Kuileta Madrid Bongo ni kituko

Mda si mrefu kutakuwa na pata shika nguo chani pale Bernabeu pale itakapo zikutanisha Timu zenye upinzania na vinazofukuzana kwa karibu kwani leo kama R.Madrid ikishinda itakuwa imebakiza point moja tu nyuma ya vinara Barc...eeee Mungu ibariki R.Madrid ipate ushindi mnono

Ni hayo tu
 
Wameshaanza ni dakika ya nne bado hakuna magoli
 
Hii mechi naweza iangalia wapi online waheshimiwa? Si unajua tena wengine hatuna DSTV wala vioo vya kuweza kukamata masafa ya mbali. Kwa mwenye fununu, ni channel gani kwenye internet itaonesha/inaonesha mechi za La Liga na hasa huu mtanange wa leo atudokeze hapa jamvini!
 
balaa gani hili maana TANESCO walikuwa wametufisadi ile umeme unarudi madrid 1 Barc 0 kufumba na kufumbua Mardid 1 Barc 2 daaaaaa kweli soka halitabiliki na bado wanatukosa....
 
Wasipotulia leo Real wanaweza kufungwa mengi sana ngome yao inavuja kupita kiasi.
 
Leo naona Baca wamepania kikweli, magoli: Henry, Puyol na Mesi bado magoli ya Eto'o.
 
Madrid wanadefend kijinga na kizembe! Barca tunao tu J4, pale Stamford Bridge, London SW6
 
BAK, Naona jamaa wanapiga jaramba kwa ajili ya kucheza darajani


Naam, wanajua Stamford wana kazi kubwa sana maana Drogba and company watahaha kuhakikisha wanawatundika BARC na kurudi tena kwenye fainali ya UEFA kwa mwaka wa pili mfululizo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom