Kujibizana na wakwe...kumewahi kukutokea ?

Kujibizana na wakwe...kumewahi kukutokea ?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,093
Reaction score
43,281
Kuna wakati mtu anajikuta anajibizana vibaya na wakwe kwa sababu mbalimbali. Wanaweza kuwa ni wazazi wa mwenza wako au shemeji na wifi zako. Jamii zetu zinatilia mkazo sana heshima kwa wakwe lakini wakati mwingine vikizidi ni mno. Wanaweza kuleta mawazo ya jinsi ya kusimamia nyumba yako ambayo kwa kweli yanapakana na matusi....umeweza kusurvive au ndoa ikaletwa matatani sababu ya wakwe?

Unashauri wenye matatizo na wakwe wafanye nini?
 
Kujibizana na wakwe ni utovu wa nidhamu
 
siwezi kujibizana na wakwe kama ni wazazi wa mwenza wangu ila kama ni kaka/dada aah hao wakiingia kwenye 18 yangu ninawapa tuu...hasa wakina dada na midomo yao siwezi kuwaachia..everyone has to earn respect so wakitaka heshima na wao watoe heshima
 
Awe mzazi au yoyote akiingi 19 zangu nampa live bila kujali ni mkwe mama au baba ukitaka jiheshimu na fanya yanayokuhusu ila nikikuheshimu sana nitanyamaza kimya ila itakukost maana haitakuwa kama nilivokuwa nakuheshimu zamani. Mzee Mwanakijiji umeshazeeka achna na lile jukwaa la siasa njoo huku MMUutupe uzoefu katika haya siunaona leo umefunguka kivingine zaidi kheheeheh
 
Last edited by a moderator:
Mkwe hata akijamba mbele yako hupaswi kuziba pua
 
Kujibizana na wakwe ni utovu wa adabu kwa kiwango cha juu na hakuna sababu yoyote itakayohalalisha.

Mkwe ni mzazi wa mwenzio.Ukimjibu vibaya ujue mwenye mzazi wake ataumia sana rohoni.
Unachopaswa kufanya pale mkwe kakuboa kupita maelezo ni kumwachia mwenye mzazi wake achukue uamuzi.
Wewe usimjibu mzazi wa mwenzio, mjibu mzazi wako mwenyewe ikibidi.
 
Kuna wakati mtu anajikuta anajibizana vibaya na wakwe kwa sababu mbalimbali. Wanaweza kuwa ni wazazi wa mwenza wako au shemeji na wifi zako. Jamii zetu zinatilia mkazo sana heshima kwa wakwe lakini wakati mwingine vikizidi ni mno. Wanaweza kuleta mawazo ya jinsi ya kusimamia nyumba yako ambayo kwa kweli yanapakana na matusi....umeweza kusurvive au ndoa ikaletwa matatani sababu ya wakwe?

Unashauri wenye matatizo na wakwe wafanye nini?

Utajivunjia heshimu kujibizana na wakwe zako|!
Mkeo naye akimjibu mzazi wako utajisikiaje?
 
Kuna wakati mtu anajikuta anajibizana vibaya na wakwe kwa sababu mbalimbali. Wanaweza kuwa ni wazazi wa mwenza wako au shemeji na wifi zako. Jamii zetu zinatilia mkazo sana heshima kwa wakwe lakini wakati mwingine vikizidi ni mno. Wanaweza kuleta mawazo ya jinsi ya kusimamia nyumba yako ambayo kwa kweli yanapakana na matusi....umeweza kusurvive au ndoa ikaletwa matatani sababu ya wakwe?

Unashauri wenye matatizo na wakwe wafanye nini?

Hakuna sababu ya kujibizana vibaya na mtu yeyote awe ndugu yako au ndugu wa mume/mke wako. Jenga tabia ya kujiamini na siku zote jitahidi kutenda yaliyo ya haki na inapotokea umetenda kinyume uwe mwepesi wa kuomba msamaha. Jitulize, jifunze kukaa kimya na kutafakari kabla hujajibu lolote, usikurupuke, tambua jambo na nyakati za hatari, mdomo wako uwe mzito kutamka usiyokuwa na uhakika nayo. Hii itakusaidia kuishi vizuri na kila mtu, popote.

