Kuhusu kumiliki ardhi Zanzibar, wengi hatukumwelewa Rais Hussein Mwinyi

Makonyeza

Member
Feb 2, 2020
69
252
Nimepitia kurasa kadhaa katika mitandao ya kijamii kama Facebook, magroup ya WhatsApp na Jamii Forums watu wakiijadili kauli ya Rais WA Zanzibar Dr. Hussein Ally Mwinyi alioitoa akikisisitiza kwamba Mtanzania Bara haruhusiwi kumiliki ardhi KISIWANI Zanzibar.

Wengi wa wachangiaji wameonekana kutokubaliana na kauli yake na wengine wakienda mbali zaidi kuulaani Muungano kuonekana hauna maana wakilinganisha na ukweli kwamba Mzanzibar anaruhusiwa kumiliki ardhi Tanganyika kwa Kadri ya uwezo wake.

Suala ka Mungano ni suala mtambuka linalohitaji Mijadala yake binafsi. Na naomba nikiri na mimi kwamba ni kweli Muungano una changamoto zake nyingi tu, inazohitaji hekima za viongozi wetu katika kuzitatua. Leo sitozungumzia sana huko, nitajikita hapa kwenye suala la ardhi tu.

Kwanza ifahamike Ardhi si jambo la Muungano. Naam, si suala ambalo nchi hizi mbili Tanganyika na Zanzibar zimekubaliana kushare kwa mujibu wa ule mkataba wa Muungano uliosainiwa na wazee wetu.

Hii ndio kusema kwamba kila upande wa Muungano una ardhi yake na sheria zake binafsi zinazoongoza na kusimamia matumizi ya ardhi kwao.

Na ni kwa sababu hiyo Zanzibar ina wizara yake ya ardhi kama ilivyo kwa serikali ya Muungano(ilipaswa iwe serikali ya Tanganyika).
Sasa basi, kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya Zanzibar, sharti la mtu kumiliki ardhi ni lazima awe Mzanzibar wa kuzaliwa(Zanzibariz by birth), wakati huku kwetu Bara sharti ni kuwa Mtanzania tu inatosha kumilikishwa ardhi,bila kujali huo utanzania wako umeupataje, almuhimu iwe ni uraia halali kwa mujibu wa sheria zetu (wa kuzaliwa au wa kuomba).

Sheria zetu hutungwa kwa malengo, kila sheria ikitungwa hutungwa kwa sababu, ikilenga jambo au dhamira fulani.

Zanzibar ina eneo la Ukubwa wa kilomita za mraba 1650(wengine wanasema 2000),wakati Tanzania Bara Ukubwa wake ni kilomita za mraba 945,000 ikiwa ndio nchi yenye ardhi kubwa zaidi kuliko nchi zote za Afrika ya nashariki.

Sasa kutokana na udogo wa ardhi ya Zanzibar ndipo ilipokubaliwa kwamba isiwe sehemu ya Muungano na sheria rafiki itungwe ili kuilinda ardhi hiyo.

Kumbuka ndani ya kilomita hizo za mraba 2000 (ambazo ndo ndogo hata kwa Jiji la Dodoma kwa zaidi ya kilomita za mraba 600), Wanzanzibar wapatao 1,500,000/-(kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012)wanahitaji ardhi kwa matumizi ya makazi, maeneo ya wazi, viwanda na Uwekezaji, ardhi ya akiba, ardhi ya mkakati wa kimazingira kuhifadhi uoto wa asili na misitu, huduma za jamii(hospital na mashule/vyuo) na kilimo japo cha kiwango cha kawaida(small scale farming).

Ukigawanya Ukubwa wa ardhi iliyopo na idadi yao unakuta ardhi waliyonayo ni ndogo sana. Na wasiwasi upo kutokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kutokana na kasi waliyonayo kwenye kuzaliana ambayo inatajwa ni asilimia 4 kwa kila mwaka(wenzetu wanazaliana sana), kuna kila dalili Kuna wakati ardhi ya Zanzibar haitowatosha hata Wazanzibar wenyewe. Kwa kuangalia mbali ililazimu kuweka mazingira ya kuilinda ardhi Yao.

Pengine kama haitodhuru Sasa wangepaswa kuanzia kujipanga kugawa ardhi kwa kwenda juu, yaani hati ya ardhi itolewe juu ya nyumba iliyokwishajengwa.

