Bei ya Kiwanja kama goba na mapinga ni maeneo ya bei nafuu ikilinganishwa na miji kama Dar, lakini bei hutofautiana kutokana na umbali, kingine, urahisi wa usafiri kama barabara, daladala..., miundombinu ya kimsingi kama umeme na maj,
Makadirio ya bei ya kiwanja kwa goba ni milioni 10 hadi 30 kwa ploti kwa maeneo ya pembezoni, na mapinga ni milioni 5 hadi 20 kwa ploti isiyo na miundombinu.
Maeneo mengine ya bei nafuu ni kama kigambon,, pugu, kibaha, au maeneo ya mikoani kama morogoro ila kama una uwezo wa kuhama..pia zingatia urahisi wa kufika kwenye kiwanja
Bajeti ya Ujenzi
Kwa apartments 3 za kisasa makadirio ya gharama ni,
Ujenzi wa kawaida, shilingi 300,000 hadi 500,000 kwa m². Ukubwa wa kila apartment, studio ya m² 25–35 inatosha (jumla m² 75–105 kwa zote 3). Jumla ya gharama ya ujenzi ni kama 22.5–52.5 milioni, bila kujumuisha miundombinu.
Mambo ya kuongeza kwenye bajeti yako kama maji ya kujitegemea, gharama ya kisima cha maji milioni 5 hadi 15 au tanki la kukusanyia maji ya mvua. Nishati ya kujitegemea Paneli za jua mil 3 Hadi 10 au jenereta kwa dharura. Ufungaji wa choo, Septic tank milioni 2–5,,ukarabati wa kiwanja, kutengeneza barabara ndani ya compound n.k,,,Jumla yaweza kucheza 45.5–117.5 milion
Bajeti yako ya milion 100 inaweza kutosha lakini, chagua kiwanja cha bei ya chini ya 15M,,
Pia fanya ujenzi wa gharama nafuu kwa kutumia vifaa vya kawaida, na kwa kutumia fundi mzuri na muaminifu ila usimamizi muhimu sana,,,,tengeneza miundombinu kwa taratibu (kwa mfano, anza na septic tank, kisha solar baadaye).
nakushaur pia utafute wataalam wa kutengeneza michoro, wakusikilize pia na unachohitaji ili kuepuka gharama zisizohitajika kwa kutengeneza mchoro wenye mambo mengi bila sababu, pia jenga kwa hatua unaeza kuanza na apartments 2, kisha ongeza ya tatu baadaye., narudia simamia mwenyewe, epuka makampuni makubwa ya ujenzi, waajiri fundi wazoefu na waaminifu na ue site kila siku.
Bajeti yako ya TZS 100M inaweza kufikia malengo yako ikiwa utanunua kiwanja cha mil 15–25 pia ukijenga kwa gharama ya chini kwa mfano, 60M kwa ujenzi na miundombinu
Fanya utafiti wa kina wa bei za kiwanja na ubagein bei...Kwa urahisi, anza na kutafuta kiwanja kwa bei chini ya 20M, halafu plan ujenzi kwa bajeti iliyobaki.. kila la heri