Ogopa kujiandaa kwa magonvi, yaani usiwe mwepesi kuwaza kuwa eti mtu akija kwenye 18 zangu namlipua, hapana usijiandae kwa mabaya, siku zote waza yaliyo mema. Jifunze kuuepuka uovu. Katika dunia hii hakuna aliyekamilika, kuwa mwepesi kujishusha na kuzielewa tabia za wengine. Jitahidi kuzizuia hasira zako. Simamia msimamo wako usiyumbishwe.
 
Kuna wakati mtu anajikuta anajibizana vibaya na wakwe kwa sababu mbalimbali. Wanaweza kuwa ni wazazi wa mwenza wako au shemeji na wifi zako. Jamii zetu zinatilia mkazo sana heshima kwa wakwe lakini wakati mwingine vikizidi ni mno. Wanaweza kuleta mawazo ya jinsi ya kusimamia nyumba yako ambayo kwa kweli yanapakana na matusi....umeweza kusurvive au ndoa ikaletwa matatani sababu ya wakwe?

Unashauri wenye matatizo na wakwe wafanye nini?

Mimi nawaheshimu sana wakwe zangu na watu wote wa upande wa mke wangu, hawajawahi kuingilia kwa namna yeyote maswala ya ndoa au familia yangu kwa namna yeyote ile nawashukuru sana kwa hilo, lakini hata wangethubutu kufanya hivyo wasingeweza kupata nafasi maana maana sipendi mbali na wakwe hata marafiki au ndugu wa upande wangu waingilie mambo yangu ya kifamilia, japo ushauri ulioletwa kiheshima naweza kuufanyia kazi kama ni wa msingi
 
Nini kujibizana Kuna machalii wanawala mpaka mama wake zao
 
Ushauri mzuri ni kukaa nao mbali. Wazazi wa mwenza wako ni sawa na wazazi wako kwahiyo njia nzuri ya kuepusha mifarakano ni kutokaribiana na kama unahisi kuwa hamuwezi endana kwenye mambo kadha. Katekista wangu aliniambia nilipomuuliza pale mzazi anapokuwa amemkosea mtoto anapashwa kufanya nini, alinijibu njia pekee ya kutotenda dhambi na kuvunja Amri ya mwenyezi Mungu ni kujitahidi kadri kukaa mbali na mzazi mkorofi. Wakwe nao ni wazazi wetu
 
nadhani hapa inategemea na makuzi.

Je, unaweza jibizana na mzazi wako akikuwaza? Unaweza kumpayukia?

Nadhani, hata wake kwa mtazamo wangu ni kama wazazi wangu.

Kama naweza payuka kwa mzazi wangu, basi hata mkwe nitampayukia, ila kama siwezi kwa mzazi wangu nitaanzia wapi kwa mkwe?

Maana hata mzazi wangu ameshaingia kwenye 18 zangu, lakini sioni kumpayukia.

Mfano, mie nina mkamwana hapa kwangu, nilikuwa nashangaa kwa nini ni mzito sana kuamkia, kupokea mtu. Last week nimeenda kwao, sasa nimemwelewa. Familia haina ushirikiano, hakuna kupokelewa, kuamkiana kwa manati, jamani.

Sasa ninajipanga jinsi gani atafundishika ili aweze kuendana na mazingira ya hapa. Vinginevyo ni mtu mzuri ila kuna vitabia vinanishangaza.
 
Kujibizana ni kukosa nidhamu, sio tu na mkwe bali na mtu yeyote aliekuzidi umri. Hata kama atajitahidi kuleta usimamizi nyumbani kwangu najua ni kwa muda tu. Kama ni mtu wa kukaa nae kwa muda mrefu kwa sababu ya ugonjwa, then i will let his son handle her. Same as for my dad ama mama, nitawajibika kumlinda mwenza wangu dhidi ya ukorofi wao. Kama mume ni zombie na anaona sawa mamake anayoyafanya nitamuachia asimamie hiyo nyumba kwa gharama za mwanae entirely na huku nikihakikisha mie na wanangu hatuwi disturbed. Maisha yanaendelea kwa raha zao.