Sasa nirudi kwa kauli ya Rais Hussein Mwinyi, inawezekana maneno aliyotumia hakueleweka, lakini alichomaanisha ni kwamba kwa ardhi ya Zanzibar kila mtu ataruhusiwa kumiliki lakini kwa utaratibu tofauti na unaotumika huku kwetu Bara.

Kwa maana kwamba, kwa wa Zanzibar kumiliki ardhi watatakiwa kuthibitisha uzanzibar wao kwa kuzaliwa. Na kwa asiye MZanzibar atamiliki ardhi kwa njia ya Uwekezaji pekee. Yaani anaweza kusajili kampuni ndani ya Zanzibar na kampuni hiyo kwa sababu umesajili wa Zanzibar itaruhusiwa kumiliki ardhi (zingatia kwamba Kampuni ni mtu kisheria, yaani legal person).

Na kwa kusajili kampuni bila shaka dhamira ya mwenye kampuni ni kuwekeza sehemu fulani, Ndiyo kauli ya Mheshimiwa Rais Mwinyi ilitokea hapo.

Hivyo ndivyo ilivyo hata huku kwetu Bara, licha ya haki ya kumiliki kuwa wazi kwa Mtanzania yeyote, lakini umiliki huo una Kikomo, unaweza kupewa miaka 33,66 au 99, Yote ndo yale yale tu, ni sawa na Abdallah kumuita Dulla tu. Muda huo ukiisha ardhi si yako inarudi kwa Rais. BADO umekodishwa hujamilikishwa.

Lakini tusijisahau, sababu wanayoitumia Zanzibar kutoruhusu wasio wa Zanzibar kumiliki ardhi, kimsingi Ndiyo tunayo tumia na sisi kukataa kufungua mipaka ya jumuiya ya Afrika ya nashariki kwenye ardhi kwa kuhofia Wakenya kuja kuitwaa ardhi yetu yote(jambo ambalo binafsi silikubali)

Kwako Mtanzania Bara, kama unataka kumiliki ardhi Zanzibar ni rahisi sana, nenda kasajili kampuni, utapata kibali cha kufanya biashara Zanzibar, then tumia kampuni yako kuomba ardhi, utapewa bila kinyongo.

Muungano udumuuuuuuuu

_20220428_134845.JPG
 
Watu wa visiwani wanamiliki mahekari kwa maelfu uku bara ila kwao hata hawataki tuende
 
Kumbuka ndani ya kilomita hizo za mraba 2000 (ambazo ndo ndogo hata kwa Jiji la Dodoma kwa zaidi ya kilomita za mraba 600), Wanzanzibar wapatao 1,500,000/-(kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012)wanahitaji ardhi kwa matumizi ya makazi, maeneo ya wazi, viwanda na Uwekezaji, ardhi ya akiba, ardhi ya mkakati wa kimazingira kuhifadhi uoto wa asili na misitu, huduma za jamii(hospital na mashule/vyuo) na kilimo japo cha kiwango cha kawaida(small scale farming)
Kwanini wanang'ang'ania kuitwa nchi!! Ipo siku watajutia kukataa kuwa moja ya wilaya za mkoa wa Pwani au Dar
 
Na wasiwasi upo kutokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kutokana na kasi waliyonayo kwenye kuzaliana ambayo inatajwa ni asilimia 4 kwa kila mwaka(wenzetu wanazaliana sana) , kuna kila dalili Kuna wakati ardhi ya Zanzibar haitowatosha hata Wazanzibar wenyewe. Kwa kuangalia mbali ililazimu kuweka mazingira ya kuilinda ardhi Yao.

Hawataki kujitambua hawafikirii kesho ya vizazi vyao
 
Sasa basi, kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya Zanzibar, sharti la mtu kumiliki ardhi ni lazima awe Mzanzibar wa kuzaliwa(Zanzibariz by birth), wakati huku kwetu Bara sharti ni kuwa Mtanzania tu inatosha kumilikishwa ardhi,bila kujali huo utanzania wako umeupataje, almuhimu iwe ni uraia halali kwa mujibu wa sheria zetu (wa kuzaliwa au wa kuomba).
Yale mahoteli yote makubwa ni ya wazanzibar?
 
