Kujenga Apartments

Kujenga Apartments

Habari zenu wadau..

Mimi ni mdada nakuja kwenu kuomba ushauri.

Nataka kujenga appartments za kisasa ambazo zitakuwa ni sebule, chumba, choo, na jiko.. luku ya kujitegemea na maji kujitegemea. Nimepanga kujenga tatu in a compound.
Sasa bajeti yangu ni kama milioni 100. Kiwanja sina bado.

Je itanitosha kiwanja na ujenzi. Maeneo niliyopanga nitafute kiwanja ni goba kama bei zitakuwa juu sana nakimbilia mapinga..naombeni ushaur wenu juu ya kupata eneo potential kuendana na bajeti yangu
Kuna namna unahitaji ushauri wa kitaalamu kwa kutumia "Leverage" ili ufanye vitu vikubwa kwa pesa kidogo.
 
Mil 30 hapati kiwanja cha kujenga hizo nyumba anazotaka kwa ukubwa huo kwa Goba labda angalau mil 50 na hapo nahs bado ndogo Goba viwanja vimechangamka sasa hivi na kadri siku zinavoenda kodi za nyumba zinakuja juu.
Bei ya Kiwanja kama goba na mapinga ni maeneo ya bei nafuu ikilinganishwa na miji kama Dar, lakini bei hutofautiana kutokana na umbali, kingine, urahisi wa usafiri kama barabara, daladala..., miundombinu ya kimsingi kama umeme na maj,

Makadirio ya bei ya kiwanja kwa goba ni milioni 10 hadi 30 kwa ploti kwa maeneo ya pembezoni, na mapinga ni milioni 5 hadi 20 kwa ploti isiyo na miundombinu.

Maeneo mengine ya bei nafuu ni kama kigambon,, pugu, kibaha, au maeneo ya mikoani kama morogoro ila kama una uwezo wa kuhama..pia zingatia urahisi wa kufika kwenye kiwanja

Bajeti ya Ujenzi
Kwa apartments 3 za kisasa makadirio ya gharama ni,
Ujenzi wa kawaida, shilingi 300,000 hadi 500,000 kwa m². Ukubwa wa kila apartment, studio ya m² 25–35 inatosha (jumla m² 75–105 kwa zote 3). Jumla ya gharama ya ujenzi ni kama 22.5–52.5 milioni, bila kujumuisha miundombinu.

Mambo ya kuongeza kwenye bajeti yako kama maji ya kujitegemea, gharama ya kisima cha maji milioni 5 hadi 15 au tanki la kukusanyia maji ya mvua. Nishati ya kujitegemea Paneli za jua mil 3 Hadi 10 au jenereta kwa dharura. Ufungaji wa choo, Septic tank milioni 2–5,,ukarabati wa kiwanja, kutengeneza barabara ndani ya compound n.k,,,Jumla yaweza kucheza 45.5–117.5 milion

Bajeti yako ya milion 100 inaweza kutosha lakini, chagua kiwanja cha bei ya chini ya 15M,,
Pia fanya ujenzi wa gharama nafuu kwa kutumia vifaa vya kawaida, na kwa kutumia fundi mzuri na muaminifu ila usimamizi muhimu sana,,,,tengeneza miundombinu kwa taratibu (kwa mfano, anza na septic tank, kisha solar baadaye).

nakushaur pia utafute wataalam wa kutengeneza michoro, wakusikilize pia na unachohitaji ili kuepuka gharama zisizohitajika kwa kutengeneza mchoro wenye mambo mengi bila sababu, pia jenga kwa hatua unaeza kuanza na apartments 2, kisha ongeza ya tatu baadaye., narudia simamia mwenyewe, epuka makampuni makubwa ya ujenzi, waajiri fundi wazoefu na waaminifu na ue site kila siku.

Bajeti yako ya TZS 100M inaweza kufikia malengo yako ikiwa utanunua kiwanja cha mil 15–25 pia ukijenga kwa gharama ya chini kwa mfano, 60M kwa ujenzi na miundombinu
Fanya utafiti wa kina wa bei za kiwanja na ubagein bei...Kwa urahisi, anza na kutafuta kiwanja kwa bei chini ya 20M, halafu plan ujenzi kwa bajeti iliyobaki.. kila la heri
 
Mil 30 hapati kiwanja cha kujenga hizo nyumba anazotaka kwa ukubwa huo kwa Goba labda angalau mil 50 na hapo nahs bado ndogo Goba viwanja vimechangamka sasa hivi na kadri siku zinavoenda kodi za nyumba zinakuja juu.
Bora nikazijenge mapinga. Atleast naweza pata plot kwa unafuu na kubwa
 
Habari zenu wadau..

Mimi ni mdada nakuja kwenu kuomba ushauri.

Nataka kujenga appartments za kisasa ambazo zitakuwa ni sebule, chumba, choo, na jiko.. luku ya kujitegemea na maji kujitegemea. Nimepanga kujenga tatu in a compound.
Sasa bajeti yangu ni kama milioni 100. Kiwanja sina bado.

Je itanitosha kiwanja na ujenzi. Maeneo niliyopanga nitafute kiwanja ni goba kama bei zitakuwa juu sana nakimbilia mapinga..naombeni ushaur wenu juu ya kupata eneo potential kuendana na bajeti yangu
Hiyo bajeti Yako inatosha kabisa ila inabidi uwe makini sana tena sana inabidi ujue kulia lia update punguzo kubwa pia Fanya tafiti kabla hujanunua material yoyote ujue bei location yanapopatikana Kwa wingi Cha mwisho jua kua payback period yake ni muda mrefu sana ndio pesa yako itarudi ila gharama za kuziendesha hizo apartment ni kubwa kidogo maana Kuna viujenzi vya mara Kwa mara, na usicheke na yoyote Hata kama anakutomba vizuri ni hayo tu
 
Komaa na Morogoro Rd ndiyo rafiki kwa uwekezaji wa nyumba kwa sasa huko Mapinga sikushauri,ukikosa kiwanja Goba au bei ikawa kubwa sana pandisha Kibamba.

Leo nina mdogo wangu alikuwa anapatania kiwanja Kibamba Luguruni 2km kuingia ndani jamaa wenye nacho wanataka 16mill so bado huko kuna viwanja nafuu kidogo.
 
1749755769393.png
 
Ushauri, kwanza tafuta kiwanja sehemu ambayo ni potential, watu wengi wanapenda kupanga sehemu ambazo zinafikika na ambazo zimeshaendelea
 
Kama kweli wewe ni dada nifuate nikupe ushauri mzuri Hadi utaupenda.Lakini kama ni dume usije
 
Habari zenu wadau..

Mimi ni mdada nakuja kwenu kuomba ushauri.

Nataka kujenga appartments za kisasa ambazo zitakuwa ni sebule, chumba, choo, na jiko.. luku ya kujitegemea na maji kujitegemea. Nimepanga kujenga tatu in a compound.
Sasa bajeti yangu ni kama milioni 100. Kiwanja sina bado.

Je itanitosha kiwanja na ujenzi. Maeneo niliyopanga nitafute kiwanja ni goba kama bei zitakuwa juu sana nakimbilia mapinga..naombeni ushaur wenu juu ya kupata eneo potential kuendana na bajeti yangu
Njoo mapinga kumetulia ndio nipo huku
 
Back
Top Bottom