VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kwa mujibu wa Katiba na Sheria zetu zinazoliongoza Bunge, Rais ni sehemu ya Bunge. Kama Rais aliridhia (kwa kuusoma au kusomewa au kutafsiriwa mkataba wa kuikodisha Bandari yetu kwa DP Word) kusainiwa kwa mkataba huo, sehemu moja ya Bunge imeshaupitisha. Mnaelewa?
Kichama, Rais ni Mwenyekiti wa CCM. Bunge 'lote' linatokana na CCM. Kama Mwenyekiti ameuona; ameoneshwa; ameusoma; amesomewa; ametafsiriwa au ameutafsiri mkataba huo kabla ya kusainiwa kwake, kuna Mbunge wa kupimana ubavu na Mwenyekiti? Mnaandika lakini?
Amini nawaambia, mtu pekee wa kufanya vile watanzania wanavyotaka kuhusiana na mkataba huo (kuhusu masuala muhimu kama muda wa mkataba; maslahi tuyapatayo kama taifa; athari za hatari za mkataba huo; umuhimu wa mkataba huo na mambo mengineyo) ni Rais na Mwenyekiti wetu. Tuko pamoja?
Hakuna kama yeye. Ni yeye tu. Mengine yote yatakuwa ni maigizo kulingana na maagizo. Amini nawambieni, kama ilivyo ada, mtengeneza tatizo ndiye 'atakayelitatua'. Na atashangiliwa. Mnabisha? Subirini mjionee.
Caucus ina ukakasi wa kasi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Kichama, Rais ni Mwenyekiti wa CCM. Bunge 'lote' linatokana na CCM. Kama Mwenyekiti ameuona; ameoneshwa; ameusoma; amesomewa; ametafsiriwa au ameutafsiri mkataba huo kabla ya kusainiwa kwake, kuna Mbunge wa kupimana ubavu na Mwenyekiti? Mnaandika lakini?
Amini nawaambia, mtu pekee wa kufanya vile watanzania wanavyotaka kuhusiana na mkataba huo (kuhusu masuala muhimu kama muda wa mkataba; maslahi tuyapatayo kama taifa; athari za hatari za mkataba huo; umuhimu wa mkataba huo na mambo mengineyo) ni Rais na Mwenyekiti wetu. Tuko pamoja?
Hakuna kama yeye. Ni yeye tu. Mengine yote yatakuwa ni maigizo kulingana na maagizo. Amini nawambieni, kama ilivyo ada, mtengeneza tatizo ndiye 'atakayelitatua'. Na atashangiliwa. Mnabisha? Subirini mjionee.
Caucus ina ukakasi wa kasi!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)