Kujamba, Kupiga chafya na Kucheua kwa sauti

Kichankuli

JF-Expert Member
Dec 18, 2008
887
189
Wakati nikikua, kule kwetu, kucheua kwa nguvu iliashiria shibe. Na kila ilipotokea inalazimu wenzio waliopo karipu wa kufagilie; kama ni mkeo atakwambia "Njiko/Nkabako yani"-ikimaanisha mume wangu, akicheua mwanamke huambiwa "Kibayi yito"-Ikimaanisha ng'ombe jike anayetoa maziwa mengi. Aidha mtu akipiga chafya shurti wenzie wamumwitikie kwa kumwambia "kusa-ikimaanisha fuka. Matendo yote mawili yamekuwa yakifanyika kwa sauti pasibo kulazimika kuwataka radhi wenzio. Lakini pia japokuwa kule kwetu kujamba miongoni mwa kundi la wenzio haikuwa inakubalika bil kujali ushuzi umetolewa kwa sauti kubwa au kimyakimya, kumekuwa na maelezo kwa watu waliowahi kuishi karibu na Wadosi/Wahindi kwamba wao kujamba ni suala la kawaida tu (sina uhakika na hili).

Ambacho ningependa Dr. JF na wadau wengine wa Weledi ya Afya ni kunijulisha:

1) Iwapo kuna madhara yoyote yanayoweza kusababishwa na mtu kubania kutoa ushuzi, chafya au kucheua;
2) Ni ipi njia sahihi na bora kiafya (siyo kiustaarabu) ya kujamba, kucheua na kupiga chafya ati ya kwa sauti au kwa kubania?
 
kichankuli

ni kweli kuna madhara kwa mtu kujibania kutoa ushuzi na chafya,ila kwa case ya kubania ushuzi madhara yake siyo makubwa sana kwani itakusababishia mchafuko tu tumboni,ila katika hili la kujizuia kupiga chafya ni hatari zaidi.

kupiga chafya kunasababishwa na allergy reaction,mara nyingi kabla ya kupiga chafya mtu uweza patwa na muwasho puani,ukiona hali hiyo usijizuie kupiga chafya maana utakapojizuia utasababisha kimiminika na vitu vyote vinavyotoka wakati wa kupiga chafya kuingia katika sinuses (uunganisha sehemu fulani za kinywa na ubongo pia sehemu fulani za uso na ubongo kupitia mishipa ya damu iitwayo vena) na masikio,hali hiyo yaweza kusababisha infection katika sehemu usika pia uweza sababisha ngoma ya sikio kupasuka.

Njia sahihi ya kupunguza kujamba ni kupunguza gasi katika mfumo wa kumeng'enya chakula(tumbo na utumbo). Hakikisha unapunguza kula vyakula vinavyopelekea gasi kwa wingi tumboni na katika utumbo, vyakula hivyo hasa ni vile vya starch mfano viazi na nk pia waweza daktari kwa ushauri zaidi maana wakati mwingine mtu aweza kuwa na walakini katika enzymes wanaohusika na kumeng'enya aina fulani ya chakula hasa starch.

Kuhusu hilo la chafya sina uhakika ila vizuri kupiga chafya hata kama upo katika watu wengi kuliko kujizuia.
 
Kiroboto thanks a lot, ila kuna watu wengine wana tabia mbaya tu ya kubeua kwa nguvu na asione kwamba walio karibu nae watajisikiaje. hata chafya ukiitoa kwenye hadhara basi kiustaarabu useme sorry au excuse me!

Ebu wafundishe na hilo linasaidia sana. Kwa mfano manakula sehemu ya watu wengi, umeshiba unacheua ila ya sauti usifikirie kwamba wenzio wanaweza kuchefukwa kwa sababu ya ukosefu wa ustaarabu.
 
A fart is a combination of normal, everyday gases and small indigestible molecules from your food.

Nitrogen: 20-90% - Since nitrogen is the primary component of our atmosphere, it is also the primary component of your flatulance. It's basically useless filler: the talcum powder of your ass gas.

Carbon Dioxide: 10-30% - CO2 presence in a fart is miniscule in comparison to nitrogen, but it is one of the more abundant chemicals in them. CO2 volume is increased if you drink a large amount of carbonated sodas or drinks.

Hydrogen 0-50% - How someone could have a 50% hydrogen fart is foreign to me, however it is abundant in your farts from the foods and liquids that you ingest.

Oxygen 0-10% - Ends up in your farts the same way that nitrogen does.

Methane 0-10% - People commonly think that methane makes farts stink. This is false, as methane is odorless. However, like hydrogen, methane is flammable so it does enable you to light a fart.

Sulfur compounds and thiols (mercaptans): trace amounts - These are what makes your farts actually smell bad. These chemicals include hydrogen sulfide (rotten egg smell) and dimethyl sulfide. Some of these chemicals are produced by bacteria within the intestines. However, sulfur rich foods like beans, onions, and eggs enable people to produce farts that are much more rancid than normal.
 
huyu jamaa ni mwanaume au mwanamke, ana umri gani sijui? mbona anaongea mambo ya kitotoooooo, kiajabuuuuuu, hivy akili hiii itakuwa imeoa hata mke kweli wajameni?
 
Back
Top Bottom