george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,177
- 1,823
Naomba uandike hiki kitu kaka kwani mimi kinaniumiza sana, nina miaka 35 sijaolewa nahisi kila mwanaume ananiona Malaya.
Iko hivi, kipindi cha ujana nikiwa chuo kuna mwanaume nilikua naye, kama unavyojua ujana tukachorana tattoo, kiunoni na nyingine kwenye paja juu kabisa.
Baada ya kumaliza chuo kila mtu akaiangaia mtaani tukaachana, hivyo katika kuifuta ile tattoo nikalazimika kuchora ua kiunoni hivyo ikawa kubwa na hii ya kwenye paja nilichora picha fulani ya ndege hivyo ikawa imepanda juu kabisa karibu na sehemu za siri.
Kaka hiko kitu kimekuwa kikinitesa sana, kila nikiingia kwenye mahusiano nikishakutana na mwanaume kimwili tu unamuona anabadilika. Napata wanaume kweli lakini wanaona kama vile mimi ni Malaya, yaani siwaelewi kabisa.
Kuna wakati niliamua kutokutana kimwili kabisa na mwanaume mpaka ndoa. Kweli kuna kijana mmoja yeye ni mlokole alinikubalia na kila kitu kilikaa vizuri tulikaa mwaka bila kukutana kimwili. Akaja kwetu na kunipeleka kwao.
Ila kuna siku sijui ilikuaje akaona picha yangu moja ya zamani ambayo nilipost Facebook. Kaka ni ya zamani sana kiasi kwamba hata siijui kwani hata Facebook situmii na hiyo akaunti sina hata password yake. Tulikua tunaogelea na marafiki zangu sasa nilivaa nguo za kuogelea hivyo zile Tattoo zikaonekana.
Akaniuliza, "Huyu ni nani?" Nililazimika kumuambia ukweli kwani nilijua nishaharibu. Tangu hapo alibadilika na kusimamisha kila kitu.
Najua ni makosa Kaka niliyofanya na sina namna ya kurekebisha. Lakini naomba uandike kuwa si kila mwanaume anajichora tattoo ni Malaya. Nimechoka Kaka kuachwa kwa vitu vidogo. Waambie wanaume waache ushamba.
Vipi Mdau Una Maoni Gani Kuhusu Jambo Hili....!?
Iko hivi, kipindi cha ujana nikiwa chuo kuna mwanaume nilikua naye, kama unavyojua ujana tukachorana tattoo, kiunoni na nyingine kwenye paja juu kabisa.
Baada ya kumaliza chuo kila mtu akaiangaia mtaani tukaachana, hivyo katika kuifuta ile tattoo nikalazimika kuchora ua kiunoni hivyo ikawa kubwa na hii ya kwenye paja nilichora picha fulani ya ndege hivyo ikawa imepanda juu kabisa karibu na sehemu za siri.
Kaka hiko kitu kimekuwa kikinitesa sana, kila nikiingia kwenye mahusiano nikishakutana na mwanaume kimwili tu unamuona anabadilika. Napata wanaume kweli lakini wanaona kama vile mimi ni Malaya, yaani siwaelewi kabisa.
Kuna wakati niliamua kutokutana kimwili kabisa na mwanaume mpaka ndoa. Kweli kuna kijana mmoja yeye ni mlokole alinikubalia na kila kitu kilikaa vizuri tulikaa mwaka bila kukutana kimwili. Akaja kwetu na kunipeleka kwao.
Ila kuna siku sijui ilikuaje akaona picha yangu moja ya zamani ambayo nilipost Facebook. Kaka ni ya zamani sana kiasi kwamba hata siijui kwani hata Facebook situmii na hiyo akaunti sina hata password yake. Tulikua tunaogelea na marafiki zangu sasa nilivaa nguo za kuogelea hivyo zile Tattoo zikaonekana.
Akaniuliza, "Huyu ni nani?" Nililazimika kumuambia ukweli kwani nilijua nishaharibu. Tangu hapo alibadilika na kusimamisha kila kitu.
Najua ni makosa Kaka niliyofanya na sina namna ya kurekebisha. Lakini naomba uandike kuwa si kila mwanaume anajichora tattoo ni Malaya. Nimechoka Kaka kuachwa kwa vitu vidogo. Waambie wanaume waache ushamba.
Vipi Mdau Una Maoni Gani Kuhusu Jambo Hili....!?