Profesy
JF-Expert Member
- Jun 24, 2009
- 385
- 13
Baada ya msuguano wa #Posho, Bunge letu maalum la Katiba limepoteza karibu wiki nyingine nzima kubishana kuhusu uamuzi wa kuwa na Kura ya Wazi au Kura ya Siri. Tayari wiki mbili zimepita la Bunge la siku 70 (wiki 7) lakini yaliofanyika ni majadiliano ya Posho na hili la kura.Hili linatuonyesha kabisa wengi wa wakilishi wetu katika hili Bunge wameenda zaidi kimaslahi yao binafsi au ya kichama. Tunachosahau ni kwamba hili ni Bunge maalum la Katiba na walionda huko ni wawakilishi wa wananchi na maslahi yanatakiwa yawe ya wananchi na nchi yetu kwa ujumla (national interests).Ingawa nimejitahidi sana kunyamaza huku nikifatilia mitandaoni na kwenye magazeti, nimeona nisiendelee kunyamaza. Wiki hii nilichambua kitabu cha Chinua Achebe There Was A Country: A Personal History of Biafra na kati ya mambo ambayo Achebe alihimiza ni kuwa waandishi lazima washiriki katika harakati za kisiasa. Kwa maneno mengine lazima waandike la sivyo watakuwa tu kama footnotes. Hilo ndo nililojifunza sana na ukisoma uchambuzi wangu utaona ata nimenukuu aya nzima kutoka kwa Achebe kuonyesha umuhimu wa kuandika. Hivyo nami nimeona nisikae kimya tena kuhusu hili swala la Kura ya Siri au Kura ya Wazi.Kidemokrasia kabisa na kwa mantiki ya Bunge Maalum kama hili la Katiba hoja yenye nguvu ni ya Kura Ya Wazi. Kwa nini? Kwa sababu zifuatazo:
SOURCE: Kuhusu Kura Ya Wazi au Kura Ya Siri #BungeKatiba | Aikande Kwayu
- Bunge hili linawakilisha wananchi katika makundi mbali mbali. Waliotumwa ni wawakilishi wa hayo makundi hivyo wanatakiwa maamuzi yao yawe wazi ili wanaowakilishwa wajue wawakilishi wao walisimamia lipi.
- Kusema kuwa wawakilishi wataogopa vyama vyao na hawatakuwa na uhuru wa kusimamia wanachoamini ni UOGA na pia KUZALALISHA utume ambao wawakilishi hawa wamepewa na makundi yao na pia Rais. Wewe kama umepewa utume na nafasi kama hii ni kwamba umeaminika kuwa una uwezo wa kuchambua na kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya wananchi na Taifa. Kwa nini uogope leo kusema kwa wazi msimamo wako?
- Kura Ya Wazi itasaidia wajumbe KUWAJIBIKA na maaumuzi waliofanya. Nimekumbuka sana kampeni za 2008 za Marekani ambapo Obama alimshinikiza Mama Clinton kuwajibika na kura yake ya kupitisha vita vya Iraki. Kura za jambo lile muhimu zilikuwa za wazi na ndio maana inajulika ni nani alipigia nini. Uingereza wabunge nao wanapiga kura za wazi kwenye mambo muhimu na wale ambao wanapingana na misimamo ya vyama vyao wanajulikana na huwa wanaitwa rebels. Na hii ni ilama ya demokrasia maana mtu ana uhuru wa mawazo na msimamo wake. Kwa mifano zaidi na michanganuo juu ya rebellions in parliament angalia Rates of rebellion, 1945-2014 | Revolts . Kwa hiyo hakutakuwa na neno kukiwa kuna rebels ambao watapingana na misimamo ya vyama vyao katika vifungu flani flani vya katiba. Huu ndio utashi wa kidemokrasia. Mbona Mbunge Esther ameweza kuwa kinyume na msimamo wa chama chake na kutetea kura ya siri? Hivyo angeweza pia kupiga kura ya wazi kwa jambo ambalo si sawa na msimamo wa chama chake.
SOURCE: Kuhusu Kura Ya Wazi au Kura Ya Siri #BungeKatiba | Aikande Kwayu