Sasa nirudi kwa kauli ya Rais Hussein Mwinyi, inawezekana maneno aliyotumia hakueleweka, lakini alichomaanisha ni kwamba kwa ardhi ya Zanzibar kila mtu ataruhusiwa kumiliki lakini kwa utaratibu tofauti na unaotumika huku kwetu Bara.
Kwa maana kwamba, kwa wa Zanzibar kumiliki ardhi watatakiwa kuthibitisha uzanzibar wao kwa kuzaliwa. Na kwa asiye MZanzibar atamiliki ardhi kwa njia ya Uwekezaji pekee. Yaani anaweza kusajili kampuni ndani ya Zanzibar na kampuni hiyo kwa sababu umesajili wa Zanzibar itaruhusiwa kumiliki ardhi (zingatia kwamba Kampuni ni mtu kisheria, yaani legal person).
Kwanini alitumia maneno yaliyoeleweka kwako peke yako huku akijua viwango vya uelewa vya watanzania kulingana na elimu wanayowapa? Huoni kwamba kwa sikio la tatu kuna jambo haliko sawa linafanywa kimchongomchongo?
 
Nimepitia kurasa kadhaa katika mitandao ya kijamii kama facebook, magroup ya whatsapp na Jamii forums watu wakiijadili kauli ya Rais WA Zanzibar Dr. Hussein Ally Mwinyi alioitoa akikisisitiza kwamba Mtanzania Bara haruhusiwi kumiliki ardhi KISIWANI Zanzibar.
Wengi wa wachangiaji wameonekana kutokubaliana na kauli yake na wengine wakienda mbali zaidi kuulaani Muungano kuonekana hauna maana wakilinganisha na ukweli kwamba Mzanzibar anaruhusiwa kumiliki ardhi Tanganyika kwa Kadri ya uwezo wake.
Suala ka Mungano ni suala mtambuka linalohitaji Mijadala yake binafsi. Na naomba nikiri na mimi kwamba ni kweli Muungano una changamoto zake nyingi tu, inazohitaji hekima za viongozi wetu katika kuzitatua. Leo sitozungumzia sana huko, nitajikita hapa kwenye suala la ardhi tu.
Kwanza ifahamike Ardhi si jambo la Muungano. Naam, si suala ambalo nchi hizi mbili Tanganyika na Zanzibar zimekubaliana kushare kwa mujibu wa ule mkataba wa Muungano uliosainiwa na wazee wetu.
Hii ndio kusema kwamba kila upande wa Muungano una ardhi yake na sheria zake binafsi zinazoongoza na kusimamia matumizi ya ardhi kwao.
Na ni kwa sababu hiyo Zanzibar ina wizara yake ya ardhi kama ilivyo kwa serikali ya Muungano(ilipaswa iwe serikali ya Tanganyika).
Sasa basi, kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya Zanzibar, sharti la mtu kumiliki ardhi ni lazima awe Mzanzibar wa kuzaliwa(Zanzibariz by birth), wakati huku kwetu Bara sharti ni kuwa Mtanzania tu inatosha kumilikishwa ardhi,bila kujali huo utanzania wako umeupataje, almuhimu iwe ni uraia halali kwa mujibu wa sheria zetu (wa kuzaliwa au wa kuomba).
Sheria zetu hutungwa kwa malengo, kila sheria ikitungwa hutungwa kwa sababu, ikilenga jambo au dhamira fulani.
Zanzibar ina eneo la Ukubwa wa kilomita za mraba 1650(wengine wanasema 2000),wakati Tanzania Bara Ukubwa wake ni kilomita za mraba 945,000 ikiwa ndio nchi yenye ardhi kubwa zaidi kuliko nchi zote za Afrika ya nashariki.
