Ndugu zangu,
Usiku huu nime-google jina langu ndipo nimekutana na habari hii; ' Maggid Mjengwa ana virus?
Nimejadiliwa katika angle hiyo kwa kile kilichodaiwa na mwanzisha mada kuwa Mjengwablog haikurusha picha za tamasha la anti virus.
Ukweli habari na mjadala huo umeniburudisha na kunipa elimu pia. Ama hakika, ishi ujionee na ujifunze kutoka kwa wanadamu wenzako.
Kwamba nimeshambuliwa binafsi kwa kuwa Mjengwablog haiku-post picha za tamasha la Anti- Virus. Na ni jana tu hapa Iringa nimenunua kitabu cha Mr. Sugu kuhusu maisha yake- From Streets to The parliament.
Ndugu zangu,
Mie naishi na kufanya kazi Iringa. Ni mahali ambapo hata mtandao wa intaneti wakati mwingine ni wa shida. Na kublogu huku tunajitolea tu. Hata matangazo ya maana kwenye blogu wengine sisi hatuna. Ukweli tumeamua kuwa ' suguz'. Watu tuliojitolea kwa miaka mingi, kuwa tutapambana hadi risasi ya mwisho. Ndio maana, tunatumia senti za mifukoni mwetu kuendesha blogu zetu. Na mimi kazi ya kublogu naifanya nikiwa na wakati ziada.
Tena siku hizi nina mwanafunzi wangu aliye Dar na anayejitolea wakati mwingine kuifanya kazi hiyo. Kuhusu picha za tamasha hilo linalosemwa nami niliziona zimetundikwa kwenye Mjengwablog na mwanafunzi wangu huyo.
Niwahakikishie, kuwa Mjengwablog ni blogu huru. Haijapata kununuliwa na haitakuja kununuliwa kufanya kazi za kishabiki. Na mimi kama mmiliki wa blogu ndivyo nilivyo. Sijapata kununuliwa na sitakuja kununuliwa nimfanyie mtu kazi ya kishabiki na isiyo na maslahi ya kitaifa.
Pamoja na yote hayo. Niseme tu, kwa hata mabaya yaliyoandikwa hapa juu yangu, sina kinyongo na mtu. Na nirudie, niliyosoma hapa usiku huu yameniburudisha pia. Nimebaki nikicheka mwenyewe kuona jinsi watu wanavyonifikiria, kunituhumu na kunihukumu, bila hata kunipa nafasi ya kunisikiliza.
Nawatakia usiku mwema.
Maggid,
Iringa.
.
Usiku huu nime-google jina langu ndipo nimekutana na habari hii; ' Maggid Mjengwa ana virus?
Nimejadiliwa katika angle hiyo kwa kile kilichodaiwa na mwanzisha mada kuwa Mjengwablog haikurusha picha za tamasha la anti virus.
Ukweli habari na mjadala huo umeniburudisha na kunipa elimu pia. Ama hakika, ishi ujionee na ujifunze kutoka kwa wanadamu wenzako.
Kwamba nimeshambuliwa binafsi kwa kuwa Mjengwablog haiku-post picha za tamasha la Anti- Virus. Na ni jana tu hapa Iringa nimenunua kitabu cha Mr. Sugu kuhusu maisha yake- From Streets to The parliament.
Ndugu zangu,
Mie naishi na kufanya kazi Iringa. Ni mahali ambapo hata mtandao wa intaneti wakati mwingine ni wa shida. Na kublogu huku tunajitolea tu. Hata matangazo ya maana kwenye blogu wengine sisi hatuna. Ukweli tumeamua kuwa ' suguz'. Watu tuliojitolea kwa miaka mingi, kuwa tutapambana hadi risasi ya mwisho. Ndio maana, tunatumia senti za mifukoni mwetu kuendesha blogu zetu. Na mimi kazi ya kublogu naifanya nikiwa na wakati ziada.
Tena siku hizi nina mwanafunzi wangu aliye Dar na anayejitolea wakati mwingine kuifanya kazi hiyo. Kuhusu picha za tamasha hilo linalosemwa nami niliziona zimetundikwa kwenye Mjengwablog na mwanafunzi wangu huyo.
Niwahakikishie, kuwa Mjengwablog ni blogu huru. Haijapata kununuliwa na haitakuja kununuliwa kufanya kazi za kishabiki. Na mimi kama mmiliki wa blogu ndivyo nilivyo. Sijapata kununuliwa na sitakuja kununuliwa nimfanyie mtu kazi ya kishabiki na isiyo na maslahi ya kitaifa.
Pamoja na yote hayo. Niseme tu, kwa hata mabaya yaliyoandikwa hapa juu yangu, sina kinyongo na mtu. Na nirudie, niliyosoma hapa usiku huu yameniburudisha pia. Nimebaki nikicheka mwenyewe kuona jinsi watu wanavyonifikiria, kunituhumu na kunihukumu, bila hata kunipa nafasi ya kunisikiliza.
Nawatakia usiku mwema.
Maggid,
Iringa.
.