Mwingereza
JF-Expert Member
- Jan 21, 2014
- 1,111
- 2,752
Kama Mwana CCM, tena mbunge mstaafu anayetetea kiti chake kwa mara nyingine, napata wakati mgumu sana jimboni ninapokutana na wapiga kura na washabiki wa CCM. Inaonekana wazi kabisa kwamba tunapoteza wanachama wetu wengi mno, kitendo ambacho kitatutia aibu ifikapo kipindi cha uchaguzi. Majuzi hapa Morogoro CCM mkoa, niliwakuta wana CCM kama 7 wamekaa wanasikiliza hotuba ya Lissu aliyoitoa BUNDA kutumia simu ya mkononi. Walimalizia kwa kuweka vichwa chini, na kudai tutawajibu, ila tutajibu nini?
Moto wa Tindu Lissu umezua mijadala mizito nchini kote, na wanachama wa CCM walio wengi wanataka CCM tuwajibu CHADEMA kwa hoja, matokeo yake tunawajibu kwa hoja mfu na propaganda za hovyo. Hata mtoto wa Darasa la kwanza hawezi kukubali hoja ya kuvunjwa kwa Flyover na kuuza Vyuma kama Skrepa.
Mbaya zaidi ni kuvurugwa kwa Tasnia ya habari. Kuwanyima hawa watu nafasi ya kuonekana kwenye vyombo vya habari imewapa umaarufu mkubwa sana na huruma ya kutisha kutoka kwa wananchi, na imeonekana wazi kabisa kwamba serikali ya CCM imekuwa ikiwaonea.Kitendo hiki kimewafanya wananchi walio wengi wahache kabisa kuangalia TV na kuamia kenye mitandao ya kijamii, WhatsApp, Facebook na Instagram ambako habari za Lissu zinasambaa kwa kasi ya ajabu. Kimataifa ndio usiombe, vyombo vya kimataifa inaonyesha serikali ya CCM ilivyo Serikali ya hovyo.
Mbaya zaidi ambayo inahitaji kukemewa ni hii ya kuwafanyia hawa watani wetu wa jadi fujo. Hii ni mbaya sana. Inahitaji kukemewa kwa nguvu zote na wahusika wote wakamatwe na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria, pamoja na polisi walioshiriki kwenye hizi vurugu. Vinginevyo dhana ya CCM kuwatumia polisi itakuwa imehalalishwa kwa maana hiyo, uchaguzi wa October utakuwa ni Raia Vs. PoliciCCM
Moto wa Tindu Lissu umezua mijadala mizito nchini kote, na wanachama wa CCM walio wengi wanataka CCM tuwajibu CHADEMA kwa hoja, matokeo yake tunawajibu kwa hoja mfu na propaganda za hovyo. Hata mtoto wa Darasa la kwanza hawezi kukubali hoja ya kuvunjwa kwa Flyover na kuuza Vyuma kama Skrepa.
Mbaya zaidi ni kuvurugwa kwa Tasnia ya habari. Kuwanyima hawa watu nafasi ya kuonekana kwenye vyombo vya habari imewapa umaarufu mkubwa sana na huruma ya kutisha kutoka kwa wananchi, na imeonekana wazi kabisa kwamba serikali ya CCM imekuwa ikiwaonea.Kitendo hiki kimewafanya wananchi walio wengi wahache kabisa kuangalia TV na kuamia kenye mitandao ya kijamii, WhatsApp, Facebook na Instagram ambako habari za Lissu zinasambaa kwa kasi ya ajabu. Kimataifa ndio usiombe, vyombo vya kimataifa inaonyesha serikali ya CCM ilivyo Serikali ya hovyo.
Mbaya zaidi ambayo inahitaji kukemewa ni hii ya kuwafanyia hawa watani wetu wa jadi fujo. Hii ni mbaya sana. Inahitaji kukemewa kwa nguvu zote na wahusika wote wakamatwe na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria, pamoja na polisi walioshiriki kwenye hizi vurugu. Vinginevyo dhana ya CCM kuwatumia polisi itakuwa imehalalishwa kwa maana hiyo, uchaguzi wa October utakuwa ni Raia Vs. PoliciCCM