Sasa kutokana na udogo wa ardhi ya Zanzibar ndipo ilipokubaliwa kwamba isiwe sehemu ya Muungano na sheria rafiki itungwe ili kuilinda ardhi hiyo.
Kumbuka ndani ya kilomita hizo za mraba 2000 (ambazo ndo ndogo hata kwa Jiji la Dodoma kwa zaidi ya kilomita za mraba 600), Wanzanzibar wapatao 1,500,000/-(kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012)wanahitaji ardhi kwa matumizi ya makazi, maeneo ya wazi, viwanda na Uwekezaji, ardhi ya akiba, ardhi ya mkakati wa kimazingira kuhifadhi uoto wa asili na misitu, huduma za jamii(hospital na mashule/vyuo) na kilimo japo cha kiwango cha kawaida(small scale farming).
Ukigawanya Ukubwa wa ardhi iliyopo na idadi yao unakuta ardhi waliyonayo ni ndogo sana. Na wasiwasi upo kutokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kutokana na kasi waliyonayo kwenye kuzaliana ambayo inatajwa ni asilimia 4 kwa kila mwaka(wenzetu wanazaliana sana) , kuna kila dalili Kuna wakati ardhi ya Zanzibar haitowatosha hata Wazanzibar wenyewe. Kwa kuangalia mbali ililazimu kuweka mazingira ya kuilinda ardhi Yao.
Pengine kama haitodhuru Sasa wangepaswa kuanzia kujipanga kugawa ardhi kwa kwenda juu, yaani hati ya ardhi itolewe juu ya nyumba iliyokwishajengwa.
Sasa nirudi kwa kauli ya Rais Hussein Mwinyi, inawezekana maneno aliyotumia hakueleweka, lakini alichomaanisha ni kwamba kwa ardhi ya Zanzibar kila mtu ataruhusiwa kumiliki lakini kwa utaratibu tofauti na unaotumika huku kwetu Bara.
Kwa maana kwamba, kwa wa Zanzibar kumiliki ardhi watatakiwa kuthibitisha uzanzibar wao kwa kuzaliwa. Na kwa asiye MZanzibar atamiliki ardhi kwa njia ya Uwekezaji pekee. Yaani anaweza kusajili kampuni ndani ya Zanzibar na kampuni hiyo kwa sababu umesajili wa Zanzibar itaruhusiwa kumiliki ardhi (zingatia kwamba Kampuni ni mtu kisheria, yaani legal person).
Na kwa kusajili kampuni bila shaka dhamira ya mwenye kampuni ni kuwekeza sehemu fulani, Ndiyo kauli ya Mheshimiwa Rais Mwinyi ilitokea hapo.
Hivyo ndivyo ilivyo hata huku kwetu Bara, licha ya haki ya kumiliki kuwa wazi kwa Mtanzania yeyote, lakini umiliki huo una Kikomo, unaweza kupewa miaka 33,66 au 99, Yote ndo yale yale tu, ni sawa na Abdallah kumuita Dulla tu. Muda huo ukiisha ardhi si yako inarudi kwa Rais. BADO umekodishwa hujamilikishwa.
Lakini tusijisahau, sababu wanayoitumia Zanzibar kutoruhusu wasio wa Zanzibar kumiliki ardhi, kimsingi Ndiyo tunayo tumia na sisi kukataa kufungua mipaka ya jumuiya ya Afrika ya nashariki kwenye ardhi kwa kuhofia Wakenya kuja kuitwaa ardhi yetu yote(jambo ambalo binafsi silikubali)
Kwako Mtanzania Bara, kama unataka kumiliki ardhi Zanzibar ni rahisi sana, nenda kasajili kampuni, utapata kibali cha kufanya biashara Zanzibar, then tumia kampuni yako kuomba ardhi, utapewa bila kinyongo.

