Kuimarika kwa shilingi imenikera sana!

Kuimarika kwa shilingi imenikera sana!

Mgonjwa shilingi leo hajambo, baada ya kupewa dozi kali ya dola 800m zilikopwa fasta kutoka serikali ya South Africa, bado yupo kwenye uangalizi mkali wa timu ya madaktari bingwa, ambao wamekiri dozi hii bado ni ndogo na nafuu iliyoonekana leo ni ya muda mfupi kama hakuna suluhisho la kudumu la kupata dozi zingine kwa kiwango kikubwa, basi afya ya shilingi itaendelea kutetereka na huenda ikasababisha umauti wake.
 
BOT wameingiza mzigo sokoni baada ya kukosa dollar 800m kutoka RMB ya na Uchina.

Pia makampuni yanalipa wages end month, kwa hiyo hili suluhisho la muda tu
 
Mgonjwa shilingi leo hajambo, baada ya kupewa dozi kali ya dola 800m zilikopwa fasta kutoka serikali ya South Africa, bado yupo kwenye uangalizi mkali wa timu ya madaktari bingwa, ambao wamekiri dozi hii bado ni ndogo na nafuu iliyoonekana leo ni ya muda mfupi kama hakuna suluhisho la kudumu la kupata dozi zingine kwa kiwango kikubwa, basi afya ya shilingi itaendelea kutetereka na huenda ikasababisha umauti wake.

Nchi nyingime hayo mabilioni huingia kwa kuuza bidhaa nje sie mpaka tukope duh!
 
Mkuu, itakuwa ivo. Wamefunika kombe mwanaharamu apite tu. Hii sio internal forces but external.

Kuna member kaongea cream sana "kwa serikali makini,haiwezi kushusha thamani ya pesa kwa kiwango icho na ili khali inajua kuna wafanyabiashara waliokuwa wameguswa kwa namna moja au ingine kwa mpasuko wa bei ya dollar dhidi ya shilling"

I agree with you! Hii ni zima moto serikali imeinject dola za mikopo, na hakika sisi last consumers itatucost!
 
Khaa!! Hivi hizi dola mnazitumia wapi wakuu?? Maana sijawahi hata kuiona mimi ..
 
afadhali ishuke maana nilikuwa nataka niagize gari ila dollar ilikiwa juu sana
 
Nimeahirisha kubadilisha dola hadi shilingi itakaposhuka acha nizitamie hukohuko Bank. Tshs imepanda ghafla mno hii ni nguvu ya soda wenye roho ngumu tunaisubiria huku juu.
 
Views zaidi ya 3,400 wanafatilia huu uzi...ni dhahiri wengi wameumia na huu mporomoko wa $
 
Nimeahirisha kubadilisha dola hadi shilingi itakaposhuka acha nizitamie hukohuko Bank. Tshs imepanda ghafla mno hii ni nguvu ya soda wenye roho ngumu tunaisubiria huku juu.
Ahahaaaa.
SIZITAKI MBICHI HIZI LOL!!!
 
Pole aisee, kumbe na wewe ni miongoni mwa mnaolaani watu wanapopiga kelele malipo yafanyike kwa shilingi

US kuna shilingi? mshahara wangu unaingia TZ kwa dollar, so wakati ule shillingi iko chini mshahara wangu ilipanda sana... hata hivyo angalia mwisho wa comment yangu ile ,,, in general nashukuru kwa serekari kuweza kuthibiti kushuka kwa pesa yetu nikalinganisha na na DRC nilipo.... soma kwanza kabla ya ku koment negatively
 
Nyie mnaotaka sh yetu iendelee kuwa dhaifu ni wapu/uzi na hamna maana.. shida ya miafrika ni mi binafsi kupindukia... huangalii mdhara ya kuporomoka kwa shilingi katika upana wake bali unajiangalia wewe tuu..

hizo dola hata baada ya kuzibadilisha bado zitakumbana na ukweli halisi kuwa uchumi uko hoi..

Hebu onesheni kuwa makini japo kwa kiasi kidogo...
 
Back
Top Bottom