Naamini CWT ni mafisadi tena sana,ila siungi mkono hoja yakuanzisha chama kipya,badala yake nashauri ya fuatayo:
1.Katiba ya CWT ipitiwe upya ili kubaini mapungufu na kuyarekebisha.
2.Mapato ya chama yawekwe bayana na matumizi yake.
3.Ifanyike Auditing KATIKA mali za CWT na repoti ipelekwe kwa wanachama ikajadiliwe
4.Makato ya mshahara yapungue na kuwa kiwango kimoja km vile 2,000/=kwa mwezi kuliko asilimia hiyo 3 au 2inayokatwa sasa hivi kwani:
i.Chama kina rasilimali nyingi kwa sasa tosha kuendeshea chama
ii.Chama kina ingiza wanachama wengi kwa mwaka kutokana na ajira za walimu takribani 25,000 kila mwaka walimu wapya huajiriwa,hivyo michango ya fedha ni nyingi.
iiii.Kiwango cha asilimia 2 au 3 inayokatwa sasa siyo lazima,kwani kiwango hicho kilipangwa wakati chama kikiwa kichanga na kinahitaji mapato mengi kujiendesha,kwa sasa kiwango hicho ni kikubwa.
5.Mfumo wa kuwatunza wanachama wastafu uangaliwe upya,kwani si haki mwanachama amekichangia chama kipindi chote cha utumishi halafu akistaafu aishie kupewa bati 20,atafanyia nini? bati 100 angalau na inawezekana,au apewe mkono wa kwa heri 1,500,00 0/=
6.Mikutano ya mara kwa mara na wanachama na viongozi wakuu iwe inapatiwa kipaumbele nk.
Haya ni mambo machache ya kushughulikia na wengine wanaweza kubainisha na mengine,changamoto hizi zikitatuliwa chama ni kizuri,
Kubomoa nyumba unayoishi na kujenga mpya kwa mara moja si jambo jepesi.
Pia ili kujitoa kutoka chama kilichopo na kujiunga na chama kipya bila kubainisha changamoto zilizopo katika chama cha awali ni kazibure.Utajuaje kama chama kipya hakitakuwa na matatizo?
Karibuni kwa maoni.