Muungano udumuuuuuuuuView attachment 2204064

Ungeweka habari yako vizuri iwe rahisi kusomeka, mfano "paragraphs" e.t.c
 
Nimepitia kurasa kadhaa katika mitandao ya kijamii kama Facebook, magroup ya WhatsApp na Jamii Forums watu wakiijadili kauli ya Rais WA Zanzibar Dr. Hussein Ally Mwinyi alioitoa akikisisitiza kwamba Mtanzania Bara haruhusiwi kumiliki ardhi KISIWANI Zanzibar.

Wengi wa wachangiaji wameonekana kutokubaliana na kauli yake na wengine wakienda mbali zaidi kuulaani Muungano kuonekana hauna maana wakilinganisha na ukweli kwamba Mzanzibar anaruhusiwa kumiliki ardhi Tanganyika kwa Kadri ya uwezo wake.

Suala ka Mungano ni suala mtambuka linalohitaji Mijadala yake binafsi. Na naomba nikiri na mimi kwamba ni kweli Muungano una changamoto zake nyingi tu, inazohitaji hekima za viongozi wetu katika kuzitatua. Leo sitozungumzia sana huko, nitajikita hapa kwenye suala la ardhi tu.

Kwanza ifahamike Ardhi si jambo la Muungano. Naam, si suala ambalo nchi hizi mbili Tanganyika na Zanzibar zimekubaliana kushare kwa mujibu wa ule mkataba wa Muungano uliosainiwa na wazee wetu.

Hii ndio kusema kwamba kila upande wa Muungano una ardhi yake na sheria zake binafsi zinazoongoza na kusimamia matumizi ya ardhi kwao.

Na ni kwa sababu hiyo Zanzibar ina wizara yake ya ardhi kama ilivyo kwa serikali ya Muungano(ilipaswa iwe serikali ya Tanganyika).
Sasa basi, kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya Zanzibar, sharti la mtu kumiliki ardhi ni lazima awe Mzanzibar wa kuzaliwa(Zanzibariz by birth), wakati huku kwetu Bara sharti ni kuwa Mtanzania tu inatosha kumilikishwa ardhi,bila kujali huo utanzania wako umeupataje, almuhimu iwe ni uraia halali kwa mujibu wa sheria zetu (wa kuzaliwa au wa kuomba).

Sheria zetu hutungwa kwa malengo, kila sheria ikitungwa hutungwa kwa sababu, ikilenga jambo au dhamira fulani.

Zanzibar ina eneo la Ukubwa wa kilomita za mraba 1650(wengine wanasema 2000),wakati Tanzania Bara Ukubwa wake ni kilomita za mraba 945,000 ikiwa ndio nchi yenye ardhi kubwa zaidi kuliko nchi zote za Afrika ya nashariki.

Sasa kutokana na udogo wa ardhi ya Zanzibar ndipo ilipokubaliwa kwamba isiwe sehemu ya Muungano na sheria rafiki itungwe ili kuilinda ardhi hiyo.

Kumbuka ndani ya kilomita hizo za mraba 2000 (ambazo ndo ndogo hata kwa Jiji la Dodoma kwa zaidi ya kilomita za mraba 600), Wanzanzibar wapatao 1,500,000/-(kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012)wanahitaji ardhi kwa matumizi ya makazi, maeneo ya wazi, viwanda na Uwekezaji, ardhi ya akiba, ardhi ya mkakati wa kimazingira kuhifadhi uoto wa asili na misitu, huduma za jamii(hospital na mashule/vyuo) na kilimo japo cha kiwango cha kawaida(small scale farming).

Ukigawanya Ukubwa wa ardhi iliyopo na idadi yao unakuta ardhi waliyonayo ni ndogo sana. Na wasiwasi upo kutokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kutokana na kasi waliyonayo kwenye kuzaliana ambayo inatajwa ni asilimia 4 kwa kila mwaka(wenzetu wanazaliana sana), kuna kila dalili Kuna wakati ardhi ya Zanzibar haitowatosha hata Wazanzibar wenyewe. Kwa kuangalia mbali ililazimu kuweka mazingira ya kuilinda ardhi Yao.

Pengine kama haitodhuru Sasa wangepaswa kuanzia kujipanga kugawa ardhi kwa kwenda juu, yaani hati ya ardhi itolewe juu ya nyumba iliyokwishajengwa.

Sasa nirudi kwa kauli ya Rais Hussein Mwinyi, inawezekana maneno aliyotumia hakueleweka, lakini alichomaanisha ni kwamba kwa ardhi ya Zanzibar kila mtu ataruhusiwa kumiliki lakini kwa utaratibu tofauti na unaotumika huku kwetu Bara.

Kwa maana kwamba, kwa wa Zanzibar kumiliki ardhi watatakiwa kuthibitisha uzanzibar wao kwa kuzaliwa. Na kwa asiye MZanzibar atamiliki ardhi kwa njia ya Uwekezaji pekee. Yaani anaweza kusajili kampuni ndani ya Zanzibar na kampuni hiyo kwa sababu umesajili wa Zanzibar itaruhusiwa kumiliki ardhi (zingatia kwamba Kampuni ni mtu kisheria, yaani legal person).

Na kwa kusajili kampuni bila shaka dhamira ya mwenye kampuni ni kuwekeza sehemu fulani, Ndiyo kauli ya Mheshimiwa Rais Mwinyi ilitokea hapo.

