muzi
JF-Expert Member
- Jun 17, 2016
- 1,046
- 1,473
Katika ulimwengu wa sasa NO FREE LUNCH, Hata mabilionea duniani hawawezi kukupa pesa bure tu pasipokujiuliza impact ya msaada anaokupa labda kwake yeye, jamii inayokuzunguka, majirani zako, na wadau wote kwa ujumla. Kwa hili kukubaliliwa kujengewa uwanja wa mpira na msikiti mkubwa are there the priorities of the nation??? Je zipo kwenye ilani ya chama. Watakonufaika na uwanja na msikiti ni wangapi.
Ni vijiji vingapi havina maji, huduma ya afya, elimu. Vipi swali NYETI la kujenga viwanda ambalo ndo makakati wa nchi kwa ujumla. Bado nina wasiwasi kuwa ahadi ya kufanya hayo hazikuombwa na mkuu wa kaya BALI ni kitu anachohitaji kufanya mfalme mtukufu mgeni katika ardhi yetu kwa agenda binafsi ya kurahisisha baadhi ya mambo amabayo tutajaona siku za usoni.
TUNAJIDANGANYA TU.
Henry Kissinger wakati Fulani alipata kuishauri serikali ya Marekani enzi hizo. Kwamba ukitaka kulikamata bara la Afrika nenda kamweke sawa Julius Nyerere na Tanzania. Ukimweka sawa Nyerere basi ni rahisi kwa mataifa mengine.
KUHUSU MOROCCO
Miaka 32 iliopita tuliwatangazia Morocco msimamo wetu kupinga mabavu yake huko Sahara Magharibi. Tuliwaambia pia waafrika wenzetu.Tuliutangazia ulimwengu wote. Msimamo wetu ulikuwa kuwaunga mkono Sahara Magharibi ili wajitawale.
Miaka 32 baadaye tumeikaribisha Morocco nchini kwa gego na fizi (Hongereni). Tumeketi mezani kuzungumza na Mfalme Mohammed VI (sina hiyana Naye).
Tumemwambia ushirikiano wetu ni diplomasia ya uchumi, demokrasia na mengineyo. Halafu tumemwambia atujengee nyumba ya Ibada na uwanja wa soka huko Dodoma. Vyote amekubali. Sina tatizo na maombi hayo. Tatizo ni kujidanganya kwetu bila soni.
Toka mwezi Januari mwaka huu kuna kampeni kubwa imeshika kasi Morocco irudishiwe uanachama wa AU. Julai 17 mwaka huu kule Kigali, Rwanda, Mfalme Mohammed VI aliandika barua kwenda kwa Mwenyekiti wa AU, Rais Idris Derb kwamba wapewe nafasi yao AU. Akaomba huruma ya wanachama wa AU(kuna mgawanyiko, na naamini pia utazihusisha Anglophone na Francophone).
Morocco imefanikiwa kushawishi baadhi ya wanachama kwa Afrika kaskazini na magharibi. Kwa upande wa nchi za SADC Ina maana Morocco wamefuata ushauri wa Henry Kissinger, ikamate Tanzania na mengine yatafuata. Naamini kwa SADC ni Tanzania na Afrika kusini tu. Wanachama wa EAC hawana ubavu huo ukiondoa Tanzania.
Sasa tumemtangazia "njaa" Mfalme. Tunamtegemea "kiuchumi" atufadhili. Hivi utakuwa na msimamo gani dhidi yake? Hivi Mfalme hawezi kusema aungwe mkono kwenye juhudi za kurejea AU? Halafu sharti lake ni kwamba Sahara Magharibi ibakie kuwa sehemu yake.
Tunajua Novemba wakuu wa Afrika wamekaribishwa Morocco. Naamini hakuna sababu ya kujidanganya wala kumung'unya maneno.
Tuseme kuwa tumebadili msimamo na tunaungana na Morocco. Ama baniani mbaya Kiatu chake dawa? Nimeambiwa ni suala la kibiashara ndicho tunachojali. Heee! Hakika hayo?? Tunajidanganya mno.
