Kuibadili gesi asilia kuwa petroli na dizeli kunaweza punguza gharama tunazotumia kuagiza mafuta kutoka nje

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,328
8,246

Kuibadili gesi asilia yetu kuwa mafuta ya petroli na dizeli kunaweza punguza gharama tunazotumia kuagiza mafuta hayo kutoka mataifa ya nje​


Ni hivi wakuu,

Gesi asilia imeundwa kwa kampoundi zinazoitwa methane (CH4). Kampaundi hizo zina kaboni moja na hydrojeni nne.

Petroli imeundwa kwa kampoundi zenye kaboni kuanzia 6 hadi 12.

Dizeli imeundwa kwa kampaundi zenye kaboni kuanzia 12 hadi 20.

Mafuta ya taa yameundwa kwa kampaundi zenye kaboni kuanzia 9 mpaka 16.

Mafuta ya ndege yameundwa kwa kampaundi zenye kaboni kuanzia 9 mpaka 16.

Wakati wa kuibadili gesi asilia kuwa mafuta, hapo kinachofanyika ni kufanya miungano ya kikemikali kuzibadili hizo kampaundi za methane zenye kaboni moja zilizomo ndani ya gesi asilia kutupatia kampaundi zenye kaboni kuanzia sita hadi 20 na zaidi ambazo zinapatikana kwenye mafuta.

Kisha kinachofanyika baada ya hapo ni kufanya utenganisho wa kikemikali kupata petroli, dizeli, mafuta ya taa, LPG, na prodakti zingine.

Hatua ya kwanza gesi asilia inabidilishwa kuwa kaboni monoksaidi na hydrojeni gesi.

Hatua ya pili monoksaidi na hyrojeni ziaungana kutengeneza kampaundi zenye kaboni nyingi na hydrogeni nyingi.

Hatua ya tatu kampaundi zenye kaboni nyingi na hydrojeni zilizotengenezwa zinatenganishwa kutoa petroli, dizeli, mafuta ya taa, mafuta ya injini, nk.

Njia nyingine niya kutengeneza petroli moja kwa moja.

Hapa hatua ya kwanza gesi asilia inabadilishwa kuwa koboni monoksaidi na hydrojeni.

Hatua ya pili kaboni monoksaidi na hydrojeni zinaunganishwa kutengeneza methanol.

Hatua ya tatu methanol inabadilishwa kuwa petroli.

Hivi ndivyo wenzetu CHINA, SOUTH AFRICA, na mataifa mengine wanavyoibadilisha gesi asilia kutengeneza mafuta.

Hii ndio tunaita natural gas value chain to get valueble products. Au Natural Gas utilization.

Kwenye Tanzania Natural Gas Utilization Master Plan ya Wizara ya Nishati 2016 hadi 2045 hivi viwanda vyote vipo. Na hesabu zilishapigwa kilichobaki ni utekelezaji tu.
 
Nakubaliana nawe kabisa kwa hili, ni muhimu tukaanza kufikiri kwa kushirikiana na ubongo, yes bei ya mafuta inazidi kupaa juu na itaendelea kuongezeka kama nchi na sisi wenyewe tujitahidi kufanya yafuatayo ili tupunguze utumiaji wa mafuta; tuimarishe na tuboreshe public transport, hii itasaidia mno kupunguza magari barabarani; barabara zetu tuzivunje na kuzijenga upya hizi za sasa ni uchafu fulani; Driving skills kwa madereva ni muhimu to avoid stop and driving maana hii style unatumia mafuta mengi na jaribu sana kucheza na traffic lights ili usisimame pale.
 

Kuibadili gesi asilia yetu kuwa mafuta ya petroli na dizeli kunaweza punguza gharama tunazotumia kuagiza mafuta hayo kutoka mataifa ya nje​

Gharama kwani anayeleta mafuta nani? si mashirika binafsi haina mahusiano na gharama zozote kwa serikali ndio kwanza serikali inanufaika na tax. ungesema kwa mtu binafsi kama unataka kupunguza gharama za matumizi ya mafuta iko technology ya kufunga gas kwenye gari ila tatizo sina uhakika kama gari za diesel inafaa sina uhakika na hili ila watu wanatumia hii kitu.
 
Tumeshindwa hata kutumia hiyo gas kumaliza tatizo sugu la umeme, kweli kabisa tumeshindwa kunua generators na kutumia gas yetu kumaliza tatizo la umeme? naanza kupata wasiwasi inawezekana hatuna gas tunayofikiria tunayo au serikali na viongozi wake wana ugonjwa wa akili
 
Gharama kwani anayeleta mafuta nani? si mashirika binafsi haina mahusiano na gharama zozote kwa serikali ndio kwanza serikali inanufaika na tax. ungesema kwa mtu binafsi kama unataka kupunguza gharama za matumizi ya mafuta iko technology ya kufunga gas kwenye gari ila tatizo sina uhakika kama gari za diesel inafaa sina uhakika na hili ila watu wanatumia hii kitu.
Mkuu naomba fikiria tena. Kuna kitu hujafikiria vizuri. Ukishindwa kabisa ndio nitakufumbua macho bei zitakavyopungua.
 
Tumeshindwa hata kutumia hiyo gas kumaliza tatizo sugu la umeme, kweli kabisa tumeshindwa kunua generators na kutumia gas yetu kumaliza tatizo la umeme? naanza kupata wasiwasi inawezekana hatuna gas tunayofikiria tunayo au serikali na viongozi wake wana ugonjwa wa akili
😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃
 
Back
Top Bottom