Hivyo ndivyo ilivyo hata huku kwetu Bara, licha ya haki ya kumiliki kuwa wazi kwa Mtanzania yeyote, lakini umiliki huo una Kikomo, unaweza kupewa miaka 33,66 au 99, Yote ndo yale yale tu, ni sawa na Abdallah kumuita Dulla tu. Muda huo ukiisha ardhi si yako inarudi kwa Rais. BADO umekodishwa hujamilikishwa.

Lakini tusijisahau, sababu wanayoitumia Zanzibar kutoruhusu wasio wa Zanzibar kumiliki ardhi, kimsingi Ndiyo tunayo tumia na sisi kukataa kufungua mipaka ya jumuiya ya Afrika ya nashariki kwenye ardhi kwa kuhofia Wakenya kuja kuitwaa ardhi yetu yote(jambo ambalo binafsi silikubali)

Kwako Mtanzania Bara, kama unataka kumiliki ardhi Zanzibar ni rahisi sana, nenda kasajili kampuni, utapata kibali cha kufanya biashara Zanzibar, then tumia kampuni yako kuomba ardhi, utapewa bila kinyongo.

Muungano udumuuuuuuuu

View attachment 2204064
Tunakuelewa. Ila ninavyoelewa mzanzibari mkazi ni mtanzania yeyote aliyeishi zanzibar mfululizo kwa miaka mitano. Haijalishi hata kama ametokea bara. Je huyo nae hawezi kumiliki ardhi au ni wale tu kabila yao wazanzibari hata kama wanaishi bara na wanamiliki ardhi huku bara?
 
Nimepitia kurasa kadhaa katika mitandao ya kijamii kama Facebook, magroup ya WhatsApp na Jamii Forums watu wakiijadili kauli ya Rais WA Zanzibar Dr. Hussein Ally Mwinyi alioitoa akikisisitiza kwamba Mtanzania Bara haruhusiwi kumiliki ardhi KISIWANI Zanzibar.

Wengi wa wachangiaji wameonekana kutokubaliana na kauli yake na wengine wakienda mbali zaidi kuulaani Muungano kuonekana hauna maana wakilinganisha na ukweli kwamba Mzanzibar anaruhusiwa kumiliki ardhi Tanganyika kwa Kadri ya uwezo wake.

Suala ka Mungano ni suala mtambuka linalohitaji Mijadala yake binafsi. Na naomba nikiri na mimi kwamba ni kweli Muungano una changamoto zake nyingi tu, inazohitaji hekima za viongozi wetu katika kuzitatua. Leo sitozungumzia sana huko, nitajikita hapa kwenye suala la ardhi tu.

Kwanza ifahamike Ardhi si jambo la Muungano. Naam, si suala ambalo nchi hizi mbili Tanganyika na Zanzibar zimekubaliana kushare kwa mujibu wa ule mkataba wa Muungano uliosainiwa na wazee wetu.

Hii ndio kusema kwamba kila upande wa Muungano una ardhi yake na sheria zake binafsi zinazoongoza na kusimamia matumizi ya ardhi kwao.

Na ni kwa sababu hiyo Zanzibar ina wizara yake ya ardhi kama ilivyo kwa serikali ya Muungano(ilipaswa iwe serikali ya Tanganyika).
Sasa basi, kwa mujibu wa sheria ya ardhi ya Zanzibar, sharti la mtu kumiliki ardhi ni lazima awe Mzanzibar wa kuzaliwa(Zanzibariz by birth), wakati huku kwetu Bara sharti ni kuwa Mtanzania tu inatosha kumilikishwa ardhi,bila kujali huo utanzania wako umeupataje, almuhimu iwe ni uraia halali kwa mujibu wa sheria zetu (wa kuzaliwa au wa kuomba).

Sheria zetu hutungwa kwa malengo, kila sheria ikitungwa hutungwa kwa sababu, ikilenga jambo au dhamira fulani.

Zanzibar ina eneo la Ukubwa wa kilomita za mraba 1650(wengine wanasema 2000),wakati Tanzania Bara Ukubwa wake ni kilomita za mraba 945,000 ikiwa ndio nchi yenye ardhi kubwa zaidi kuliko nchi zote za Afrika ya nashariki.

Sasa kutokana na udogo wa ardhi ya Zanzibar ndipo ilipokubaliwa kwamba isiwe sehemu ya Muungano na sheria rafiki itungwe ili kuilinda ardhi hiyo.