Tuseme ukweli tumekamatwa tayari. Nadhani pia siyo mbali sana ila siyo sasa, tutawakaribisha Israel, na pengine hata Makaburu wangekuwepo Afrika kusini tungewapa mwaliko.
Mimi yangu ni hayo tu. Na wazo hili ruksa kulibishia.
Wasaalamu. ©Markus Mpangala "Markus M.M
Ni vijiji vingapi havina maji, huduma ya afya, elimu. Vipi swali NYETI la kujenga viwanda ambalo ndo makakati wa nchi kwa ujumla. Bado nina wasiwasi kuwa ahadi ya kufanya hayo hazikuombwa na mkuu wa kaya BALI ni kitu anachohitaji kufanya mfalme mtukufu mgeni katika ardhi yetu kwa agenda binafsi ya kurahisisha baadhi ya mambo amabayo tutajaona siku za usoni.
TUNAJIDANGANYA TU.
Henry Kissinger wakati Fulani alipata kuishauri serikali ya Marekani enzi hizo. Kwamba ukitaka kulikamata bara la Afrika nenda kamweke sawa Julius Nyerere na Tanzania. Ukimweka sawa Nyerere basi ni rahisi kwa mataifa mengine.
KUHUSU MOROCCO
Miaka 32 iliopita tuliwatangazia Morocco msimamo wetu kupinga mabavu yake huko Sahara Magharibi. Tuliwaambia pia waafrika wenzetu.Tuliutangazia ulimwengu wote. Msimamo wetu ulikuwa kuwaunga mkono Sahara Magharibi ili wajitawale.
Miaka 32 baadaye tumeikaribisha Morocco nchini kwa gego na fizi (Hongereni). Tumeketi mezani kuzungumza na Mfalme Mohammed VI (sina hiyana Naye).
Tumemwambia ushirikiano wetu ni diplomasia ya uchumi, demokrasia na mengineyo. Halafu tumemwambia atujengee nyumba ya Ibada na uwanja wa soka huko Dodoma. Vyote amekubali. Sina tatizo na maombi hayo. Tatizo ni kujidanganya kwetu bila soni.
Toka mwezi Januari mwaka huu kuna kampeni kubwa imeshika kasi Morocco irudishiwe uanachama wa AU. Julai 17 mwaka huu kule Kigali, Rwanda, Mfalme Mohammed VI aliandika barua kwenda kwa Mwenyekiti wa AU, Rais Idris Derb kwamba wapewe nafasi yao AU. Akaomba huruma ya wanachama wa AU(kuna mgawanyiko, na naamini pia utazihusisha Anglophone na Francophone).
Morocco imefanikiwa kushawishi baadhi ya wanachama kwa Afrika kaskazini na magharibi. Kwa upande wa nchi za SADC Ina maana Morocco wamefuata ushauri wa Henry Kissinger, ikamate Tanzania na mengine yatafuata. Naamini kwa SADC ni Tanzania na Afrika kusini tu. Wanachama wa EAC hawana ubavu huo ukiondoa Tanzania.
Sasa tumemtangazia "njaa" Mfalme. Tunamtegemea "kiuchumi" atufadhili. Hivi utakuwa na msimamo gani dhidi yake? Hivi Mfalme hawezi kusema aungwe mkono kwenye juhudi za kurejea AU? Halafu sharti lake ni kwamba Sahara Magharibi ibakie kuwa sehemu yake.
Tunajua Novemba wakuu wa Afrika wamekaribishwa Morocco. Naamini hakuna sababu ya kujidanganya wala kumung'unya maneno.
Tuseme kuwa tumebadili msimamo na tunaungana na Morocco. Ama baniani mbaya Kiatu chake dawa? Nimeambiwa ni suala la kibiashara ndicho tunachojali. Heee! Hakika hayo?? Tunajidanganya mno.
Tuseme ukweli tumekamatwa tayari. Nadhani pia siyo mbali sana ila siyo sasa, tutawakaribisha Israel, na pengine hata Makaburu wangekuwepo Afrika kusini tungewapa mwaliko.
Mimi yangu ni hayo tu. Na wazo hili ruksa kulibishia.
Wasaalamu. ©Markus Mpangala "Markus M.M