo awali?i mean unamjua kama shemeji yako tokea siku nyingi au ameibukia from nowhere?maanek isije ikawa ni mume mweznio maanake huo ukarbi sasa hapana ni too much,

Hili nalo neno !
Mjini mipango na akili nyingi nguvu peleka kijijini. Ila ikiwa hivyo tunasema ni "Roho ngumu tU"
 
Maskin wa Mungu lait shemeji yako angejua unavyocheka nae ni unafki umemchoka wallah angeondoka muda huo huo!
 
Itabidi tukague vyeti vya kuzaliwa vya ndugu haswa mashemeji wa kiume haswa kama umeoa mbali na kuwajua wote inakuwa ngumu
 
Nilishaongea nae mara kibao ila nikizungumzia swala hili la nduguye huanza kulia na kununa ndio mana nawashirikisha weeeeee

asije akawa mume mwenza a.k. X halafu maskini ya mungu mwenzangu na mm unadhan ni shemeji
 
Yaani ww ..

1. Hukustagili kuoa ,.inaonyesha hukuwa tayari kuoa ,umekutupuka .

2. Mwanaume kamili tena anayesema ana mkr na watoto ,maswala ya kifamilia kama Baba wa nyumba ilikupasa kuyamaliza mwnyewe,hususani swala dogo kama hilo . Ww ndio kichwa .

3. Kuomba ushauri wa kifamilia kwenye Mitandao ya kijamii ni kuiabisha Familia yako ,zaidi ni huyo unayemuita mkeo. Kama swala lilikua kubwa na una uhakika ulifuata taratibu zote za ndoa basi kilichokupasa ni kuchukua hatua za kunuonana na mshauri wako wa ndoa ,na sio kuja kuanika mambo ya familia yako huku .

4. Hujui wajibu wako kwenye ndoa mpaka sasa ,mke kakukalia kooni.

5. Na mwisho ,acha kuiaibisha familia ,zaidi mkeo.
Mko wengi nyie na nilitazamia watu kama nyinyi kujitokeza sishangai
 
asije akawa mume mwenza a.k. X halafu maskini ya mungu mwenzangu na mm unadhan ni shemeji

"Roho ngumu" yaani baada ya ushauri huu hapa najua atakuwa na pa kuanzia pazuri tu.
Unajua haya maisha ya "DNA TEST" magumu sana utakuta jamaa kaja kuweka mimba tu halafu aondoke.
 
Back
Top Bottom