Kumbuka ndani ya kilomita hizo za mraba 2000 (ambazo ndo ndogo hata kwa Jiji la Dodoma kwa zaidi ya kilomita za mraba 600), Wanzanzibar wapatao 1,500,000/-(kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012)wanahitaji ardhi kwa matumizi ya makazi, maeneo ya wazi, viwanda na Uwekezaji, ardhi ya akiba, ardhi ya mkakati wa kimazingira kuhifadhi uoto wa asili na misitu, huduma za jamii(hospital na mashule/vyuo) na kilimo japo cha kiwango cha kawaida(small scale farming).

Ukigawanya Ukubwa wa ardhi iliyopo na idadi yao unakuta ardhi waliyonayo ni ndogo sana. Na wasiwasi upo kutokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kutokana na kasi waliyonayo kwenye kuzaliana ambayo inatajwa ni asilimia 4 kwa kila mwaka(wenzetu wanazaliana sana), kuna kila dalili Kuna wakati ardhi ya Zanzibar haitowatosha hata Wazanzibar wenyewe. Kwa kuangalia mbali ililazimu kuweka mazingira ya kuilinda ardhi Yao.

Pengine kama haitodhuru Sasa wangepaswa kuanzia kujipanga kugawa ardhi kwa kwenda juu, yaani hati ya ardhi itolewe juu ya nyumba iliyokwishajengwa.

Sasa nirudi kwa kauli ya Rais Hussein Mwinyi, inawezekana maneno aliyotumia hakueleweka, lakini alichomaanisha ni kwamba kwa ardhi ya Zanzibar kila mtu ataruhusiwa kumiliki lakini kwa utaratibu tofauti na unaotumika huku kwetu Bara.

Kwa maana kwamba, kwa wa Zanzibar kumiliki ardhi watatakiwa kuthibitisha uzanzibar wao kwa kuzaliwa. Na kwa asiye MZanzibar atamiliki ardhi kwa njia ya Uwekezaji pekee. Yaani anaweza kusajili kampuni ndani ya Zanzibar na kampuni hiyo kwa sababu umesajili wa Zanzibar itaruhusiwa kumiliki ardhi (zingatia kwamba Kampuni ni mtu kisheria, yaani legal person).

Na kwa kusajili kampuni bila shaka dhamira ya mwenye kampuni ni kuwekeza sehemu fulani, Ndiyo kauli ya Mheshimiwa Rais Mwinyi ilitokea hapo.

Hivyo ndivyo ilivyo hata huku kwetu Bara, licha ya haki ya kumiliki kuwa wazi kwa Mtanzania yeyote, lakini umiliki huo una Kikomo, unaweza kupewa miaka 33,66 au 99, Yote ndo yale yale tu, ni sawa na Abdallah kumuita Dulla tu. Muda huo ukiisha ardhi si yako inarudi kwa Rais. BADO umekodishwa hujamilikishwa.

Lakini tusijisahau, sababu wanayoitumia Zanzibar kutoruhusu wasio wa Zanzibar kumiliki ardhi, kimsingi Ndiyo tunayo tumia na sisi kukataa kufungua mipaka ya jumuiya ya Afrika ya nashariki kwenye ardhi kwa kuhofia Wakenya kuja kuitwaa ardhi yetu yote(jambo ambalo binafsi silikubali)

Kwako Mtanzania Bara, kama unataka kumiliki ardhi Zanzibar ni rahisi sana, nenda kasajili kampuni, utapata kibali cha kufanya biashara Zanzibar, then tumia kampuni yako kuomba ardhi, utapewa bila kinyongo.

Muungano udumuuuuuuuu

View attachment 2204064
Hizo ni siasa tu, yeyé baba yake mbona anamiliki ardhi na si Mzanzibari wa kizaliwa ? Mzanzibari mkaazi na uraisi wakampa. Ukikaa miaka miwili au mitatu (sikumbuki vizuri) una haki ya kitambulisho cha Mzanzibari mkaazi na kumiliki ardhi na kugombea nafasi za ubunge / uwakilishi n.k.
Siasa na uhalisia ni vitu viwili tofauti.
 
Yule Mkurugenzi wa NHC anayeshauri watu wageni wamiliki ardhi ili tuendeleze Uwekezaji naona kwanza atuombee Zanzibar na tupate kwanza Ruksa !!!!

Akili za hawa viongozi wanazijua wenyewe....
 
Back
Top Bottom