zema21
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 619
- 251
Wakuu,
Juzi jumatatu nimetumiwa sms ikinielekeza nikacheki kwenye email yangu kuna mail nimetumiwa inayohusu maelekezo ya ajira katika kampuni ya GBM (GLOBAL BUSNESS MACHINE) niliingia kwenye email yangu nikakuta maelekezo yaliyoonyesha kuwa katika kikao walichokaa "tulipo hotel" nimekuwa miongoni mwa watu waliochaguliwa kupata ajira katika kampuni hiyo..Hivyo jumatatu ya tar 23.7.2012 natakiwa kufika eneo la mikocheni karibu na chuo cha bima zilipo ofisi za kampuni hiyo kwa ajili ya certificate verification. Ikaongeza kuwa nifike na academic transcript, cheti cha kuzaliwa, na work permit kama mim sio mtanzania. Pia mahitaji mengine ni kulipa sh 30,000/= kwa ajili ya training itakayofanyika baada ya certificate verification (itafanyikia kcc Nairobi). Malipo yalitakiwa yafanyika kabla ya tar 18.7.2012 kupitia mpesa(wakaweka na namba za malipo) Wakuu nilifurahi nikasema Mungu amejibu maombi yangu ya kupata ajira. Nikafunga safari kuelekea mikocheni kutafuta ofisi za kampuni bila mafanikio kwani hakuna aliwahi kuisikia kampuni hiyo pale. Nilimpigia huyo aliyenitumia sms mara kadhaa haikupokelewa, baada ya masaa mawili alinipigia, nikajitambulisha akaniuliza nipo wapi nikamjibu mwenge. Akaniambia kuwa ofs zao zipo mwanza. Nikamwuliza mbona walisema ofisi zao zipo dar? Akanambia dar wana representative wao. Nikamwomba namba ya simu ya huyo repr akanipa nikajaribu kupiga siku nzima hazipatikani...nimejaribu kumpigia yule jamaa ili nimwambie namba alizonipa hazipatikani lakn hapatikan pia nayeye kutwa nzima!
Wakuu nishaurini nilipie hizo 30,000/= manake jioni ndo deadline..!?
Juzi jumatatu nimetumiwa sms ikinielekeza nikacheki kwenye email yangu kuna mail nimetumiwa inayohusu maelekezo ya ajira katika kampuni ya GBM (GLOBAL BUSNESS MACHINE) niliingia kwenye email yangu nikakuta maelekezo yaliyoonyesha kuwa katika kikao walichokaa "tulipo hotel" nimekuwa miongoni mwa watu waliochaguliwa kupata ajira katika kampuni hiyo..Hivyo jumatatu ya tar 23.7.2012 natakiwa kufika eneo la mikocheni karibu na chuo cha bima zilipo ofisi za kampuni hiyo kwa ajili ya certificate verification. Ikaongeza kuwa nifike na academic transcript, cheti cha kuzaliwa, na work permit kama mim sio mtanzania. Pia mahitaji mengine ni kulipa sh 30,000/= kwa ajili ya training itakayofanyika baada ya certificate verification (itafanyikia kcc Nairobi). Malipo yalitakiwa yafanyika kabla ya tar 18.7.2012 kupitia mpesa(wakaweka na namba za malipo) Wakuu nilifurahi nikasema Mungu amejibu maombi yangu ya kupata ajira. Nikafunga safari kuelekea mikocheni kutafuta ofisi za kampuni bila mafanikio kwani hakuna aliwahi kuisikia kampuni hiyo pale. Nilimpigia huyo aliyenitumia sms mara kadhaa haikupokelewa, baada ya masaa mawili alinipigia, nikajitambulisha akaniuliza nipo wapi nikamjibu mwenge. Akaniambia kuwa ofs zao zipo mwanza. Nikamwuliza mbona walisema ofisi zao zipo dar? Akanambia dar wana representative wao. Nikamwomba namba ya simu ya huyo repr akanipa nikajaribu kupiga siku nzima hazipatikani...nimejaribu kumpigia yule jamaa ili nimwambie namba alizonipa hazipatikani lakn hapatikan pia nayeye kutwa nzima!
Wakuu nishaurini nilipie hizo 30,000/= manake jioni ndo deadline..!?