Kufungua radio station

Kufungua radio station

ingekuwa nataka radio ya kibiashara inahitaji garama kubwa na kulipia mapato ila ni radio ya kijamii sana sana mziki ila ya dini alfu pia ndio nimeomba ushauri sijaamua kurusha matangazo
Mkuu hata iwe radio gani,tcra lzm ,wao ndio wanaotoa leseni hkn njia ya mkato
 
wadau wa jf habari nina transmitter ya fm radio wat 500 ila nahitaji kufungua radio station ya umbali kias tu,angalau ifikie ata mitaa 5 pekee ila sifahamu kama tcra watakubali maana ela ya kulipia trca sina wala gharama za serikali pia sina ela wadau naomba mnishauri nifanye vp ili niweze fungua radio ? na pia ni umbali upi trca wanaukubali ambao sitaulipia na radio ni kwaajili ya mziki tu msaada wadau kwenye ili

Mkuu nakupongeza kuwa na wazo hili zuri la biashara. Ninavyoelewa serikali hairuhusu kufanya unachotaka kufanya, bali inaruhusu kwa kutoa vibali(leseni) kulingana na uhitaji wako. Kwa maelezo haya uliyoandika ni dhahiri kuwa kwasasa haujakidhi vigezo vya kupata leseni hizo. Unachoweza kufanya ni kuviendeleza vigezo ulivyonavyo ili vizae zingine na kukamilika kufikia vigezo vyote. Nitakusaidia maelezo ya hili bure nitumie ujumbe inbox.

Chakushauri tu, tufanye biashara ya hiyo transmitter. Ni aina gani?
 
Mada Nzuri Kama Hii Ambayo Soon Italeta Kiwanda Haraka Kwa Maendeleo Ya Taifa Letu
Yupo Member Mmoja Anatoa Huduma Za Ushauri Na Hata Kufunga Radio, Acha Nimwite Kwenye Hii Thread Yako Aje Atoe Madini

CC: Radio Producer
Asante kwa wito mkuu
 
ingekuwa nataka radio ya kibiashara inahitaji garama kubwa na kulipia mapato ila ni radio ya kijamii sana sana mziki ila ya dini alfu pia ndio nimeomba ushauri sijaamua kurusha matangazo
Usifikiri kwamba uthibiti uliopo kwenye kufungua radio ni swala la kodi peke yake; lahasha. Ni usalama pia, pamoja na kujua unataka kuwasiliana nini na jamii kupitia mziki wako. Wewe unadhani kazi ya mziki ni kuburudisha tu? Unaelimisha, unahamasisha, unaongeza hamasa na kupitia mziki huo huo kitu kinachoitwa social action kinaweza tokea. Ndio maana itabidi ufanye usajili, uwe na katiba, na mengineyo. Hata hivyo, shughuli yeyote inayochukua muda wako na nguvu kazi ni project (Mradi) tayari. Kwahiyo dhamira yako hiyo ni nzuri endapo utaendesha mambo kitaaluma zaidi.
 
Yaani unataka uwe unapigia disco tu , utachukua wateja wawezio bure na wao wanalipia tcra
 
Nadhani umefanya vizuri kulileta hapa nakushauri kama uko hapa mjini nenda tcra ukutane na mkurugenzi wa masafa uombe ushauri,niliwahi kwenda wakati naanzisha online radio kabla ya sheria kubadirishwa nilihudumiwa vizuri sana na mambo yao yalikuwa wazi,njoo tuzungumze ndo kauli yao na juzi walizindua kauli mbiu mpya ya kupinga rushwa nadhani utapata msaada,kikubwa wasikilize kwanza wao kuliko mwingine yeyote maana zama zimebadilika.
 
wadau wa jf habari nina transmitter ya fm radio wat 500 ila nahitaji kufungua radio station ya umbali kias tu,angalau ifikie ata mitaa 5 pekee ila sifahamu kama tcra watakubali maana ela ya kulipia trca sina wala gharama za serikali pia sina ela wadau naomba mnishauri nifanye vp ili niweze fungua radio ? na pia ni umbali upi trca wanaukubali ambao sitaulipia na radio ni kwaajili ya mziki tu msaada wadau kwenye ili
Kwa swala la radio, kuna vigezo vyao ukienda kusajiri wanakupa form za kujaza, kuna vijedwali vyako vya kujaza kutokana na majukunu ya radio unayotaka kuanzisha, gharama hazikwepeki kwasababu ni sheria zilizowekwa, wala sio uonevu, timiza vigezo vyako uanzishe radio yako uruke hewani
 
Kupata leseni TCRA kuna utaratibu wake kama ni redio ya kibiashara utatakiwa kusubiri kitu kinaitwa INVITATION TO APPLY (ITA) huwa hao jamaa wanatangaza gazetini kualika wanaotaka kufungua redio sehemu husika then mna bid kwa kupeleka maandiko huko kwao ikiwemo michanganuo ya biashara yako na cash flow zako...utaratibu kwa mujibu wa sheria kama utawin hiyo process ya ITA maombi yako yatapelekwa kwa Waziri husika wa Mawasiliano atatathmini kama upewe leseni au laah!!!

Kwa redio za kijamii kidogo mchakato hauko complicated mkiwa kikundi ambacho ni hai na kina lengo husika kama wakulima nk mnaweza kuomba leseni ya redio ya kijamii.

Ila hakuna masafa ya bure hata ingekuwa kutangazia ndani kwako...ushauri kama hii michakato huiwezi uza tu hiyo transmita watu wengi wanazihitaji hasa wenye redio...wanazihitaji kama back up hasa hiyo ya Watts 500...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom