Kufutwa kwa kodi kwenye bodaboda".

Kufutwa kwa kodi kwenye bodaboda".

Jamani si wameondolewa kulipa road licence tu?
Kodi ya mapato ipo pale pale!

Kodi ya mapato kwani wanalipa bei gani?

Wenye magari pia wanalipa kodi ya mapato

Ni kuwabagua wananchi kwa kiwacanya wengie walipe kodi na wengine wasilipe.

Manake imagine.mfanyakazi mwenye kigari chake.mtumba analopa road licence na PAYE kama kawaida.
Onabidi wajengewe utamaduni wa kulipa kodi hata kwa kidogo wakipatacho. Manake mfanyakazi w kima.cha.chini naye analipa kodi

Kiujimla ni.uamuzi wa hovyo ambao hatukuutegemea kutoka kwa Mgimwa na wataalam wake
 
Kila mtu anapaswa kulipa kodi. Na kodi ya boda boda inapaswa kusimamiwa na serikali za mitaa. Yaani waziri wa serikali ya muungano anajadili boda boda badala ya kudhibiti mfumko wa bei, kupanua wigo wa kodi na kuongeza pato la taifa. Hana habari boda boda haitakuwa mambo ya muungano na tukiunda serikali ya Tanganyika nayo sio mambo ya serikali ya muungano?
 
Waziri wa Fedha jana alitamka kundoa Kodi kwenye Bodaboda , kwa lengo la kuongeza Ajira zaidi kwa Vijana .
Nnachokifahamu ,Opportunity yoyote ya Ajira hutengenezwa kwa kuzingatia Mazingira Mazuri ya ajira husika , ikiwa ni Pamoja na Bima ya Ajira Hiyo .Tumesikiliza na tunaendelea kusikiliza kila kukicha vyombo vya habari vikiripoti Majanga juu ya hizi pikipiki bila serikali kuchukua hatua yeyote kunusuru nguvu kazi ya Taifa ,ambapo vijana ndio idadi kubwa waliojikita kwnye kazi hii.
Je Serikali inatengeneza ajira , au ! Mm naona Serikali inajitengenezea Walemavu tu ,na kuua nguvu kazi ya Taifa. Serikali jipangeni kutafuta ajira zenye Mantiki na Zenye Mazingira Mazuri kwa Wananchi , acheni kufaanya Maisha ya Watu Mchezo wa Kisiasa.
Mandella naona hujatafakari ni nini kinachoendelea kwenye nchi hii na kwa jinsi huku tunapoelekea! Elewa kwamba kwa sasa hivi asilimia kubwa ya vijana waliojiajiri kwenye sekta binafsi hususani ya Bodaboda ni vijana ambao hawajamaliza hata elimu ya msingi! Na isitoshe ndio asilimia kubwa ya vijana ambao wameshafikisha umri wa kujiandikisha na kupiga kura (Namaanisha miaka 18) vijana hawa kwanza kabisa wana usongo wa maisha! na ndio asilimia kubwa ya wapiga kura! wazee wetu wameshazeeka na hawana hamasa na mashamsham ya kushabikia mambo ya siasa kwakua umri nao umeshawatupa mkono!

Tuje kwenye bajeti hii ya juzi ambayo bado haijajadiliwa bungeni kua baadhi ya bajeti fulani zitapita au zisipite! kwangu mimi kuhusiana na bajeti hii inayohusu kodi zote zinazohusu Bodaboda kufutiwa kodi zote ni kiini macho kwa sera za CCM! Kutafuta kura mwaka 2015! hii tunasema waendesha Bodaboda wamepakwa mafuta kwa mgongo wa chupa, lakini baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 kama CCM wana matarajio ya kushinda uchaguzi basi tutegemee kuanzia Bodaboda mpaka waendesha baiskeli lazima walipe kodi!

Huu ni mtazamo wangu lakini time will tell! Wananchi kaeni macho na CCM!
 
Back
Top Bottom