Lakini kujibizana na kukosea heshima mtu ambae angeweza kukuzaa sio kabisa. Ni bora kumkwepa hata kutafuta scholarship bengaz ukafilie mbali
 
sijawahi, maana twaheshimiana, kuanzia mama mkwe hadi mwifi na mashemeji, pia siwezi kumjibu vibaya mama wa mume wangu maana hata mie sitofurahia mama yangu ajibiwe vibaya naa mume wangu....baada ya kusema hayo acha nipate experience hapa
 
Mie siamini ktk kujibishana na yeyote awe mkubwa ama mdogo,huwa naondoka eneo la tukio kuepusha shari....
 
Aisee....poleni sana naona mnafurahishana hapa. Ninao maoni tofauti sana, labda mimi sikulelewa vizuri lakini niliwahi kumwambia msimamo wangu Mama Mkwe na akatafsiri kuwa nimemtukana. Tuliishi mwaka mmoja tukiwa katika hali ya kutosogeleana sana. Nimekutanma na jamaa zangu zaidi ya wanne waliowahi jibizana na Wakwe. Kuna wazazi stubborn jamani msipime....Labda mimi na wenzangu hao wanne hatukulelewa vizuri, lakini nani hapa anaweza kuvumilia Mama Mkwe anayethubutu kukulaumu kwanini huachi hela ya kutosha nyumbani kwako wakati Mkeo kajifungua...Unaacha pesa kiasi fulani jioni ukirudi Mama Mkwe anakwambia uliacha pesa kidogo na baada ya siku 2 anakutaka umruhusu binti yake asafiri kwenda kwake Mkoani eti mpaka miezi kadhaa...Hiyo imemtokea rafiki yangu na akampa live kwamba "Mama umevuka mipaka". Siku ya kutafuta suluhu Mkweo anadai faini ya karibu shilingi milioni moja, lol!
 
Aisee....poleni sana naona mnafurahishana hapa. Ninao maoni tofauti sana, labda mimi sikulelewa vizuri lakini niliwahi kumwambia msimamo wangu Mama Mkwe na akatafsiri kuwa nimemtukana. Tuliishi mwaka mmoja tukiwa katika hali ya kutosogeleana sana. Nimekutanma na jamaa zangu zaidi ya wanne waliowahi jibizana na Wakwe. Kuna wazazi stubborn jamani msipime....Labda mimi na wenzangu hao wanne hatukulelewa vizuri, lakini nani hapa anaweza kuvumilia Mama Mkwe anayethubutu kukulaumu kwanini huachi hela ya kutosha nyumbani kwako wakati Mkeo kajifungua...Unaacha pesa kiasi fulani jioni ukirudi Mama Mkwe anakwambia uliacha pesa kidogo na baada ya siku 2 anakutaka umruhusu binti yake asafiri kwenda kwake Mkoani eti mpaka miezi kadhaa...Hiyo imemtokea rafiki yangu na akampa live kwamba "Mama umevuka mipaka". Siku ya kutafuta suluhu Mkweo anadai faini ya karibu shilingi milioni moja, lol!

huyo mkwe anayedai milioni mzima kweli? Mweeeeeeeh ila hapo walibishana au walizungumza? Inawezekana mie sikumuelewa mleta mada, nilijua kupandishiana kisawasawa na mkwe......
 
huyo mkwe anayedai milioni mzima kweli? Mweeeeeeeh ila hapo walibishana au walizungumza? Inawezekana mie sikumuelewa mleta mada, nilijua kupandishiana kisawasawa na mkwe......
Ni hivi umeacha pesa Mkeo kajifungua tena ana siku 10 hivi. Mama mkwe yupo nyumbani kwako halafu wewe ukienda job huku nyuma ni darasa kwa binti yake, "haiwezekani akawa anakuachia pesa ndogo namna hii"...Jioni ukirudi unamsalimia M'mkwe hakujibu, siku ya pili anaamua kukupa live....hebu mruhusu mtoto wangu nikamuuguze kwangu...hebu niambie utakuwa na ujasiri wa kukaa kimya? @ BADILI TABIA. Baada ya wiki mbili Mama anadai fidia ya shilingi miliioni moja kwamba ametukanwa...
 
Back
Top Bottom